Naomba ushauri: Ameniambia "Baba wa nini?"

Naomba ushauri: Ameniambia "Baba wa nini?"

Nilikuwa nataka nikajitambulishe kwa wazazi wa huyu binti sasa katika kumhoji napaswa kupeleka zawadi gani? Nikaona ananiorodheshea zawadi za mama yake tu.

Nikamuulize zawadi za baba je? Akajibu "baba wa nini wewe? Wewe fuata maelekezo ninayokupa"

Nimeshindwa kuelewa maana alisema baba yake yupo hai
Kwa hiyo alivyomaliza tu kukuambia fuata maelekezo nayokupa wala hukuhoji zaidi ukakimbilia JF?
 
Wakina single mama wengine wanapandikiza chuki kwa watoto wao wanawachukia wazee wao bure hadi ukubwani.
 
Sasa mbona tunatidhana aisee 😒
We nawe;-

1.Kila mtoto anamjua mama take ila baba Huwa tunaonyeshwa TU na kumzoea kama baba hasta kama sio baba halisi!Kuna siri anajua huyo dem!
2.kina baba wote tunalea watoto wakiwa wakubwa wanasema "hakuna kama mama"hata usomeshe vipi,hata umtengenezee life kiasi gani "Hakuna kama mama"ndio shukrani atakayokupa,atakua anapiga stori na mama yake za kufurahisha sana akija kwako anatoa taarifa TU na Hana time anasepa!!

So sad kwetu kina baba!!
 
1. Inawezekana kalelewa na mama pekee kitu ambacho kimemuathiti. Anahitaji huruma japo itabidi umvumilie sana maana hakuwahi kuona mwanaume akiishi na mama yake hiyo kwako kuna vita ataona vipya na pengine kukupinga kuwa haiwezekani.

2. Kama kalelewa na baba na mama, basi kashapewa sumu na mama yake, kesha kuwa mbinafsi hafai tena
 
Fuata maelekezo taratiibu, ukijifanya mjuaji utamshindwa mapemaaa
Ni bora ahaoji sasa ivi ili kama ni kushindwa ashindwe kabisa kabla hajala hasara. Lingekua jambo la kawaida asingekuja hapa kushirikisha wakuu. Ni tabia za kibinafsi na ni mbaya sana, hivyo bora aelewe sababu ili ajiridhishe kama binti yupo sawa kufanya hivyo
 
Wakina single mama wengine wanapandikiza chuki kwa watoto wao wanawachukia wazee wao bure hadi ukubwani.
Hapa ndio mimi hujisemea kuwa mwanangu tunalea wote mimi na mke wangu. Hizi mambo za kumzalisha kisha unamwacha na kuwa unamtumia pesa za mtoto, man yeye ndio atajivisha u contawa. Kila ukituma pesa akimnunulia chochote mtoto anajua mama ndio hununua kakikua ni kitendo cha kuambiwa baba yako hakukujali nilihangaika peke yangu na kwakuwa mtoto kweli hakukuona ukimletea hata kiatu kwanini asiamini. Siku hizi wanaume wameenda mbali zaidi, hata mkiwa kwenye ndo mnaishi wote hakuna mambo ya kumpa pesa chumbani, mpe sebleni mbele ya watoto na uwe clear matumizi yake inaepusha mengi sana mbeleni. Wenzetu janja janja sana
 
Yaani swali la kujibiwa na huyo mwana mama tunaulizwa sisi, sometimes wana jukwaa tunabebeshwa mizigo isiyo yetu
 
Ipo siku atakuambia bila wewe bado anaweza kuishi vizuri tuu
 
Back
Top Bottom