mchumia tumbo
JF-Expert Member
- Jun 19, 2012
- 1,459
- 476
Nadhani tuwe tunakubaliana na ukweli.
Mtoa mada ameeleza vizuri na inaonekana tatizo hilo la wahamiaji haramu linagusa eneo la magharibi tu!
Kama maeneo mengine ya mipaka yetu, tuna watu wa jamii kama siyo koo moja ukivuka mpaka. Ukiangalia Kusini, huwezi kuwatenga watu wa Mozambique na Mtwara kiasi kwamba kipindi cha uchaguzi, watu wa ng'ambo ya mpaka wanachagua uongozi wa upande mwingine. Ukiangalia wamasai, huwezi kutofautisha wa Kenya na Tanzania. Mkoa wa Mara huwezi kujua nani ni nani mpaka watu wanavuka mpaka kunyang'anyana mifugo. Nk.
Siku zijazo tusishangae wanasiasa wanatushambulia watu wa kusini wakisema wanaopinga bomba la gesi ni wa kutoka Msumbiji. Au tukasikia kuwa wamasai walioko Ifakara ni wanaotoka Kenya; pale wakuu wa nchi watakapotofautiana na nchi hizo jirani.
Ninachokiona, tusiweke siasa kwenye uhamiaji haramu. Kama tunafanya zoezi lisiwe zimamoto na lisiwaguse baadhi kama kweli tuna nia ya kumaliza tatizo.
Angalizo:
Kwa aina ya wahamiaji haramu, hususan wale wa mikoa ya Kagera na Kigoma, kuna makabila ya watusi na wahutu walioingia miaka mingi iliyopita. Hawa wote wamekuwa wakiishi kama watanzania kwa miaka mingi kutokana na historia ya kabla 1920 wakati tukiwa na Deutch East Africa ambapo Rwanda na Burundi zilikuwa sehemu ya nchi hiyo.
Tatizo linakuja pale tunapowafukuza upande mmoja wa wahamiaji hao kutokana na sura badala ya uharamu wao. Watusi wanatambulika kirahisi wakati wahutu wamejibatiza makabila ya hapa nchini na kukubalika. Mimi nasubiri watangaze kuwa iperation imemalizika ndo tutaanza kuwataja waliojificha, ingawa wengine wana nyadhifa za juu na bila shaka itakuwa vigumu kuwashughulikia.
Anjo
Hata ukijitetea utarudi tu kwenu,hakuna muhaya mwenye sura ya kitutsi.