NANI ATAKUWA RAIS MUOKOZI WA TANZANIA???
Wakati ndugu zetu wa ZNZ tayari washajua nani atakuwa Rais wao baada ya uchaguzi wa 2010, sisi kutoka Bara bado tunatia mikono yetu gizani kumdhania huyu au yule atafaa kama Kikwete kweli atapumzika mwakani kutokana na matatizo yake ya akili.
Kama Rais ajae atatoka tena CCM kama wengi wanavyotabiri, basi hatuna haja ya kupata shida ya kumfikiria nani ni mfanyakazi bora au dikteta zaidi katika kazi ambae atakuja kutufaa na kuiokoa hii nchi. Mwana-CCM yoyote yule atafaa. Hii nchi ni kweli imegombolewa na TANU, lakini haitookolewa na CCM. Ni lazima kiwe chama chengine cha kuleta mapinduzi hayo tunayoyalilia kila siku. CCM imemalizika na Kikwete kaizika haina fire power tena!
Yoyote atakaetoka CCM mwakani kama Rais mpya wa Jamhuri yetu, hatokuwa tofauti na Kikwete au na hao wawili waliopita, hata kama yeye hivi sasa ni waziri anaesifika kwa kulitumikia Taifa letu vizuri sana. Kuwa waziri mzuri na mchapakazi is one thing na kujakuwa Rais muokozi is quite another. CCM tayari ishajiwekea system yake mbovu na mtu yoyote atakaechaguliwa hatoweza kuenda kinyume na system hio, hata kama akiwa mfanyakazi mzuri sana. Kwahivyo, wale wanaomfikiria fulani anafaa watakuja kuvunjika moyo watakapokuja kumuona huyo waliemchagua ni sawasawa au zaidi ya huyu Kikwete, kwasababau system ya CCM ya kubebana ni tayari ishakuwa set up na ukikataa kuwabeba wenzio basi ujue utakuenda na maji.
Ni juzi juzi tu hapa tulipomuona Nyerere mbaya alivyompeleka mbele Mkapa na sote tukawa tunamlilia Kikwete na Lowassa, kwani tukiona wao ni watoto wa new generation na mambo chini yao yangekuwa mazuri. Je, new generation imetupeleka wapi leo? Bado tu hatujaacha hii tabia ya kumuona mtu fulani atatufaa kutoka CCM? CCM yote haitotufaa seuze mtu fulani. CCM kishakuwa chama obsolete na kinafaa kipigwe marufuku, kama
kilivyopigwa marufuku CCCP kule Urusi.
Kwahivyo, tunapofikiria nani atatufaa - mtu yoyote kutoka CCM iwe out of our minds. Hata akitoka mbinguni, lakini akiwa
mwana-CCM basi mambo yatakuwa haya haya tu kama yalivyo
hivi sasa. Hii ni kwasababu ya system ya kubebana
ilivyo na sio kwasababu ya mtu mwenyewe alivyo.
Atakaeiokoa nchi hii ni Rais kutoka upinzani na sio kutoka CCM. Kwahivyo, badala ya kupeyana nambari za simu ili tumshawishi mtu fulani wa CCM agombee urais mwakani, ni bora tutumie nguvu zetu kuvishawishi vyama vya upinzani nchini vikubaliane kumuweka mtu mmoja kugombea urais. Wapinzani wakiungana CCM itaanguka na hapo ndipo tutakapopata muokozi wa kweli wa hili Taifa. Kutegemea fulani ni waziri machachari na hodari wa kazi yake kutoka CCM na atakuja kuliokoa Taifa ni sawa na kutokutumia akili zetu vizuri, kwani katika chaguzi zetu za Rais hapa Tanzania tunakichagua chama na sio mtu. Kwahivyo, CCM ikishinda urais na Rais mpya akawa anafanyakazi zake kinyume na system ya kubebana ya CCM ilivyo, definitely watamuweka upande na badala yake fisadi atawekwa kuwa Rais na mambo yataenda kama yalivyo hivi sasa!
