Nani anastahili kumrithi Mizengo Pinda?

Nani anastahili kumrithi Mizengo Pinda?

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,203
Reaction score
162,766
Ukiangalia mwenendo mzima wa sakata la Tegeta Escrow account,utagundua kuwa, kuna uwezekano mkubwa wa waziri mkuu ambae nae amekuwa akituhumiwa kupata mgao,kuwa implicated katika kashifa hii na hivyo kutakiwa kuwajibika.

Kuna viashiria kadhaa kuwa PM anaweza kutakiwa kuwajibika kwa kujiuzulu.

Mosi,Pinda ametajwa sana kupata mgao(sina uhakika) katika hili sakata na sidhani kama itakuwa ni uzushi tu maana siku zote mambo huanza hivi hivi na mwisho wa siku inageuka kuwa kweli.

Pili,imekuwa ikisemwa kuwa kashifa hii huenda ikaiangusha serikali na mh.Zitto pekee alikwenda mbali zaidi kwa kusema sakata hili linaweza kuangusha "tembo mkubwa".

Sasa mh.Zitto anaposema kashifa hii inaweza kumuangusha tembo mkubwa,hapo alikuwa anamlenga nani zaidi ya waziri mkuu?

Mbali na viashiria hivyo,jambo lingine linalomuweka Pinda katika wakati mgumu wa ku-survive kashifa hii na pia ku-survive vote of no confidence endapo tutafika huko,ni hatua yake ya kujiingiza katika kinyang'anyiro cha uraisi ndani ya CCM.

Kwa mtazamo wangu,wapinzani wake watatumia mwanya huo kummaliza kwa kuhakikisha(ku-facilitate) upigwaji wa kura hiyo na ikipigwa aondoke.

Sasa kwa utangulizi huo,ni dhahiri PM anaweza kuondoka kwa style ile ile ya mtangulizi wake unless ripoti hiyo ya CAG iandaliwe kum-favor(ichakachuliwe).

Je,endapo hayo yatatokea,unadhani ni nani anastahili/anafaa kumrithi Mizengo Pinda?

Kwa maneno mengine,kuna yeyote mwenye utendaji wa kukushawishi uamini kuwa anafaa kurithi mikoba ya mh.Pinda kutoka katika baraza la mawaziri la sasa?

Kumbuka,kwa mujibu wa gazeti la Nipashe la jana tarehe 08/11/2014,taarifa ya CAG inaweza kuwasilishwa kwa spika wiki hii inayoanza kesho na kisha ikapangiwa siku ya kuwa-tabled bungeni.
 
Wapo wengi sana na wazuri, tatizo kubwa la mfumo wetu wa kupata viongozi unazuia watu wazuri kupatikana, ila unaruhusu manyang`au kupenya. Na mzuri akipenya,anajikuta analazimika kuwa hovyo ili kuendelea kuwepo duniani.
 
Komba, ili magambo tuwapoteze kabisa ktk ramani ya tz!
 
Hamna anayeridhisha.....ila kwa mfumo huu uliopo watamchagua asiye na wizara maaalum
 
MIZENGO PINDA HATACHAFUKA KWA HADITHI HIZI ZA KUUNGAUNGA - WANAOMTUHUMU WANA LAANA ZA VYAMA VYAO NA WANAJIJUA WAKINISOMA-POTELEA POTE WAJE NA POVU LA MATUSI,UJUMBE HUU WANAUSOMA KIMOYOMOYO-WANAOWATUMA KUCHAFUA WATU WAWAMBIE WAKAJIPANGE UPYA,MADUKA YAO YA WIZI YAMEFUNGWA RASMI,VIBARAKA WANATAPATAPA HAWAJUI MWAKANI KAMA watapewa MAGARI YA KUFANYIA KAMPENI HUKO MAJIMBONI KWAO KAMA WALIVYOZOEA,UJUMBE HUU NI DEDICATION KWA WASAKA TONGE WOTE NA WAPAMBE WAO!!!!
 
yule mbunge aliyekata sana mauno wakati wa bmk la miccm mzee kitoronto a.k.a jah people anafaa upm
 
Solution ni kurudi kwenye uchaguzi tu kwani hata kiranja mkuu ameshindwa kazi.
 
Sasa awe mwnamke tuandike historia.......nampendekeza mama Rwakatale au yule mbunge wa NKENGE,,,Bi. Asumpta Mshama.........au nyie mnaonajeeeeeee.....!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mfumo mbovu wa kupata viongizi na watendaji wazuri uliuwawa na uongozi wa sasa. Ndio maana most of incumbent wana uwezo mdogo katika kutekeleza majukumu yao. Dalili kubwa inaonekana hata wanapoadress public. Wanaongea vitu ambavyo ukitafakari unajiuliza hivi huyu kafikaje hapo. Uongo ndo usiseme. Naamini kwamba competent people hawawezi kudanganya. Viongozi na watendaji wakuu hupatikana through nepotism. We killed meritocracy approach. Sasa hata kama ni darasa la saba uwe tu na mtu wa kukusemea kule juu una ula. Haijalishi una uwezo au la. Unless we uprooted the rulling system-the country will remains in shambles
 
Sasa awe mwnamke tuandike historia.......nampendekeza mama Rwakatale au yule mbunge wa NKENGE,,,Bi. Asumpta Mshama.........au nyie mnaonajeeeeeee.....!!!!!!!!!!!!!!!!

.... Au Shyrose Bhanji
 
.... Jah Peopla Darasa La Saba Anafaa Sana

Majibu kama haya watu mnayatoa kwa utani ila ni kielelezo tosha kuwa watu wamekata tamaa.

Poleni watanzania wenzangu.

Ipo siku tutafika tu kule tunakokutaka.
 
Nafasi hii ibaki wazi, Rais kwa muda huu abebe jukumu hilo mpaka atakapo maliza muda wake. Lukuvi aendelee kuiwakirisha serikali bungeni (kama naye hakuguswa na kadhia hii). Tumechoka kulipa masulufu baadhi ya mawaziri wakuu wasitaafu walioiletea nchi majanga.
 
Sasa awe mwnamke tuandike historia.......nampendekeza mama Rwakatale au yule mbunge wa NKENGE,,,Bi. Asumpta Mshama.........au nyie mnaonajeeeeeee.....!!!!!!!!!!!!!!!!

Naona ume focus na Nshomiles au macho yangu tu.
 
Back
Top Bottom