Nani wanamshauri rais TZ? - Lazima tutafakari hili...

Mjadala ni kuhusu washauri wa rais,awamu zilizopita wanafahamika i mean there is transparency kwenye uteuzi wa washauri wa rais,kama unakumbuka kuna kipindi ambacho kingunge alikuwa mshauri wa rais juu ya mambo ya siasa.Uteuzi ni jambo moja lakini inapofikia mahali rais anakuja na majibu mepesi kwa maswala mazito watz inabidi tuhoji weledi wa washauri wake.Hivi watoto walalamike na baba ulalamike nani atakuwa msaada ndani ya nyumba?that house should collapse.

Mimi nimeongelea mjumuisho wa Matatizo yetu kwa ujumla, kwamba tunafikiri kwamba Bw.Kikwete au sijui Bw.Pinda ndio tatizo, kumbe sio, tatizo NI SISI Watanzania kwa ujumla wetu, yaani Utamaduni wetu, na anayoyafanya Bw.Kikwete sio mapya, na yangefanywa na Mtanzania karibu yoyote yule aliyezaliwa na kukulia TZ, kwa maana ndiyo Utamaduni wetu unavyotukuza, hivyo kutegemea kwamba kuna lolote jipya litakuja kutoka kwa Viongozi ambao wametokana na jamii hii yetu ni kujidanganya na tutasubiri mpaka Yesu atakaporudi, na huyo Kiongozi hatotokea!

 
Sasa mambo yanazidi kuwa mabaya sababu mshauri wake mkuu alishatutokaga.
 
Mimi nimeongelea mjumuisho wa Matatizo yetu kwa ujumla, kwamba tunafikiri kwamba Bw.Kikwete au sijui Bw.Pinda ndio tatizo, kumbe sio, tatizo NI SISI Watanzania kwa ujumla wetu, yaani Utamaduni wetu, na anayoyafanya Bw.Kikwete sio mapya, na yangefanywa na Mtanzania karibu yoyote yule aliyezaliwa na kukulia TZ, kwa maana ndiyo Utamaduni wetu unavyotukuza, hivyo kutegemea kwamba kuna lolote jipya litakuja kutoka kwa Viongozi ambao wametokana na jamii hii yetu ni kujidanganya na tutasubiri mpaka Yesu atakaporudi, na huyo Kiongozi hatotokea!


Wewe nawe unaandika andika tu hujua hata unachoandika au nadhan hujaelewa kinachosemewa hapa. Basi kama mleta mada alikwenda mbali fananisha washauri wa Marais wetu waliopita au angalia Hotuba za Mkapa na huyo unaemtetea hapa.
 
Wewe nawe unaandika andika tu hujua hata unachoandika au nadhan hujaelewa kinachosemewa hapa. Basi kama mleta mada alikwenda mbali fananisha washauri wa Marais wetu waliopita au angalia Hotuba za Mkapa na huyo unaemtetea hapa.

S
imtetei mtu yoyote yule, bali nasema Bw.Kikwete, Bw. Mkapa, Bw.Pinda n.k wamezaliwa na kukulia katika hii jamii yetu hivyo, hawawezi kuwa tofauti na sisi, na yote wanayoyafanya wengi wetu tungefanya hivyo hivyo tu, hakuna cha Hotuba nzuri wala mbaya, wote wameshirikiana kwa namna moja au nyingine kutuuza na kuuza nchi yetu, na bado wataendelea kufanya hivyo mpaka tuje tubadilike kama jamii, hata kama wakiajili mwandika Hotuba kutoka sijui Mwezini nini Marekani!

 

S
imtetei mtu yoyote yule, bali nasema Bw.Kikwete, Bw. Mkapa, Bw.Pinda n.k wamezaliwa na kukulia katika hii jamii yetu hivyo, hawawezi kuwa tofauti na sisi, na yote wanayoyafanya wengi wetu tungefanya hivyo hivyo tu, hakuna cha Hotuba nzuri wala mbaya, wote wameshirikiana kwa namna moja au nyingine kutuuza na kuuza nchi yetu, na bado wataendelea kufanya hivyo mpaka tuje tubadilike kama jamii, hata kama wakiajili mwandika Hotuba kutoka sijui Mwezini nini Marekani!


Kwa hiyo hata washauri wa JK Nyerere ni sawa na Wa JK?
 
Kwa hiyo hata washauri wa JK Nyerere ni sawa na Wa JK?

Siwajui mimi washauri wa Bw.Nyerere! Ila ninachokijua ni kwamba, maisha yetu hayajabadilika, haijalishi tuna Kiongozi gani au ana shauriwa na nani, au sijui anaandikiwa Hotuba gani, maisha bado ni Mabaya kuanzia Raisi wa kwanza mpaka wa sasa hivi, hakuna afadhali yoyote ile! tumekuwa tukipigika na bado tunaendelea kupigika tu, hivyo Ushauri wa Hotuba mzuri au mbaya haujabadilisha maisha yetu kwa vyovyote vile zaidi ya kuzidi kuyaadidimiza!
 
ukihoji utendaji wa rais utaambiwa rais si mtu pekee(personally)bali ni taasisi....kwa maana hiyo dhana ya rais kushauriwa iko pale pale..haiepukiki...upende usipende...wengine watakwambia rais hawezi kujua kila kitu kinachotokea TZ...na ndio maana ana wawakilishi kila sehemu(including mawaziri)....all these people are there to work on behalf of the president...pamoja na kwamba yeye ndie mwenye final say ofcourse....

Naelewa hilo kabisa lakini wanakosea kitu kimoja. Raisi ana final say isiyokuwa na "Vision." Kwa nini nasema hivyo?

Marais wote waliopita baada ya Baba wa Taifa, hakuna hata mmoja anayeingia madarakani na vision. Baba wa Taifa ameacha legacy kwa kuwaunganisha watanzania wote kuwa kitu kimoja, priceless. Baada yake kila alimfuatia ameacha negative legacy.

Angalia suala la umeme. Toka kipindi cha Mwinyi umeme unatuchezea danadana. Kama Raisi yeyote angelipa hiliswala kipau mbele as his first and foremost on his to do list, sasa hivi tungekuwa tunamsimulia utendaji kazi wake, biashara na viwanda vingeshamiri, isingekuwa kero kwa wawekezaji na ajira zingeongezeka. Lakini kila mwaka, kila kiongozi ni njia mpya ya ulaji.
 
Hata mimi hili limenikera sana. La Raisi kulalamika badala ya kuonyesha njia. Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa kuongoza ni kuonyesha njia. Kwa mfano raisi anapolalamikia wakristo na waislamu badala ya kusimama na katiba ya nchi, hii inanikera. Mwovu ni mwovu mbele ya sheria bila kijali dini yake. Uovu ni uovu kisheria bila kujali dini. Waliochoma makanisa ni waovu bila kujali dini zao. Walioua viongozi wa kidini ni waovu bila kujali dini zao. Raisi angetakiwa aoneshe wazi msimamo huo na kuamuru vyombo vyake vya dola kuwasaka na kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria mara moja. Mkristo mwovu akamatwe na muislamu mwovu akamatwe bila kujali dini zao. Lakini kulalamika kuwa hawa vitabu vyao vitakatifu vimenajisiwa kana kwamba sasa wana uhalali wa kuchoma makanisa ni kitu ambacho hakikutarajiwa kutamkwa na Raisi. Halafu malalamishi ya raisi yanasababishwa na hali ya kutaka kubalance kati ya Wakristo na Waislamu. Hali ya kutaka kuwapendeza wote. Hii inaleta taswira ya kuwa naye yumo katika kundi mojawapo la wanamigogoro hawa! Uovu ni uovu tu. Raisi anatakiwa kuupiga vita kwa kuwa yeye ni msimamizi wa Katiba ambayo ndiyo msingi wa Sheria inayompa haki kila raia bila kujali dini. Sasa wabunge wanalalamika, mashehe wanalalamika, maaskofu wanalalamika, vijana wanalalamika, wanawake wanalalamika, wafanyakazi wanalalamika, wanafunzi vyuoni wanalalamika na kila mmoja analalamika halafu hata na Raisi naye analalamika! Nani atuonyeshe njia sasa? Kama kuna washauri wa Raisi, wana hatia ya kumfanya raisi wetu awe analalamika. MSAIDIENI RAISI WETU JAMANI!
 
Tatizo ni kwamba unafanya makosa yaleyale ambayo siku zote tunayafanya, umetolea mfano wa Marekani kwamba tuige wanavyofanya, bila kutambua kwamba Marekani na Tanzania ni jamii 2 zenye Tamaduni 2 tofauti, hivyo linalofanyika Marekani na kuonekana kama ni kitu cha kawaida haliwezi kufanyika kwetu!

Anayoyafanya yote Bw.Kikwete ni sawa kabisa na yanaendana na Utamaduni wetu na ndio jinsi tulivyo, na Watz karibu wote ambao wamezaliwa na kukulia TZ wangefanya hivyo hivyo, kama wangepata hiyo nafasi, na ndio maana hakuna jipya ktk kwa Viongozi wetu!

Unaongelea kuhusu ushauri, we tazama maisha yetu ya kawaida tu, Je tunaweza kutatua matatizo hata madogo tu? Hata magomvi tu ya kifamilia mpaka Wazee wasafiri kutoka vijijini ndio waje watupatanishe, na wote tuko hivyo!
Je Marekani watu wako hivyo?

Jiulize ni lini mara ya mwisho ulishawahi kumshauri Mtanzania wa kawaida na akakusikiliza? Au lini mtu alikufwata akakuomba ushauri wa jambo la maana?
Mtanzania wa kawaida anajua kila kitu, yeye ni mtaalamu wa kila kitu, sasa kwa nini Bw.Kikwete awe tofauti? Kwani Bw.Kikwete ametokea wapi?



Uko unajua sana, Mbongo ni mtaalam wa kila kitu, sasa hivi kila mtu akitazama kifusi cha jengo lililoporomoka anatoa Comments eti Zege lilikuwa hafifu, mtaani akionekana mtu kakonda Naked eyes zinasema kakanyaga /Papa au dudu washa. Wabongo ni wajuaji sana ndo maana Mungu kawaletea Rais mwenye taaluma yao, Si unakumbuka ulivozama Meli Zanzibar kafika tu eneo la tukio anaanza kutoa Ushauri wa Kitaalam kwa Madaktari umuhimu wa kuanza kupima DNA za maiti bila kuuliza mazingira yepi yanaruhusu hali hiyo!
 
Kwa hiyo hata washauri wa JK Nyerere ni sawa na Wa JK?

Hotuba ni makelele tu cha msingi ni utendaji, wote ni Zero ndo maana tangu uhuru hatujawahi kutoka kwenye top 5 ya nchi masikini!
 
Tumechoka na hoja za udogo wa raisi. Huyu ndivyo alivyo, hajawahi kuwa mwingine mwone kabadilika. Hajawahi kufanya lolote la maana na hana record yoyote ya ufanisi katika miaka yake si yaurasi tu bali hata kule nyuma. Kilichomsaidia ni uenzetu. Sas aleo mnataka abadilike kwa mbinu gani?

If he is doing any good or bad, that is not his problem. Kazi kwenu mliomchagua pamoja na kujua historia zake. Sasa leo mnalalamika nini? Na sana sana akikugundua unamchallenge usishangae fimbo ya kisasi ikakuandama maana the man is merceless in revenging.

Mtindo wake ni ule ule. Babu seya na watoto wake wote wakatiwa hatiani kwa makosa makubwa ambayo yasingemwacha huru mwalimu aliyekuwa akiwapeleka watoto kule.

Usishangae na hili la ku ignore magaidi wa mwamsho, kina ilunga, watesi wa ulimboka, mauaji ya mwangosi, arusha, morogoro, kibanda n.k halafu dola inafuatilia tuhuma za rwakatare na ku support ni visasi kwa ajli ya viongozi wa Chadema kuvalia njuga masuala ya ufisadi wakati na yeye akiwa ni miongoni mwa watuhumiwa..

Mungu tunusuru.
 

S
imtetei mtu yoyote yule, bali nasema Bw.Kikwete, Bw. Mkapa, Bw.Pinda n.k wamezaliwa na kukulia katika hii jamii yetu hivyo, hawawezi kuwa tofauti na sisi, na yote wanayoyafanya wengi wetu tungefanya hivyo hivyo tu, hakuna cha Hotuba nzuri wala mbaya, wote wameshirikiana kwa namna moja au nyingine kutuuza na kuuza nchi yetu, na bado wataendelea kufanya hivyo mpaka tuje tubadilike kama jamii, hata kama wakiajili mwandika Hotuba kutoka sijui Mwezini nini Marekani!

issue si kuandikiwa hotuba.....issue ni utendaji wa rais....na jinsi ya kuuboresha...
 
