Naomba taarifa kuhusu soko la mbaazi

Naomba taarifa kuhusu soko la mbaazi

allen creo

Member
Joined
May 12, 2016
Posts
13
Reaction score
4
Habari wanakilimo wenzangu,
Mwenye ushauri na soko la mbaazi na wanunuzi wa bei nzuri wa hili zao,Shamba langu lipo morogoro.
 
Una kiasi gani je mzigo upo mjini tayari au bado shamba ?
 
Una kiasi gani je mzigo upo mjini tayari au bado shamba ?
bado shamba ,mkuu, kiasi natarajia kuvuna mweiz wa 7 mwishoni najaribu kupata uhakika wa soko kabisa,niko na jamaa yangu tulipiga eka 15
 
Morogoro njia ya kwenda kilosa kijiji cha Msowero kitongoji kinaitwa Kumbilwa
hizo zinanunuliwa sana na wahindi wa kampuni ya TATA msimu ni mwez wa sita na wasaba mara nyingi kama wataka dalali haya kama wataka direct yote sawa lakini wengi wanatumia dalali ili kuepusha usumbufu na kuwa na uhakika . ntakupa namba za watu kama ukihitaji ( EXPORT,AY,AFRISIAN) Baadhi ya kampuni zinazo nunua
 
hizo zinanunuliwa sana na wahindi wa kampuni ya TATA msimu ni mwez wa sita na wasaba mara nyingi kama wataka dalali haya kama wataka direct yote sawa lakini wengi wanatumia dalali ili kuepusha usumbufu na kuwa na uhakika . ntakupa namba za watu kama ukihitaji ( EXPORT,AY,AFRISIAN) Baadhi ya kampuni zinazo nunua
Ntashkuru sana mkuu, nifowadie namba za hao jamaa,Thanks kwa msaada
 
HII KAMA POUA SANA, HONGERENI WAZEE KWENYE MSAFARA WA MAMBA KENGE NAO WAPO
 
Mbaazi inalipa lakini inatakiwa usiwe na chini ya Ton 10 ikiwa zaidi ndio poa zaidi kwani inakua rahisi kusafirisha mzigo pekeyako bira kuchanganya na mtu mwingine Soko ni Mohamed Enterprises hakuna haja ya Darari hapo nenda Pugu Pale Pugu Road wananunua bila shida
 
Mbaazi inalipa lakini inatakiwa usiwe na chini ya Ton 10 ikiwa zaidi ndio poa zaidi kwani inakua rahisi kusafirisha mzigo pekeyako bira kuchanganya na mtu mwingine Soko ni Mohamed Enterprises hakuna haja ya Darari hapo nenda Pugu Pale Pugu Road wananunua bila shida
Nashkuru kwa taharifa yako mkuu
 
wana jamii nataka kulima mbaazi Morogoro sasa nahitaji information juu ya kilimo hiki naomba aanae weza kujua ni wapi nitapata maelekezo sahihi juu ya kilimo hiki naomba anisaidie
 
Habari ndugu wana jamiiforum, ni mara yangu ya kwanza kupost ila ni msomaji mzuri hasa hii kolamu ya kilimo na ufugaji,. Naombeni msaada kwa anaejua hasa Mtaalamu wa kilimo au Mtu ambaye ameshafanya kilimo cha Mbaazi, Je ekari moja unaweza kupata Magunia mangapi ikiwa utalima kiusahihi? Pls nisaidie maana nimelima ufuta mara tatu mfululizo lakini mafanikio ni madogo now nataka kulima mbaazi ufuta nipumzike kwanza., thanks
 
Mkuu nimeingia hapa mara kadhaa naona uzi wako unanyanyasika nikona niingilie kati.
Kikubwa wakulima waliowengi japo tanzania ni kubwa ila naamini zaidi ya 90% hua hawalimi mbaazi peke yake ndio maana unakosa majibu.Waliowengi huchanganya mbaazi kwenye shamba la mahindi na mara nyingi unakuta kipaumbele kinakua mahindi sio mbaazi.Hivyo mbaazi hupandwa ndani ya shamba la mahindi kwa uchache.
Hivyo inakua ngumu watu kukupa takwimu heka moja inaweza toa mbaazi kiasi gani kwani waliowengi huchanganya mbaazi ndani ya shamba la mahindi.
Japo hujapata jibu lakini naamini nimepunguza pressure kidogo mkuu
 
Asante sana mkuu kwa maelezo yako. ni kweli wengi wanafanya hivyo ndio maana nikajaribu kutafuta mtu humu kama alisha lima mbaazi peke yake, but ntajaribu kuwasiliana na wataalamu wa SARI kule arusha nadhani watanipa jibu.. Asante sana mkuu
 
Asante sana mkuu kwa maelezo yako. ni kweli wengi wanafanya hivyo ndio maana nikajaribu kutafuta mtu humu kama alisha lima mbaazi peke yake, but ntajaribu kuwasiliana na wataalamu wa SARI kule arusha nadhani watanipa jibu.. Asante sana mkuu
Thnx a lot nd al da best!
 
Kuna jamaa yangu amelima mbaaz pekeake anadai kwa wastan hk 1 inaweza kutoa gunia 7 za mbaaz
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom