Nani Fisadi-CCM ama Serikali?

Chama cha mafisadi ndio kimeshika utamu. Kwa hiyo kama viongozi wa serikali wanatoka katika chama cha mafisadi basi serikali pia imejaa mafisadi na ni fisadi pia. Utakuwaje sio fisadi kama mafisadi wanaachiwa wanapeta tu bila kuchukuliwa hatua zozote?

Sasa wewe unasubiri nani awachukulie hatua? Kuna sheria yoyote inayokuzuia kuwachukulia hatua? Tatizo lenu mnataka kufanya ufisadi ni political agenda. Mtu kama fisadi anatakiwa kupelekwa mahakani na mtanzania yoyote ana uhuru wa kufanya hivyo. Kama unashindwa mwambie Slaa awapeleke mahakamani kwa maana yeye ndiye mwenye ushahidi wote.
 
CCM Kuongeza kiwango cha MadiniBy Mike Mushi | Published 11/26/2005 | Habari Mpya |
CCM Kuongeza kiwango cha Madini


shein-2005-52.jpg

Chama Cha Mapinduzi kinakusudia kuongeza kiwango cha thamani ya madini kutoka asilimia 0.3 ya hivi sasa hadi kufikia asilimia 3 iwapo chama hicho kitashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk Ali Mohamed Shein amesema pamoja na kuongeza viwango vya madini hayo pia serikali ijayo itahakikisha inatengeneza vito vya madini hapa hapa nchini ili kuweza kuuza madini kwa tija.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Londoni wilayani Manyoni.

Amesema suala la madini limepewa kipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005-2010 kutokana na ukweli kwamba sekta ya madini inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua uchumi wa nchi.

Amewaambia wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa ili kufanikisha azma hiyo serikali itatoa mikopo na elimu kwa wachimbaji wadogo wadogo kwa njia ya semina na mikutano ili waweze kujua namna ya kuchimba madini hayo kitalaam.

�Baada ya kupewa mikopo, mpewe elimu kwa njia ya semina, mikutano au warsha mjue namna ya kuchimba madini hayo kitalaam�. Aliwaeleza wananchi hao ambao wengi wao ni wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu katika eneo hilo.

Dk. Shein amethibitisha kuwa serikali ya awamu ya nne itaendelea kukaribisha wawekezaji wakubwa katika sekta ya madini na pia itaangalia upya sera yake ya madini ili iweze kuwanufaisha wadau wote.

Amesisitiza wananchi wakichague Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndio chama pekee kinachoonyesha jitihada za kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kuweza kupambana na umasikini hali ambayo hatmae itawafanya kuwa na maisha bora.

Katika hatua nyingine Mgombea Mwenza huyo amewataka wachimbaji wadogo wa madini nchini kutumia fedha wanazozipata kwa kujijenga kimaisha kwa kuwa na nyumba bora, kutunza afya zao na kusomesha watoto na sio kwa anasa.

�Fedha ni fedheha, zikiwa nyingi zinachanganya kidogo hujui utazifanyia nini, unaishia sehemu ukiulizwa wewe nani na wewe unauliza pia wewe nani. Huo si utumiaji mzuri wa fedha�. Alisema Dk Shein

�Hata hivyo starehe zikizidi inachangia maambukizi ya ukimwi hilo nalo ni tatizo tukitambua ukimwi sasa ni janga la kitaifa. Hivyo hamna budi kuwa waangalifu na matumizi ya fedha�. Aliongeza.

Nafikiri ita-make more sense tukisema Fisadi amekuwa Mwanaccm kuliko mwanaccm ni fisadi ! upo hapo ?
 
Sasa wewe unasubiri nani awachukulie hatua? Kuna sheria yoyote inayokuzuia kuwachukulia hatua? Tatizo lenu mnataka kufanya ufisadi ni political agenda. Mtu kama fisadi anatakiwa kupelekwa mahakani na mtanzania yoyote ana uhuru wa kufanya hivyo. Kama unashindwa mwambie Slaa awapeleke mahakamani kwa maana yeye ndiye mwenye ushahidi wote.

tatizo lingine ndio hilo ! watu wanajua mahakama zilipo, na baada ya kufuata sheria, wanatumia kama political agenda kushinda kura uchaguzi ujao, but little do they know kwamba watu wapo steps ahead kushusha hadhi hizo propaganda zao, na bora wawe na plan a, b, c, ..............z maana uchaguzi ujao sio kama wanavyodhani !

walisema mkapa fisadi, sasa kesi iko wapi hadi leo ?
 