Tumechoka na hoja za udogo wa raisi. Huyu ndivyo alivyo, hajawahi kuwa mwingine mwone kabadilika. Hajawahi kufanya lolote la maana na hana record yoyote ya ufanisi katika miaka yake si yaurasi tu bali hata kule nyuma. Kilichomsaidia ni uenzetu. Sas aleo mnataka abadilike kwa mbinu gani?

If he is doing any good or bad, that is not his problem. Kazi kwenu mliomchagua pamoja na kujua historia zake. Sasa leo mnalalamika nini? Na sana sana akikugundua unamchallenge usishangae fimbo ya kisasi ikakuandama maana the man is merceless in revenging.

Mtindo wake ni ule ule. Babu seya na watoto wake wote wakatiwa hatiani kwa makosa makubwa ambayo yasingemwacha huru mwalimu aliyekuwa akiwapeleka watoto kule.

Usishangae na hili la ku ignore magaidi wa mwamsho, kina ilunga, watesi wa ulimboka, mauaji ya mwangosi, arusha, morogoro, kibanda n.k halafu dola inafuatilia tuhuma za rwakatare na ku support ni visasi kwa ajli ya viongozi wa Chadema kuvalia njuga masuala ya ufisadi wakati na yeye akiwa ni miongoni mwa watuhumiwa..

Mungu tunusuru.
..hamna mtanzania mwenye kuijali nchi(majority)asiyejua kuwa ali mess up kumchagua kuwa rais...hilo linajulikana...issue ni tunafikaje kwenye next election kwa mtindo huu??....maana kwa mambo yanavyokwenda...kweli naiona 2015 iko mbali sana....
 
Kwa kuhitimisha..labda ifike sasa mahaliswala la rais kuwa na washauri iwekwe rasmi kwenye katiba yetu mpya...na mambo ya msingi ya kutolea ushauri kwa rais yaainishwe....yakiwemo maswala ya kisiasa....kidini....kiuchumi..kiafya..n.k..n.k..

Kwa style maoni ya hiyo Katiba Mpya yanavyokusanywa na aina ya maoni yanayokusanywa; usishangae kuona vitu vya msingi kama hivi HAVIZINGATIWI!!

Lakini pia ikumbukwe; kwani USHAURI NI DAWA UNAYOLAZIMISHWA UNYWE???? Mshauri akikwambia HARIBU HIKI (japo nichema) na wewe ukakubali; nani wa kulaumiwa??? KIONGOZI ASIYESHAURIKA HASHAURIKI TUU hata kama washauri wake ni WEREVU KWA KIWANGO CHA JUU na wanamwambia ukweli!!!! SHERIA HATA KAMA KALI KIASI GANI, KAMA HAITEKELEZWI itakiwavyo nikujaza makbrasha ya serikali tuuu!!!!
 
..hamna mtanzania mwenye kuijali nchi(majority)asiyejua kuwa ali mess up kumchagua kuwa rais...hilo linajulikana...issue ni tunafikaje kwenye next election kwa mtindo huu??....maana kwa mambo yanavyokwenda...kweli naiona 2015 iko mbali sana....

Na kuna kila dalili ya serikali ku impose similar candidate kwa sababu hali inavyoonyesha sasa, jamaa anataka ku eliminate kama siyo ku eradicate kila brain inayoona yenye uwezo wa kuinfluence changes. Atapinga mabadiliko kwa gharama yoyote kwa sababu anapenda sifa na asingependa aweke record inayoonyesha alipwaya hadi system mpya ikaingia na pia hatapenda kuona utawala unaomfuata unamnyooshea vidole kwa makosa makubwa aliyoyafanya wakat wa utawala wake.

Kwa hayo aanatumia vizuri muda wake liobaki wa kujenga mazingira yakuendelea kumiliki nchi hata baada ya kustaafu. Akiwaondoa wote wanao mquestion, akabakiza wapambe wanafiki na waoga, nani atasimamia maslahi ya watanzania maskini na wa jinga?

Mungu tusaidie.
 
