Nani anasema CHADEMA ni Imara kiasi Hicho !?

Nani anasema CHADEMA ni Imara kiasi Hicho !?

betlehem
Kama wewe hauko Imara sisi wenzio tuko imarq na tunazidi kujenga chama.
Tunashukuru kwa kukiri kwako kuwa wewe ni dhaifu na goi goi na huwezi kuwa na thaman yeyote ndani ya CHADEMA.
inshort haujawahi kuwa Mwanachama wa CHADEMA aisee.
Utahangaika sana na 2013 ndo hiyo inaoishia zake.

Nilikuwa simuelewi betlehem ila sasa nimeshamuelewa. Ila wanachama wa aina yako ni aibu sana na hasara kwa chadema. Inawezekana wewe ni chadema chumbani ndio maana unamtukana nja kumvua uanachama kamanda mwenzako kwa kutoa wazo tofauti na akili yako.
 
Last edited by a moderator:
CHADEMA iko imara maana yake nini?

Hivi kwanza CHADEMA ni nini hasa?

Hivi tunajua CHADEMA ni wazo tu!? Na wazo huwa ndani ya watu, hivyo wazo hilo huonekana kupitia matendo ya wale ambao wazo lipo ndani yao? Hivi tunajua CHADEMA ni mimi na wewe?

Chama cha siasa ni wazo tu na sio kitu yabisi ambacho kimewekwa mahali. Inashangaza sana mimi na wewe tukiwa tunasema mara kwa mara kwamba CHADEMA ni imara hali mimi na wewe hatujafanya wala hatufanyi chochote cha maana kuuweka uimara huo. Tunazungumza kana kwamba CHADEMA ni kitu "Concreate" ambacho kipo mahala na kipo "Constant".

Yatupasa tufahamu kwamba CHADEMA ni mimi na wewe, na matendo yetu ndio yanayotoa taswira ya kwamba CHADEMA ni nini, CHADEMA ni imara au ni dhaifu n.k. Kusema tu CHADEMA ni imara wakati mimi na wewe hatuna kitu chochote cha maana tunachokifanya ili kuleta au kuhakikisha uimara huo unadumu, si sahihi hata kidogo.

Jiulize hapo ulipo mpaka sasa ni nini umefanya ili kudhihirisha au kuchangia huo uimara wa CHADEMA? Kama hamna ulichofanya na hamna unachofanya, basi badilika haraka na chukua hatua 2014. Elewa CHADEMA ndio wewe! Na kuwajibika na kujituma kwako, ndio kutaifanya CHADEMA iwe imara na kinyume chake!

Elewa! Mimi na wewe tukiwa na mshikamano kwenye mambo ya msingi huo ndio uimara na taswira ya CHADEMA na tukiwa tunagawanyika gawanyika ndio udhaifu wa CHADEMA, na matendo huzungumza zaidi ya maneno.

Elewa! Tukiwa tunaonesha uwezo wetu katika kudhibiti na kutatua migogoro ndani na nje yetu huo ndio uimara wetu na tukiwa tunashindwa kufanya hivyo ndio udhaifu wetu, na matendo yanaongeea zaidi ya maneno.

Elewa! Tukiwa tunaongea hoja za msingi kila mara ndio uimara wetu na tukiwa tunaongea mambo tu ili mradi ndio udhaifu wetu, na matendo huzungumza zaidi ya maneno!.

Elewa! Tukionesha jazba (udhaifu) ndio tunaonesha taswira ya chama na tukionesha hekima (uimara)ndio tunaonesha taswira ya chama na matendo huzungumza zaidi ya maneno!

Elewa! Tukionesha chuki na visasi katika jamii yetu ndio tunaonesha taswira ya chama (udhaifu) na tukionesha busara na ustaarabu (uimara) tunaonesha taswira ya chama vile vile!

Elewa! Tukiwa tunatenda uadilifu katika jamii zetu tunatoa taswira ya chama chetu katika muelekeo huo na kinyume chake.

Haiingii akilini na wala haina maana kusikia mke na mume wanapigishana kelele mara kwa mara ndani ya nyumba mara chupa zinarushwa halafu wakitoka nje wanasema "ndoa yetu imara ati" matendo yanaongea zaidi ya maneno! (ni mfano tu jamani). Na mimi na wewe ndio tunaamua tufanye nini ili tutoe taswira gani!

Wakati tunafunga mwaka, wewe unayesema CHADEMA ni imara, jiulize, umetoa mchango gani katika uimara huo au wewe mwenyewe ni imara kiasi gani na katika jambo gani! Kwa sababu CHADEMA ni mimi na wewe. Zaidi ya hapo mimi niseme CHADEMA si imara kama ambavyo tunazungumza. Tunatakiwa tuiimarishe 2014 vilivyo kwa matendo, na ni mimi na wewe na wala sio fulani na fulani!.