Quote:
Originally Posted by jmushi1
CCM Kuongeza kiwango cha MadiniBy Mike Mushi | Published 11/26/2005 | Habari Mpya |
CCM Kuongeza kiwango cha Madini

Chama Cha Mapinduzi kinakusudia kuongeza kiwango cha thamani ya madini kutoka asilimia 0.3 ya hivi sasa hadi kufikia asilimia 3 iwapo chama hicho kitashinda katika Uchaguzi Mkuu ujao.

Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM Dk Ali Mohamed Shein amesema pamoja na kuongeza viwango vya madini hayo pia serikali ijayo itahakikisha inatengeneza vito vya madini hapa hapa nchini ili kuweza kuuza madini kwa tija.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki alipokuwa akihutubia mkutano wa kampeni uliofanyika katika kijiji cha Londoni wilayani Manyoni.

Amesema suala la madini limepewa kipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2005-2010 kutokana na ukweli kwamba sekta ya madini inachangia kwa kiasi kikubwa katika kuinua uchumi wa nchi.

Amewaambia wananchi waliohudhuria mkutano huo kuwa ili kufanikisha azma hiyo serikali itatoa mikopo na elimu kwa wachimbaji wadogo wadogo kwa njia ya semina na mikutano ili waweze kujua namna ya kuchimba madini hayo kitalaam.

Dk. Shein amethibitisha kuwa serikali ya awamu ya nne itaendelea kukaribisha wawekezaji wakubwa katika sekta ya madini na pia itaangalia upya sera yake ya madini ili iweze kuwanufaisha wadau wote.

Amesisitiza wananchi wakichague Chama Cha Mapinduzi kwa kuwa ndio chama pekee kinachoonyesha jitihada za kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kuweza kupambana na umasikini hali ambayo hatmae itawafanya kuwa na maisha bora.

Kama kuna mbunge humu akipita JF, mwenye uchungu na nchi yake kwanza amwulize serikali yetu je imetimiza hayo maneno highlited?

Pili wamwulize ndugu Chiligati ambaye kama sikosei ni mbunge wa hiyo sehemu Londoni alipokuwa akitoa hotuba Dr...Je hawo wachimbaji wadogo wadogo wa sehemu hio wamefikia wapi ki maendeleo?

Maanake mara ya mwisho nilipokuwa hapo wachimbaji wadogo walisitishwa kazi zao za uchimbaji bila fidia kwa sababu kampuni ya Shanta Mine walikuwa wanafanya drilling na wakaleta na security na mbwa wakali hata ikawa wana vijiji hawawezi kukatiza sehemu ambazo walikuwa wakilima ati kwa sababu kuna exploration inaendelea.....hiyi ndio nchi yetu huko vijijini...na jinsi tulivyokuwa makondooo hakuna tunalifanya tunabaki kusikitika na kukaa chini kucheza karata na bao...siku imeenda
 
Hao wabunge badala ya kugangamala watu wakamatwe na mambo ya EPA na RICHMOND...Wao wanakimbia bunge kwasababu ya uchawi..Halafu wakirudi huko wanaendeleza LIBENEKE!
Watakaa vipi na MAFISADI MAFIOSO ndani ya BUNGE TUKUFU halafu waseme ni MASLAHI YA TAIFA?
 
Kama kuna mbunge humu akipita JF, mwenye uchungu na nchi yake kwanza amwulize serikali yetu je imetimiza hayo maneno highlited?

Pili wamwulize ndugu Chiligati ambaye kama sikosei ni mbunge wa hiyo sehemu Londoni alipokuwa akitoa hotuba Dr...Je hawo wachimbaji wadogo wadogo wa sehemu hio wamefikia wapi ki maendeleo?

Maanake mara ya mwisho nilipokuwa hapo wachimbaji wadogo walisitishwa kazi zao za uchimbaji bila fidia kwa sababu kampuni ya Shanta Mine walikuwa wanafanya drilling na wakaleta na security na mbwa wakali hata ikawa wana vijiji hawawezi kukatiza sehemu ambazo walikuwa wakilima ati kwa sababu kuna exploration inaendelea.....hiyi ndio nchi yetu huko vijijini...na jinsi tulivyokuwa makondooo hakuna tunalifanya tunabaki kusikitika na kukaa chini kucheza karata na bao...siku imeenda

Wanajua kila kitu!
Hata kwenye sera zao za madini CCM wamemention hilo la kudai yatawasaidia wananchi!
Sasa tume mpya iliundwa ya nini ile ya madini?
Ushauri gani mpya ambao wakongwe hao Mafioso hawaulewi?
 