Kwa style maoni ya hiyo Katiba Mpya yanavyokusanywa na aina ya maoni yanayokusanywa; usishangae kuona vitu vya msingi kama hivi HAVIZINGATIWI!!

Lakini pia ikumbukwe; kwani USHAURI NI DAWA UNAYOLAZIMISHWA UNYWE???? Mshauri akikwambia HARIBU HIKI (japo nichema) na wewe ukakubali; nani wa kulaumiwa??? KIONGOZI ASIYESHAURIKA HASHAURIKI TUU hata kama washauri wake ni WEREVU KWA KIWANGO CHA JUU na wanamwambia ukweli!!!! SHERIA HATA KAMA KALI KIASI GANI, KAMA HAITEKELEZWI itakiwavyo nikujaza makbrasha ya serikali tuuu!!!!
..this may be the case with our president....maana bado sijaamini kuwa hawapo watu wa kumshauri jinsi ya kuyakabili mambo yanayotokea.....mbona kina mzee Mwinyi waliweza??....mzee Mwinyi alikuwa na sifa moja kubwa sana(pamoja na mapungufu yake)...yaani kusikiliza ushauri wa washauri wake....na ndio maana aliweza kufanya better kwenye baadhi ya mambo....hususani hili la udini(ukimlinganisha na JK)...Hivi inawezekana kweli JK hakai hata na hawa wazee wakaongea?????au kina Mkapa??....au hata ex PMs..ambao wana experience za nyuma (kama imeshindikana kuwa na official presidential advisors)
 
Tatu

"Raisi anajua kusoma na kuandika. Raisi ana macho na masikio. Kwa maana hiyo anaweza kupambanua maswala muhimu yanayowagusa wananchi na taifa kwa ujumla"

Wewe unaishi dunia gani ? Kwani hujui kuwa mfalme wenu aliwahi kusema tena akiwa ughaibuni kuwa hajui kwanini nchi yenu ni maskini!!! Je kiongozi kama huyo anaweza kupambanua masuala muhimu ya nchi yake?
 
Na kuna kila dalili ya serikali ku impose similar candidate kwa sababu hali inavyoonyesha sasa, jamaa anataka ku eliminate kama siyo ku eradicate kila brain inayoona yenye uwezo wa kuinfluence changes. Atapinga mabadiliko kwa gharama yoyote kwa sababu anapenda sifa na asingependa aweke record inayoonyesha alipwaya hadi system mpya ikaingia na pia hatapenda kuona utawala unaomfuata unamnyooshea vidole kwa makosa makubwa aliyoyafanya wakat wa utawala wake.

Kwa hayo aanatumia vizuri muda wake liobaki wa kujenga mazingira yakuendelea kumiliki nchi hata baada ya kustaafu. Akiwaondoa wote wanao mquestion, akabakiza wapambe wanafiki na waoga, nani atasimamia maslahi ya watanzania maskini na wa jinga?

Mungu tusaidie.
hili linawezekana...maana shida kubwa ya TZ..ni mchakato wa kupata mgombea urais..huko kwenye vyama....wanapowekana kwa matakwa yao binafsi...alafu wanakuja kuwapa raia mtu boggus wampigie kura....maana raia hawahusiki na uteuzi wa mgombea urais kwa ujumla wao....tatizo nchi hii ni uozo kwenye system nzima inayotawala nchi hii....its terrible yaani..yaani tuombe mungu tupate katiba mpya na tuweze kuisimamia.....maana kwa mtindo huu...hata katiba mpya inaweza kuwa nzuri lakini ikakosa watu makini wa kuisimamia.....
 
Ndugu mtoa uzi , unayoyasema siyo mapya yamesemwa mpaka basi. Kuna bwana mmoja aliandika makala yenye kurasa sita juu ya washauri wa kikwete. Makala hiyo iliitwa " Ugumu wa kumshauri rais Kikwete. Baada ya makala hiyo akaja Johnson Mbwambo mwandishi ambaye yupo wazi kuwa yeye na serikali ya sasa ni mafuta na maji japo wanaoendesha serikali sio maadui zake. Yaani hana personal conflict na baba Rizi ila hakubaliani kabisa na rais Kikwete kwenye mambo mengi. Soma makala hii
Raia Mwema - Ya sasa mapya, hatujayaona tangu Uhuru!
hapo ndoo utaona kuwa sikio la kufa halisikii dawa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom