Nani ni mmiliki wa Channel 10?

JAYJAY

JF-Expert Member
Oct 31, 2008
7,510
7,541
ni muda mrefu nimekuwa nikifuatilia taarifa ya habari ya ch10 kwenye kipengele cha uchambuzi wa magazeti na mara zote magazeti ya the guardian ltd ya mzee mengi huwa yanawekwa kapuni.sasa naomba kuuliza kwa anayefahamu mmiliki wake ninahisi kuna influence fulani hapo.
 
Channel ipo huru sana na pia inatokana na zile commentary za siku toka katika magazeti hayo
 
Channel 10 hivi sasa inamilikiwa na mafisadi papa waliotajwa na Mengi. Hivyo sio rahisi hawa ku-review magazeti ya "adui' yao. Kama sikosei majority shareholder ni Tanil Somaiya, yule mwenye dili nyingi za ku-supply vitu mbalimbali jeshini, kv magari aina ya Iveco, helikopta mbovu, nk
 
Last edited:
ni muda mrefu nimekuwa nikifuatilia taarifa ya habari ya ch10 kwenye kipengele cha uchambuzi wa magazeti na mara zote magazeti ya the guardian ltd ya mzee mengi huwa yanawekwa kapuni.sasa naomba kuuliza kwa anayefahamu mmiliki wake ninahisi kuna influence fulani hapo.
Wewe unayeuliza anayemiliki so what? kwa magazeti ya mengi yasipotajwa what is a deal?? (magazeti ya mengi yana umuhimu kwako kanunue) kwa chanel 10 siyo muhimu???
Utawajua walionunuliwa na watu mlima mrefu.
 
Channel 10 hivi sasa inamilikiwa na mafisadi papa waliotajwa na Mengi. Hivyo sio rahisi hawa ku-review magazeti ya "adui' yao. Kama sikosei majority shareholder ni Tanil Somaiya, yule mwenye dili nyingi za ku-supply vitu mbalimbali jeshini, kv magari aina ya Iveco, helikopta mbovu, nk
 
Kwa muda wa kutosha sasa Channel imekuwa mali ya Rostam Aziz na genge lake na hii ndiyo vita kubwa iliyoko Tanganyika hapa .Tumaini kuwa na sense kiasi ndugu .Mtu kaluliza swali mjibu kama una jibu kama huwezi kaa pembeni .
 
Kwa muda wa kutosha sasa Channel imekuwa mali ya Rostam Aziz na genge lake na hii ndiyo vita kubwa iliyoko Tanganyika hapa .Tumaini kuwa na sense kiasi ndugu .Mtu kaluliza swali mjibu kama una jibu kama huwezi kaa pembeni .

Tumaini akinusa harufu ya dini tu basi ana-react accordingly
 
Tumaini akinusa harufu ya dini tu basi ana-react accordingly
Kivipi? sijaona tatizo la station kutakuonyesha magazeti ya mengi?? sioni kama ni big deal! Magazeti ya mengi yanapata coverage kubwa inatosha sana tu!
 
Wewe unayeuliza anayemiliki so what? kwa magazeti ya mengi yasipotajwa what is a deal?? (magazeti ya mengi yana umuhimu kwako kanunue) kwa chanel 10 siyo muhimu???
Utawajua walionunuliwa na watu mlima mrefu.
Chombo cha habari ni kwa ajili ya wananchi,huwezi kuwanyima baadhi ya taarifa,kama ni mchoyo wa habari hufai kumiliki chombo cha habari,ili habari zako za uchoyo uwasimulie familia yako.Tabia ya kutetea mafisadi hapa JF ikome kwani si sehemu yake,kama unawahusudu mafisadi ukanywe nao kahawa.Mafisadi na makuwadi wao washidwe na walegee kwa jina la Yesu.
 
mtu wa manzese hawezi kumiliki vyombo vya habari,lazima mafisadi wamiliki ili wazibe ulaji wao
 
Amen!! amini amini nawaambia, hakuna goti la fisadi au kuwadi wake ambalo halitapigwa ifikapo siku wana wa Tanganyika watakapo amka katika usingizi! Naam, tazama hata asubuhi inakaribia kwa wana wa Tanganyika nao watatoka katika usingizi wao na kuwaona waliowadhulumu mali za baba zao. Nao hao mafisadi watakuwa wamelewa kwa mali za kifisadi huku wakijigamba kuwa wao ndio.

Hapo utamwona mwana wa Tanganyika akiwa na silaha ifananayo na ile ilotumika na wana wa USA wakati walipomchagua kiongozi alovunja rekodi ya miaka mingi.
 
Mkuu;
Mengi hawamuwezi kabisa, sisi watanzania tunamwombea sana, na penye ukweli uongo utajitenga mafisadi mwisho wao ndo huu,hakuna jinsi Mungu amewaanika mpaka watajuta kuzaliwa.
 
To be fair, labda tuseme Mengi ndio kaanza haka ka-mchezo ka kutokusoma magazeti ya wenzake. Sina uhakika nani alianza, lakini ukweli ni kwamba ITV au Redio One hawachambui magazeti mengine zaidi yao. Zamani walikuwa wanachambua, lakini sasa hamna kitu.Wanachambua magazeti ya IPP Media tu.

Kwa uchambuzi wa magazeti, sikiliza Clouds FM 88.4 in Dar, 87.8 in Mbeya.
 
Wewe unayeuliza anayemiliki so what? kwa magazeti ya mengi yasipotajwa what is a deal?? (magazeti ya mengi yana umuhimu kwako kanunue) kwa chanel 10 siyo muhimu???
Utawajua walionunuliwa na watu mlima mrefu.

tuwe na busara kidoogo tunapojibu hoja za watu kwa manufaa ya sisi wengine ambao tunataka kujua ukweli,kama wewe unaujua endelea na shughuli zingine.
wewe umenunuliwa na nani kwa majibu hayo!!!
 
Kuhusu swali lako "Nani mmiliki wa Channel 10" ni kwamba channel hii ina historia ya kumilikiwa na mafisadi na matapeli wa kimataifa. Aliyeanzisha ni Muitaliano mmoia --wa kundi la Mafia -- Franco Tramontano aliypewa uraia wa Tanzania na utawala wa Mkapa baada ya serikali kuikatalia serikali ya Belgium kum-extradite kwenda kusimama kizimbani kwa wizi wa USD 2 milioni zilizokuwa za msaada kwa Tanzania na ambazo alizitumia kuanzisha Channel 10. Hiyo ilikuwa mwishoni mwa 1990s.

Akaiuza kwa Tanil Somaya -- Mtuhumiwa wa ufisadi wa radar na sasa tunasikia mtuhumiwa wa ufisadi wa Kagoda -- RA kanunua hisa nyingi. Hawa wanahisa kazi yao kubwa ni kuibomoa TV ya mzalendo Mengi baada ya kufanikiwa kuwaweka mfukoni maafisa wa TCRA na Waziri wa Habari. Hapa Tanzania tunakwenda vizuri sana.

Hiyo ndiyo historia fupi ya Channel 10 ambao nao hawasomi kabisa magazeti ya IPP Media.
 
Chombo cha habari ni kwa ajili ya wananchi,huwezi kuwanyima baadhi ya taarifa,kama ni mchoyo wa habari hufai kumiliki chombo cha habari,ili habari zako za uchoyo uwasimulie familia yako.Tabia ya kutetea mafisadi hapa JF ikome kwani si sehemu yake,kama unawahusudu mafisadi ukanywe nao kahawa.Mafisadi na makuwadi wao washidwe na walegee kwa jina la Yesu.
Tabia ya kutetea ubaguzi kwa misingi ya rangi ikome kabisa hapa JF mmiliki wa vyombo habari ana haki ya kutangaza chochote na kuacha chochote kutegemeana na muda uliopo (air time) na maslahi yake ya kibiashara pamoja na ethics za uandishi! kutokutamgaza magazeti ya mengi kati ya magazeti yote nchini siyo big deal?? who is he? mengi naye fisadi tu tena nyangumi so sijaona unachotetea hapo
 
Channel 10 kwa kiasi kikubwa inamilikiwa na wahindi. Wahindi hawapendi ku-support vitu vya weusi (Wadanganyika). Ukipita Dar jaribu kuingia restaurants za wahindi utaona kuwa wengi au wote hawauzi/hawastock bidhaa za coke. Lakini za Pepsi utazikuta. Sisi wamatumbi tunastock na kuuza zote hatuna ubaguzi. Hivi nasi tukigomea vitu vya Wahindi, nani ataumia zaidi? Ukweli unabaki kuwa wahindi ni wabaguzi wa kila kitu.
 
Tabia ya kutetea ubaguzi kwa misingi ya rangi ikome kabisa hapa JF mmiliki wa vyombo habari ana haki ya kutangaza chochote na kuacha chochote kutegemeana na muda uliopo (air time) na maslahi yake ya kibiashara pamoja na ethics za uandishi! kutokutamgaza magazeti ya mengi kati ya magazeti yote nchini siyo big deal?? who is he? mengi naye fisadi tu tena nyangumi so sijaona unachotetea hapo

Tumain,
Sidhani kama usemayo ni kweli. Kuna sheria za uandishi wa habari, mmiliki wa vyombo vya habari hana haki ya kutangaza chochote. Kuna miiko na maadili ya uandishi wa habari. Hivyo acha upotoshaji wa habari, kama hujui au mwenyewe una chuki binafsi basi ni bora ukakaa kimya.
Kwanza kisheria mmiliki wa vyombo vya habari hapaswi kuingilia urushwaji wa habari. Ndiyo maana kuna wafanyakazi wenye uelewa wa habari mfano wahariri n.k
Swala la ubaguzi limetokea wapi tena? Yaani kuuliza mmiliki wa channel 10 ndo ubaguziiiiii........
nadhani tunaelekea pabaya sasa, kila kitu ni ubaguzi.....
 
Back
Top Bottom