Naomba kuelimishwa kidogo juu ya hili

Naomba kuelimishwa kidogo juu ya hili

Carleen

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2018
Posts
8,592
Reaction score
29,545
Hi guys,
Habari zenu, natumaini mpo salama japo najua hali si shwari, kwani hofu ya corona imetawala kila pande ya dunia, tuendelee kuomba Mungu atulinde wakati huo huo tukifuata maelekezo yote yatolewayo na wizara ya afya..!!

Naomba nitoe hili jambo, katika mfumo wa swali naamini kuna wajuvi wa kutosha humu na watanisaidia barabara katika hili,

Kuna siku asubuhi tulikuwa tupo pahala na baadhi ya wamama watu wazima kama wawili na mkaka mmoja, kila mmoja kaingia mule ndani kwa ajili ya shughuli zake, akaingia mkaka mwingine, alivyomkuta mwenzie pale ndani, akamuambia 'bora hata nimekuona, twende tukapate breakfast, njaa inaniuma mno', na kweli yule mwenzie akamsapoti vyema kabisa kuwa na yeye njaa inamuuma hasa,

Wale wamama wakawashangaa, mmoja akamuambia 'wewe si tumekuozesha tu mwaka Jana? Umeshaanza kutoka nyumbani bila kuandaliwa chai mapema hivyo.!?'
Akacheka, 'hamna bwana nimemuacha amelala sitakagi kumsumbua'.! Mwenzie akachangia kuwa wanatoka wote na mkewe alfajiri na mapema, huo muda wa kuandaa chai asubuhi utatoka wapi.?

Wale wamama wakawasema sema pale, si busara mwanaume mwenye mke kutoka nyumbani bila kupata chochote asubuhi bwaana, wakaongea ongea pale, wale wakaka wakaenda zao.! Kiukweli hata sikuchangia chochote, niliona kabisa hayanihusu, wale wamama wakanigeukia eti 'binti hivyo ndivyo tunavyowafunza mkaishi na waume zenu? Nikajifanya pale 'ujue mama kila familia ina taratibu zake na pia wana makubaliano yao, hivyo kila familia inafanya kile inachoona wao wapo sahihi'.!

Sikutaka kutia comment yoyote katika lile sababu sikujiona kama nipo kwenye position ya ku-judge ama niko na 'eksipiriensi' ya kutosha katika masuala hayo yawahusuyo wanandoa, japo kiukweli sijawahi ona mtu aondoke nyumbani kwa Mama Carleen hata awe mgeni wa kuwahi basi la alfajiri eti atoke bila kutia kinywani chochote kitu, na ndivyo nilivyokuzwa nikaaminishwa hiyo ndiyo busara.!

Je, kiukhalisia kwa kuzingatia mfumo mzima wa maisha yetu ya kudamka hata kabla ya jogoo kuwika hiki kitu kipo applicable? Na kama ni ndiyo, Je, kwa ambao hawafanyi hili, hivi ndiyo inamaanisha kuwa kuna mahali tunafeli sisi kama wanawake?? Japo wanaume wetu baadhi wanaonesha kuridhika na hili, hivii ni kweli wanaume wetu mmeridhika au ndiyo zile za, wacha tu tulisongeshe gurudumu la maisha..??
 
Yaani kidume kabla ya kuoa nilikuwa najitengenezea chai mwenyewe alafu eti nimeoa nitegemee mke au nigombane nae kisa hajaamka kunitengenezea chai... Hilo kwangu wa sio ishu

Ishu kwangu mie aninyime papuchi tuu. Hapo ndio ajihesabie hana chake.
 
Nikifurahishwa nadamka saa kumi na moja chai tayari ikiwa kinyume kwakweli ni ngumu kupata hiyo mood ya kuamka mapema kuandalia mtu chai

Kwa wageni inategemeana na aina ya mgeni
Hahaha..!
Kwahiyo kumuandalia hubby chai ni mpaka ufurahishwe seriously Noelia? Ukiboeka apambane na njaa yake.?
 
Mimi bhana asubuhi nikiamka kama hajaandaa fresh tu naamsha zangu ingawa huwa anaadaa breakfast,but kama hamna mwenye mishe atakayewahi kuamka ndo anaandaa na wala siyo kesi.

Ila unamwachaje mwenzako ndani unaenda kunywa chai yeye hajanywa halafu unarudi nyumbani,ni tabia mbaya na ubinafsi

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Yaani kidume kabla ya kuoa nilikuwa najitengenezea chai mwenyewe alafu eti nimeoa nitegemee mke au nigombane nae kisa hajaamka kunitengenezea chai... Hilo kwangu wa sio ishu

Ishu kwangu mie aninyime papuchi tuu. Hapo ndio ajihesabie hana chake.
Hili pia nilitaka kufahamu, kwahiyo kumbe kwa baadhi ya wanaume hili siyo tatizo kabisa? Wanawake wa zama hizi tumebahatika kwakweli.!
 
