Naomba ushauri baada ya matokeo ya mdogo wangu

Naomba ushauri baada ya matokeo ya mdogo wangu

Ndugu samahani,najua mko bize na kutafuta mkate wa siku! Nilikua naomba ushauri wenu baada ya matokeo kutoka Mdogo wangu yeye amepata kama ifuatavyo katika tahasusi yake ya CBG.

GS.D .CHEM . E BIOS .E NA GEO. D BAM F.
DIVISON 3 YA 14.

Je, ningependa mnishauri akasomee kitu gani? Na je, anaweza kupata nafasi ya chuo kikuu kweli kwa hapa Tanzania private hasa hasa maana kwa ufaulu ninavouona sidhani kama kwa serikali anaweza kutoboa. Natanguliza shukurani.

NB: Vyuo gani anaweza kujaribu kuomba?

Sent from my TECNO BD4j using JamiiForums mobile app
Nisikilize mimi achana na wote waliocomment mwanzo, akapige diploma ya macho (Optometry) ipo Mvumi Dodoma, au diploma ya Radiology. Usisahau kuja kunishukuru.
 
Nisikilize mimi achana na wote waliocomment mwanzo, akapige diploma ya macho (Optometry) ipo Mvumi Dodoma, au diploma ya Radiology. Usisahau kuja kunishukuru.
Huu uzi uishie hapa! Nakazia akasome radiology diploma inatolewa vyuo kama muhimbili, bugando!
 
Aende akasome diploma kozi za afya especially Radioraphy pale MUHAS au CUHAS
 
Wanadai hizo kozi wako wachache.Sijui wajukuu zao watasoma kitu gani kipya ambacho kitakuwa na watu wachache
Watanzania wanawazaga diploma za afya tu, ndio uwezo unapoishia. Wanapenda kazi mteremko, za kupelekwa kama wanafunzi wa kujaguliwa sekondari. Basi serikali inafurahii sana kuwa na kundi kubwa la watu wa aina hii. Wao watasona kozi za kukutawala.
 
Watanzania wanawazaga diploma za afya tu, ndio uwezo unapoishia. Wanapenda kazi mteremko, za kupelekwa kama wanafunzi wa kujaguliwa sekondari. Basi serikali inafurahii sana kuwa na kundi kubwa la watu wa aina hii. Wao watasona kozi za kukutawala.
Mazingira ya Watanzania wengi ni hohe hahe, atleast kozi za afya unaweza bahatika kupenya bila connection kuliko hizo zenu za tabaka la watawala
 
Wanaoajiriwa saivi wengi diploma bachelor unakuta wachache wanahitajika kwa ushahidi angalia majina yaliyotoka hivi karibuni .

Kingine akienda diploma kusomea anachokipenda akamaliza anaweza kufanya kazi kisha baadae akajiendeleza either kwa mkopo au kwa kusomeshwa na kampuni husika .

Kingine ni ujuzi anapata experience ya kazi mapema sana so muache aende diploma kama atapenda
na huko akasomee nn

Sent from my TECNO BD4j using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom