Nani anashinda vita Ukraine?

Nani anashinda vita Ukraine?

Nkerebhuke

JF-Expert Member
Joined
Nov 1, 2021
Posts
796
Reaction score
2,027
Kwa heshima na taadhima naomba kuwakaribisha wanazuoni wa mambo ya vita, watafiti na wajuvi wa siasa za kimataifa kutoa elimu kuhusu nani anashinda kwenye uwanja wa medani ndani ya ukraine. Kama wewe sio mjuzi wa mambo ya medani yanayojumuisha, silaha, askari, uchumi, propaganda, mbinu na mipango ya vita tafadhari usilete ushabiki ukaharibu uzi.

Ushindi ndani ya uwanja wa vita (medani) ni jambo tata sana pale vita inapokabiliwa na propaganda nyingi sana kuliko kuupata ukweli wenyewe kutoka mstari wa mbele. Russia ni taifa kubwa sana kijeshi kulinganisha na mataifa mengi ulimwenguni hivyo kampeni yake ya kijeshi ndani ya ukraine kumeibua hisia za watu wengi sana mpaka huku kwetu Tanzania. Je jeshi la Russia limefanikiwa kuharibu na kuvunja nguvu ya jeshi la ukraine?, Je ukaraine wamefanikiwa kiasi gani kulinda nchi yao dhi ya invaders?

Pia naomba wajuzi wa mambo ya vita watoe elimu kuhusu utofauti wa na propaganda na fake news kwani wengi inaonekana hawajui maana ya propaganda ndani na nje ya uwanja wa medani.
 
Sahihisha Kwanzaa ni vita Russia na Nato
Toa maoni ambayo wenzako wata enjoy kusoma na kujifunza, weka reference namna nato anavyohusika kwa namna moja au nyingine. Lengo la huu uzi ni kutaka kupata maoni ya wajuvi wa medani ambao hawatumii hisia na hawana upande wenye uwezo mzuri wa kuchambua taarifa kisayansi.
 
Russua ameshashinda kitambo sana kwa kumega maeneo ya kimkakati. Uzi ufungwe
Naheshimu maoni yako ila nisamehe kukuambia hauna ujuzi wowote kuhusu medani, nomeshasema mwanzoni kama huna hoja pita pembeni. Hapa wanaitajika watu wanaojua ushandi wa medani unatafsiriwaje, wanaitajika watu wanaojua kwanini Russia alibadili mbuni na kuanza kutumia mizinga badala ya kuizunguka miji kwa haraka, kwanini anashambulia makazi ya watu, mashamba na viwanda. Please wajuvi njooni mtupe madini!
 
Naheshimu maoni yako ila nisamehe kukuambia hauna ujuzi wowote kuhusu medani, nomeshasema mwanzoni kama huna hoja pita pembeni. Hapa wanaitajika watu wanaojua ushandi wa medani unatafsiriwaje, wanaitajika watu wanaojua kwanini Russia alibadili mbuni na kuanza kutumia mizinga badala ya kuizunguka miji kwa haraka, kwanini anashambulia makazi ya watu, mashamba na viwanda. Please wajuvi njooni mtupe madini!
Unajaribu kuonyesha upo neutral lakini unafeli pakubwa. Unataka maoni wakati tayari una upande unaufeva. Hutaweza kukubali maoni ya upande wa pili.
 
Naheshimu maoni yako ila nisamehe kukuambia hauna ujuzi wowote kuhusu medani, nomeshasema mwanzoni kama huna hoja pita pembeni. Hapa wanaitajika watu wanaojua ushandi wa medani unatafsiriwaje, wanaitajika watu wanaojua kwanini Russia alibadili mbuni na kuanza kutumia mizinga badala ya kuizunguka miji kwa haraka, kwanini anashambulia makazi ya watu, mashamba na viwanda. Please wajuvi njooni mtupe madini!
Mnafiki mkubwa wewe, Taarifa ya CIA ni wanajeshi 15000 wa Russia wameuliwa vitani, nadhani hizi ndio habari njema upendazo.
 
Ngoja nichimbe kidogo na mimi kabla watu wa Facebook na Baikoko hawajaongezeka.
ok
ni hivi


1. Urusi imejijenga kiuchumi japo sio tishio huko duniani lakini uchumi wake ameuwekeza zaidi katika maswala ya kijeshi.

2. Kijeshi pia ipo vizuri huku akimkimbiza vizuri tu Mmarekani kwa ubunifu wa technologia za kibabe

3. maswala ya intelijensia pia kwani majasusi wa russia ndio walio sambaza formula za kutengeneza Atomic bombs zikafika russia na nchi zingine pamoja na mafanikio lukuki

Nikijikita tu katika uvamizi wa taifa la UKRAINE.

Urusi baada ya kuitwaa Krimea 2014 nilitegemea wangefanya ujasusi wa kutosha na kupiga gharama yakinifu kuliko kuingia kichwa kichwa na kupata athari zisizo tarajiwa ambazo ni mbaya

haikufanya intelijensia au ilifanya kwa uchache
matokeo yake sasa.

1. Mageneral wake wengi wakafia vitani

2. Vifaru vya kijeshi TANKS : zaidi ya 1500 kuangamizwa kabisa (irriperable)
ambapo thamani ya kifaru kimoja cha urusi aina ya T-90AM kinagharimu dola milion 4.27 sawa na bilion 9 tsh zaid ya vifaru 1500 kuangamizwa hio ni zaid ya dola 6000M zaid ya trilion 12 TSH.