Mimi bhana asubuhi nikiamka kama hajaandaa fresh tu naamsha zangu ingawa huwa anaadaa breakfast,but kama hamna mwenye mishe atakayewahi kuamka ndo anaandaa na wala siyo kesi.

Ila unamwachaje mwenzako ndani unaenda kunywa chai yeye hajanywa halafu unarudi nyumbani,ni tabia mbaya na ubinafsi

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
Nimekuelewa first para Mr. Viol, ndiyo maana wanawake wameamua kulizembea hili suala sababu wanaume wao wenyewe hawajali, kizazi chetu jamani.!!
Hapana siyo uchoyo, Ni unakuta wapo mihangaikoni si kwamba wanakunywa chai na kurudi nyumbani hapana!
 
Hili pia nilitaka kufahamu, kwahiyo kumbe kwa baadhi ya wanaume hili siyo tatizo kabisa? Wanawake wa zama hizi tumebahatika kwakweli.!

Mie katika vitu ambavyo sitagombana kabisa na mke wangu ni suala la kunipikia.
Asipopika wala sina shida huyo kwa mama ntilie wangu buku 2 nimeshiba na wala hamna kuosha vyombo.
Akipika nitaheshimu nitakula chakula chake ila sijui nianze kumuuliza kwa nini hujapika hiho kwangu haipo.

Chakula changu muhimu ni papuchi basi.
 
Kwakweli nisiwe mnafiki mpaka 'nifurahishwe' ndo nakuwa mtoto mzuri
Hahaha..!
Kwahiyo na baba wa watu kajiridhikia zake akikuta bila bila anajua Leo nimeharibu.?
Wanaumeeee, chukueni point muhimu hapa tafadhali..!
 
Kama anakunywa chai akiwa kwenye mishe hapo sawa
Nimekuelewa first para Mr. Viol, ndiyo maana wanawake wameamua kulizembea hili suala sababu wanaume wao wenyewe hawajali, kizazi chetu jamani.!!
Hapana siyo uchoyo, Ni unakuta wapo mihangaikoni si kwamba wanakunywa chai na kurudi nyumbani hapana!

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
 
Mie katika vitu ambavyo sitagombana kabisa na mke wangu ni suala la kunipikia.
Asipopika wala sina shida huyo kwa mama ntilie wangu buku 2 nimeshiba na wala hamna kuosha vyombo.
Akipika nitaheshimu nitakula chakula chake ila sijui nianze kumuuliza kwa nini hujapika hiho kwangu haipo.

Chakula changu muhimu ni papuchi basi.
Ukipata wazo la kuoa Mr. Mzabzab unishirikishe, huwezi jua naweza nikafanya maamuzi magumu maana si kwa 'wepesi' huo kaah', familia itakula kwa mama 'nitilie' mpaka ikome..!!
 
Kama anakunywa chai akiwa kwenye mishe hapo sawa

♡♤Life belongs to all who struggle for it♤♡♧
Ndiyo Mr. Viol ni kwenye mizunguko yao huko.!
 
Yaani mtu ninawahi alfajiri nisubiri chain jamani?Hayo ni Maisha ya zamani sana kwa sasa wala hayawezekani tena.kwa WK end sawa ila kwa WK days ni ngumu!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Basiii na sisi waolewaji tunashukuru Mungu, tunasema kheri..!
Maisha yamebadilika sana siku hizi nimeamini.!
 
hivii ni kweli wanaume wetu mmeridhika au ndiyo zile za, wacha tu tulisongeshe gurudumu la maisha..??
Nimependa hapa jinsi ulivyomalizia. Ok kukujibu tu ni kwamba mfumo wenyewe wa maisha unasupport kuwa hivyo kwa vile hakuna mwanaume anaependa kutoka nyumbani bila kuandaliwa kifungua kinywa na mkewe ampendae.

Wengi wetu ni waajiriwa na hutakiwa tufike vibaruani mapema hivyo tukisema tusubirie kuandaliwa kifungua kinywa tunaweza kuchelewa kazini pia ukizingatia kama usafiri mtu anaotumia ni wa public.

Waajiri (Mabosi) pekee zao ndio wanaosubiri kuandaliwa vifungua vinywa na wake zao tena usikute hata mabosi wengine pia wanahisi watachelewa vibaruani mwao hivyo hujikuta wakipata vifungua kinywa maofisini mwao.
Nawasilisha....




ᴮᵉʷᵃʳᵉ ᵒᶠ ᵗʰᵉ ᶜᵒᵛⁱᵈ ⁻ ¹⁹ [emoji377]
 
Back
Top Bottom