Nani katoa kibali cha ujenzi hapa??

Nani katoa kibali cha ujenzi hapa??

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,410
Reaction score
14,119
View attachment 69288
Wakati mwingine nashangaa sana nji hii!!
Huko kipande ya Makongo support ya nguzo inajengewa ndani ya nyumba.
Sasa hizo nguzo za umeme zikioza zitatolewa vipi?
 
Inategemea nyumba hiyo ni ya nani!!ingekuwa ni ya kabwela kama mimi ningeshakatwa ma katafunua ya kutosha na kuvunjilia mbali kibanda changu,ila huyo kaombwa!! naye katoa muda ili afikirie kuvunja ama kuacha,hii ni bongo tz.
 
Ila mkandarasi kaacha nafasi kati ya majengo mawili, hata baraza haijashikamana. Ila paa tu.
 
hiyo ndiyo bongo,
mwenye nacho anweza jenga nyumba hata kati ya barabara,
usiye nacho unanyang'anywa kiwanja chako ukiona!
 
Usalama upo wapi hapa wa huyo mwenye nyumba?
 
dirisha ambapo hiyo nguzo imepita, litakuwa likifungwa vp?
 
Hii nyumba itakua maeneo ya UZINI Zanzibar, huko Magufuli hagusi
 
Ila mkandarasi kaacha nafasi kati ya majengo mawili, hata baraza haijashikamana. Ila paa tu.


Mleta mada anaongelea nguzo ya Tanesco ya kushikiza iko ndani ya nyumba, siyo nafasi kati ya majengo mawili wala baraza kushikamana.
 
Ah bado kuamini aisee...nipe directions za kufika hapo mkuu!
 
aiseee babangu kwa mtindo huo hata usishangae nguzo kupita katokato ya uwanja wa taifa na airport
 
Mleta mada anaongelea nguzo ya Tanesco ya kushikiza iko ndani ya nyumba, siyo nafasi kati ya majengo mawili wala baraza kushikamana.
Asante Small Maza, kuna wana JF siyo critical thinkers.
Hapa najaribu kuonyesha kwanza uhatari wa kujenga kwa kuikumbatia miundombinu hatari ya umememe.
Pili hapa , right-of-way ya miundombinu ya umeme inaishia wapi? Kwa maana kwa mtindo huu watu watajenga hata chini ya nyaya za umeme.
 
Back
Top Bottom