- Ni lazima atoke upinzani
- Mwana-CCM yoyote hafai, hata akitoka mbinguni
- Bila ya upinzani kuungana, mengine yote ni ndoto ya mchana
Wakati ndugu zetu wa ZNZ tayari washajua nani atakuwa Rais wao baada ya uchaguzi wa 2010, sisi kutoka Bara bado tunatia mikono yetu gizani kumdhania huyu au yule atafaa kama Kikwete kweli atapumzika mwakani kutokana na matatizo yake ya akili.
Kama Rais ajae atatoka tena CCM kama wengi wanavyotabiri, basi hatuna haja ya kupata shida ya kumfikiria nani ni mfanyakazi bora au dikteta zaidi katika kazi ambae atakuja kutufaa na kuiokoa hii nchi. Mwana-CCM yoyote yule atafaa. Hii nchi ni kweli imegombolewa na TANU, lakini haitookolewa na CCM. Ni lazima kiwe chama chengine cha kuleta mapinduzi hayo tunayoyalilia kila siku. CCM imemalizika na Kikwete kaizika haina fire power tena!
Yoyote atakaetoka CCM mwakani kama Rais mpya wa Jamhuri yetu, hatokuwa tofauti na Kikwete au na hao wawili waliopita, hata kama yeye hivi sasa ni waziri anaesifika kwa kulitumikia Taifa letu vizuri sana. Kuwa waziri mzuri na mchapakazi is one thing na kujakuwa Rais muokozi is quite another. CCM tayari ishajiwekea system yake mbovu na mtu yoyote atakaechaguliwa hatoweza kuenda kinyume na system hio, hata kama akiwa mfanyakazi mzuri sana. Kwahivyo, wale wanaomfikiria fulani anafaa watakuja kuvunjika moyo watakapokuja kumuona huyo waliemchagua ni sawasawa au zaidi ya huyu Kikwete, kwasababau system ya CCM ya kubebana ni tayari ishakuwa set up na ukikataa kuwabeba wenzio basi ujue utakuenda na maji.
Ni juzi juzi tu hapa tulipomuona Nyerere mbaya alivyompeleka mbele Mkapa na sote tukawa tunamlilia Kikwete na Lowassa, kwani tukiona wao ni watoto wa new generation na mambo chini yao yangekuwa mazuri. Je, new generation imetupeleka wapi leo? Bado tu hatujaacha hii tabia ya kumuona mtu fulani atatufaa kutoka CCM? CCM yote haitotufaa seuze mtu fulani. CCM kishakuwa chama obsolete na kinafaa kipigwe marufuku, kama
kilivyopigwa marufuku CCCP kule Urusi.
Kwahivyo, tunapofikiria nani atatufaa - mtu yoyote kutoka CCM iwe out of our minds. Hata akitoka mbinguni, lakini akiwa
mwana-CCM basi mambo yatakuwa haya haya tu kama yalivyo
hivi sasa. Hii ni kwasababu ya system ya kubebana
ilivyo na sio kwasababu ya mtu mwenyewe alivyo.
Atakaeiokoa nchi hii ni Rais kutoka upinzani na sio kutoka CCM. Kwahivyo, badala ya kupeyana nambari za simu ili tumshawishi mtu fulani wa CCM agombee urais mwakani, ni bora tutumie nguvu zetu kuvishawishi vyama vya upinzani nchini vikubaliane kumuweka mtu mmoja kugombea urais. Wapinzani wakiungana CCM itaanguka na hapo ndipo tutakapopata muokozi wa kweli wa hili Taifa. Kutegemea fulani ni waziri machachari na hodari wa kazi yake kutoka CCM na atakuja kuliokoa Taifa ni sawa na kutokutumia akili zetu vizuri, kwani katika chaguzi zetu za Rais hapa Tanzania tunakichagua chama na sio mtu. Kwahivyo, CCM ikishinda urais na Rais mpya akawa anafanyakazi zake kinyume na system ya kubebana ya CCM ilivyo, definitely watamuweka upande na badala yake fisadi atawekwa kuwa Rais na mambo yataenda kama yalivyo hivi sasa!