CARDLESS
JF-Expert Member
- Apr 2, 2017
- 7,786
- 15,732
Nikiona andiko lako natulia kulitafakari, always unaandika vitu vya msingi, iwe unasifia au kuponda, hongera sana.Kama asingeomba msamaha na kuisimamia ile kauli yake, then, Ndugai yule, ndiye ambaye angeweza kuamua liwalo na liwe, lakini yule Ndugai aliyeufyata na kuwa mdogo kama piriton, kwa kujinyenyekeza kwa the executive, hawezi tena kuamua lolote liwe, naamini by now barua ya kuachia ngazi iko tayari.
Baada ya kuomba ule msamaha batilifu uliokataliwa, hana turufu yoyote, he has to go!.
It's true ana mengi, ila hawezi kutoa siri zozote!, ingekuwa ni kutoa siri, angetoa Lowassa, hivyo usitegemee Ndugai atatoa siri yoyote.
Japo hapa kwenye hili la 2025, Ndugai amesingiziwa tuu, lakini hawezi kujibishana na boss wake, the boss is always right, hata kama boss kashika karatasi nyeupe, akamuuliza Ndugai,
Boss: "Hii karatasi ni rangi gani?"
JYN: " Nyeupe"
Boss: "Hii nyeupe gani?, au una color blindness?, hii si nyeusi!"
JYN: "Sorry boss, mwanzo niliona vibaya, kumbe ni nyeusi".
Ndugai kwa sasa si lolote, sii chochote, hana lolote jingine isipokuwa kufungasha. Amepata ajali mbaya kisiasa, amepigwa dafrao, hawezi kuinuka tena!.
P