3. Ndege za kivita Aircrafts 200
hapa tunaongelea ndege aina ya Sukhoi Su-35 flanker E ndege moja ya aina hii inagharimu dola milion 85 sawa na zaidi ya Tsh. 197+Bilion jumla ya hasara ya ndege hizi ni zaidi ya dola bilion 17 (TSH 40+ trilion)

3. Hasara ya Armoed vehicle 2500+ ,
troops 20000+ na helcopta Tusizipigie hesabu

4. Hasara ya wanajesh zaid ya 23000+ japo hivi vifo sio big ishu kwa russia maana urusi hua haithamin sana vifo vya wanajeshi nafkiri historia ya vita wanavyo pigana urusi mnaijua hasa kwenye swala la kupoteza askari wengi tangu WW2. na mara nyingi rusia wanashinda vita kwa wingi wa Askari. tuachane na tathmin za vifo hivi kwanza nikiweka wengi mtasema ni propaganda.
ila kwa faida tu ujue theluthi mbili ya jeshi la ardhini la russia lipo Ukraine na vita vinavyo endelea hakuna shabaha za kijeshi zinazo lengwa kwa sasa so ni mwendawazimu tu anayejua kua PUTIN atashinda hii vita.

5. Gharama za uendeshaji wa vita mishahara ya wafanya kazi penshen za wanao kufa vitani kwa familia Nk

6. Vikwazo na mali zikizokua freezed na zilizo taifishwa ni matrilion ya madolari

7. Kupoteza ushawishi wa kikanda na soko la silaha na bidhaa zingine kwa washirika wake tu kama india ni ma matrilion ya madolari pia.

Kwanza hata Ardhi yaje imeanza kushambuliwa pia wanijipigia hadi karibu na moscow halafu wanarudi. kesho tena

Ukraine imepoteza pia askari na miundombinu yenye thamani ya matrilion ya dola. lakini Mbwa kula mbuzi sio hadithi hadithi ni Mbuzi kula Mbwa.
.
Maeneo walio chukua russia yana mgogoro tangu 2014 na yalikua na udhibiti wa waasi kwa kiasi fulani. mafanikio makubwa ya rusia ni Mariupol napo ni baada ya kulipua mji wote.
Sasa Russia ili kushinda vita hivi njia pekee ni Nukes maana ujio wa HIMARS ni stori ambayo wengi hawapend kusikia.

now makombora mengi ya rusia yanatokea katika Nyambizi tu.

Source: Normal Millitary critical analysis[
 
Unajaribu kuonyesha upo neutral lakini unafeli pakubwa. Unataka maoni wakati tayari una upande unaufeva. Hutaweza kukubali maoni ya upande wa pili
Personally sina ushabiki napenda kusoma na kujifunza, kumtaja russia haimanishi nime side isipokuwa nimefanya citation kutokana na taarifa tunazopata. Kwa mfano russia kushambulia makazi ya watu ni mbinu ya kutengeneza hofu kwa adui, wakati mwingine anaweza kuchoma mashamba na kuiba nafaka kama njia ya kumlazimisha adui kujisalimisha. Russia wame outgunned ukraine kwa silaha na askari, hapa unaweza kuwasifu ukraine ku hold up defence kwani unaweza kukuta askari mmoja anakabiliana na askari watano wa Russia.
 
Naheshimu maoni yako ila nisamehe kukuambia hauna ujuzi wowote kuhusu medani, nomeshasema mwanzoni kama huna hoja pita pembeni. Hapa wanaitajika watu wanaojua ushandi wa medani unatafsiriwaje, wanaitajika watu wanaojua kwanini Russia alibadili mbuni na kuanza kutumia mizinga badala ya kuizunguka miji kwa haraka, kwanini anashambulia makazi ya watu, mashamba na viwanda. Please wajuvi njooni mtupe madini!
Haihitajiki kuwa na maarifa kujua Askari wa NATO na kina CIA wapo wanaisaidia waukraine lakini wapo unoficially Kwa sababu kuepuka mgogoro na Russia officially.wakitangaza kuwepo officially maana Yake watatangaza vita officially na Russia.
 
Wanashambulia sehemu za makazi kwa sababu askari wa Ukraine wanatumia raia kama ngao kwa kujificha kwenye makazi ya raia pamoja na mashuleni
 
Naheshimu maoni yako ila nisamehe kukuambia hauna ujuzi wowote kuhusu medani, nomeshasema mwanzoni kama huna hoja pita pembeni. Hapa wanaitajika watu wanaojua ushandi wa medani unatafsiriwaje, wanaitajika watu wanaojua kwanini Russia alibadili mbuni na kuanza kutumia mizinga badala ya kuizunguka miji kwa haraka, kwanini anashambulia makazi ya watu, mashamba na viwanda. Please wajuvi njooni mtupe madini!
Wee jamaa ni kiazi kweli kwaiyo ulifungua Uzi ili upate mawazo ya kinato NATO mjinga kabisa kwaiyo anayeshinda vita ni Nani kama si Ukrein maana maeneo yote ambayo RUSSIA alisema anayataka na kachukua tayri na kaongeza mengine
 
Back
Top Bottom