tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,803
- 18,230
Wakuu heshima zenu,
Wandugu kuna rafiki yangu mmoja ameachishwa kazi kinyume cha sheria, naomba msaada wenu wa kisheria jinsi anavyoweza kupata haki zake.
Huyu bwana alikuwa akifanya kazi kwenye kiwanda kimoja cha kutengeneza nondo jijini Dar. Kwa bahati mbaya, akiwa kazini, alikatwa kiganja cha mkono wake wa kulia na mashine za kiwandani. Juhudi za madaktari kuurudishia mkono wake ziligonga ukuta. Alitibiwa jeraha la mkono uliopatwa na ajali na baada ya kupona alirejea kazini. Kwa kuwa hakuweza kufanya kazi zake kwa ufanisi kama ilivyokuwa mwanzo, mabosi wake walimhamishia kwenye kitengo kingine ndani ya kiwanda kwa muda. Lakini cha ajabu ni kwamba alipewa muda wa miezi mitatu kuomba kazi nyingine ndani ya kiwanda(endapo zitatangazwa) au nje ya kiwanda na endapo asingeweza kupata kazi yoyote basi angekuwa terminated from employment.
Baada ya kuisha miezi mitatu hakuna kazi yoyote aliyoipata ndani au nje ya kiwanda. Ikabidi atimuliwe bila huruma na bila kulipwa chochote zaidi ya kugharamiwa mkatibabu ya mkono wake.
Je, hii ni halali kisheria? Je, ni utaratibu gani wa kisheria ambao ulikiukwa hapa? Sheria za nchi zinasemaje kuhusu mtu aliyepata ulemavu kazini kama huyu ndugu yetu? Wadau naomba msaada wa kisheria katika hili na jinsi tunavyoweza kumsaidia huyu jamaa apate haki zake za kimsingi na kisheria.
Asante sana.
Wandugu kuna rafiki yangu mmoja ameachishwa kazi kinyume cha sheria, naomba msaada wenu wa kisheria jinsi anavyoweza kupata haki zake.
Huyu bwana alikuwa akifanya kazi kwenye kiwanda kimoja cha kutengeneza nondo jijini Dar. Kwa bahati mbaya, akiwa kazini, alikatwa kiganja cha mkono wake wa kulia na mashine za kiwandani. Juhudi za madaktari kuurudishia mkono wake ziligonga ukuta. Alitibiwa jeraha la mkono uliopatwa na ajali na baada ya kupona alirejea kazini. Kwa kuwa hakuweza kufanya kazi zake kwa ufanisi kama ilivyokuwa mwanzo, mabosi wake walimhamishia kwenye kitengo kingine ndani ya kiwanda kwa muda. Lakini cha ajabu ni kwamba alipewa muda wa miezi mitatu kuomba kazi nyingine ndani ya kiwanda(endapo zitatangazwa) au nje ya kiwanda na endapo asingeweza kupata kazi yoyote basi angekuwa terminated from employment.
Baada ya kuisha miezi mitatu hakuna kazi yoyote aliyoipata ndani au nje ya kiwanda. Ikabidi atimuliwe bila huruma na bila kulipwa chochote zaidi ya kugharamiwa mkatibabu ya mkono wake.
Je, hii ni halali kisheria? Je, ni utaratibu gani wa kisheria ambao ulikiukwa hapa? Sheria za nchi zinasemaje kuhusu mtu aliyepata ulemavu kazini kama huyu ndugu yetu? Wadau naomba msaada wa kisheria katika hili na jinsi tunavyoweza kumsaidia huyu jamaa apate haki zake za kimsingi na kisheria.
Asante sana.