Dada etu ana matokeo mazuri tuu form six, hvyo atakuwa na uwanja mpana wa kuchagua kozi nzuri, kabla ya hili ebu twende huku kwanza.
Nin kimesababisha kudisco? Watu wengi sana huwa wanashindwa kumaliza elimu zao za vyuo ilihali walikuwa na matokeo mazur form six sababu ya kwenda kusomea kozi wasizozipenda, unapochagua kozi husiyoipenda ni rahis sana kushindwa, maana unakosa msukumo kutoka ndan wa kukufanya uweze kukomaa na masomo yako.
Linapotokea jambo baya kama hilo la kudisco... vijana wengi linawatengenezea "self doubt" mtu anapoteza kujiamin, na mwngne anaweza akakataa kabisa kurud shulen, watu wengi wanapishana mda wanaotumia kupita kwenye mpito wa hali hizo mbili, watu waliowazunguka wana mchango mkubwa sana katika mda watakaoutumia watu hawa kutoka kwenye anguko na kusimama tena.
Ndugu yako anapopatwa na jambo kama hilo, inabid umuaminishe alishindwa hyo kozi kwakuwa haukuwa mpango wa MUNGU awe mwalim, kuna kitu kizuri zaid ameandaliwa, katika kipind hiki mtembeze kwa ndugu, jamaa na marafiki waliofanikiwa kwenye kozi nyingine ambazo kwa utash wako unaziona nzuri, ndan ya mda mchache ataanza kutaman na kupenda kuwa kama flani, maana watu wengi huwa tunapenda kozi flani kutokana na exposure tulizonazo kwa watu husika.
Baada ya wewe kutoa msaada wa kimazingira, mpe nafas achague kozi anayoiona ye inafaa, kimsingi, atachagua kati ya za watu wale uliomu expose nao.
Baada ya kufanya hayo, kijana ataenda kupiga shule vizur bila woga wa kushindwa na akiwa na mapenz yoote na anachosomea.
Sent using
Jamii Forums mobile app