Haya hawa CCM waliochota pesa za EPA halafu kwa kuitumia serikali yao wakampoteza Ballali huku wakidhani ushahidi umekufa na sasa wanataka MISIFA ILI TUSONGE MBELE....

Samuel John Tegeza Sitta</STRONG>
Huyu ni mwanasiasa machachari. Kitaaluma ni mwanasheria na mtu ninayeweza kusema pasipo kusitasita, kuwa ameandika historia pekee tangu akiwa kiongozi wa juu wa Bunge.
Ni ukweli usiopingika kwamba katika kipindi cha miaka miwili na nusu tangu awe Spika, Sitta amefanikiwa kulijengea Bunge heshima ya pekee kutokana na namna alivyoweza kusimamia kwa umakini mkubwa baadhi ya masuala mazito.
Kwanza Sitta anaweza akatajwa kuwa ni Spika aliyesaidia sana kuliongezea meno na nguvu Bunge, akiliweka katika mstari sahihi wa kimaamuzi na kulijengea taswira ambayo haikupata kuwapo siku zilizopita.
Uzito wa maamuzi kama lile la kuundwa kwa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza utata katika mkataba wa Richmond, ni ushahidi mmoja tu wa mafanikio ya Uspika wa Sitta, ambao kwa kiwango kikubwa yalimjengea heshima ya pekee ndani na nje ya Bunge.
Matokeo ya Kamati hiyo Teule ya Bunge iliyoongozwa na Dk. Harrison Mwakyembe ambayo ni pamoja na kulazimishwa kujiuzulu kwa aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri wengine wawili - Nazir Karamagi na Dk. Ibrahim Msabaha - yamemfanya Sitta aonekane shujaa wa kipekee ndani ya Bunge.
Richmond, kwa upande mwingine, imemfanya Sitta aonekane na achukue sura ya kuwa mpambanaji dhidi ya vitendo vya kifisadi ndani ya chama chake na pengine serikalini. Huu ni ukweli unaopaswa kuheshimiwa.
Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba ushujaa huu wa Samuel Sitta umefikia hatua ya kumvimbisha kichwa hata kumfanya aanze kutembea kifua mbele na kujiona kuwa ni mtu asiyetaka kuguswa.
Leo hii ni kosa kubwa na baya kabisa kumgusa au kumkosoa Sitta.
Ushahidi wa maandishi unaonyesha bayana kuwa wanahabari waliopata kumgusa mwanasiasa huyo tangu alipojitwalia ushujaa katika Kashfa ya Richmond, wamejikuta wakipewa majina mabaya kabisa na wakati mwingine wakihusishwa na kundi la mafisadi.
Hivi karibuni, mwandishi mmoja wa habari wa ‘Tanzania Daima’ Jumapili; Charles Mullinda, alifanya ‘kosa’ - kwa kujua au kutojua, kwa makusudi au kwa bahati mbaya - akamgusa Sitta sehemu mbaya kwa kuandika makala moja dhidi yake.
Kwa namna ya ajabu kabisa, ukosoaji huo dhidi ya Sitta umechukua sura ya pekee. Wabunge na waandishi kadhaa wa habari wamesikika wakieleza namna Sitta alivyoshtushwa na makala hiyo hata kuiunganisha na kile alichopata kukielezea kuwa ni ‘siasa za majitaka’.
Kwa namna ile ile alivyopata kufanya wakati zilipoandikwa taarifa kuhusu tuhuma za kutumia - isivyofaa - fedha na mali nyingine za Bunge, Sitta amesikika safari hii chini chini akihusisha upinzani huo wa hoja dhidi yake na ajenda ya mafisadi kumchafua. Huu ni upuuzi.
Sitta, kwa sababu ya kile kinachoweza kuonekana kuwa ni jeuri inayotokana na matokeo ya vita dhidi ya ufisadi, amegeuka na kuwa mtu anayeweza kusema lolote baya dhidi ya watu wengine na akaaminika na hata kuonekana kuwa ni msema kweli. Hali hii lazima ifikie mwisho.
Hivi sasa kwa sababu ya ‘jeuri’ hii, maofisa wa Bunge wanaomuona Sitta kuwa shujaa wao wa vita dhidi ya ufisadi ambayo ‘Tanzania Daima’ ina kila sababu ya kutembea kifua mbele cha kupambana na tatizo hili kabla Spika huyo hajatiwa ‘wakfu wa ushujaa zama za Kamati ya Mwakyembe’, wamefikia hatua ya kuwaogopesha wanahabari kutomgusa mkuu wao wa kazi
 
Back
Top Bottom