Uimara wako +uimara wangu + uimara wa jamaa= uimara wa chama

Udhaifu wako+ Udhaifu wangu+ Udhaifu wa jamaa = udhaifu wa chama.

...ni kweli kamanda
 
betlehem
Kama wewe hauko Imara sisi wenzio tuko imarq na tunazidi kujenga chama.
Tunashukuru kwa kukiri kwako kuwa wewe ni dhaifu na goi goi na huwezi kuwa na thaman yeyote ndani ya CHADEMA.
inshort haujawahi kuwa Mwanachama wa CHADEMA aisee.
Utahangaika sana na 2013 ndo hiyo inaoishia zake.
Haya bwana nakutakia mwaka mpya wenye mafanikio mema.
 
Michango gani wakati walio na mawazo tofauti na wewe ni wasaliti?watu wameigeuza chadema NGO ya kupatia pesa kwa wafadhili na wanagawana mchana kweupe?40,000,000.kwa DR SLAA.80,000,000.MR MBOWE kutoka kwa Mr MENGI kugharamia mkutano mkuu wa chama 2009 zilitolewa bila maelezo na baadae zikadaiwa eti ndiye aliyekikopesha chama.Hawa ndio wachangiaji wakuu?milioni 11,000,000 kila mwezi katibu mkuu Dr Slaa kutoka chadema!hau anajitolea?Ni heri ya Zitto alikataa posho na pesa yote ya chama,akawa anafanya kwa kujitolea,leo eti msaliti,shukrani ya punda...
Huyu naye vipi ?

images


ni msaliti? upi mchango wake au ni kukwapua pesa ya chama mchana kweupe?
Hau hii familia?


ChademaMkong27otoClip_0f804.jpg
 
uadilifu ni kutembea na wake za watu?
Msikamano ni kutaka kuanzisha taifa la kaskazini?
Hoja za msingi ni kuhalalisha gongo?
Unazungumzia cdm hii nayoifaham au labda sijakuelewa?

unaweza ukathibisha kwa ushahidi ni nani anatembea na mke wa mtu mkuu?na huyo mke mumue wake ni nani? Na anasemaje kuhusu mke wake kutembea na mume mwingine?na je huyo mke anakiri yeye ni mke wa mtu?na huyo mumewe anakiri kuwa huyo ni mkewe hadi sasa?, na huyo mumewe kachukua hatua gani? Halafu baada ya kujibu hayo nenda kawaulize wakubwa zako ninini maana ya mke wamtu? Na mke wamtu anakuwa na sifa gani za kumfanya awe mke wa mtu ili akiwa na mwanaume mwingine ionekane kweli kaibiwa? Naomba majibu sahihi mkuu ''PERI'' na usichengeshe maelezo yako.
 
Wewe bwana huna hoja na huna credibility ya kui correct chadema maana wewe sio mmoja wao.Cha msingi subiri mda sio mrefu utamrejeshea prezzzooo mwenye akili kama zako mjenge chama chenu imara!11
 
Akili za kuungaunga bana.sasa ngonjera za nini hapa,umeangalia vina kuliko theme.
 
CHADEMA iko imara maana yake nini?

Hivi kwanza CHADEMA ni nini hasa?

Hivi tunajua CHADEMA ni wazo tu!? Na wazo huwa ndani ya watu, hivyo wazo hilo huonekana kupitia matendo ya wale ambao wazo lipo ndani yao? Hivi tunajua CHADEMA ni mimi na wewe?

Chama cha siasa ni wazo tu na sio kitu yabisi ambacho kimewekwa mahali. Inashangaza sana mimi na wewe tukiwa tunasema mara kwa mara kwamba CHADEMA ni imara hali mimi na wewe hatujafanya wala hatufanyi chochote cha maana kuuweka uimara huo. Tunazungumza kana kwamba CHADEMA ni kitu "Concreate" ambacho kipo mahala na kipo "Constant".

Yatupasa tufahamu kwamba CHADEMA ni mimi na wewe, na matendo yetu ndio yanayotoa taswira ya kwamba CHADEMA ni nini, CHADEMA ni imara au ni dhaifu n.k. Kusema tu CHADEMA ni imara wakati mimi na wewe hatuna kitu chochote cha maana tunachokifanya ili kuleta au kuhakikisha uimara huo unadumu, si sahihi hata kidogo.

Jiulize hapo ulipo mpaka sasa ni nini umefanya ili kudhihirisha au kuchangia huo uimara wa CHADEMA? Kama hamna ulichofanya na hamna unachofanya, basi badilika haraka na chukua hatua 2014. Elewa CHADEMA ndio wewe! Na kuwajibika na kujituma kwako, ndio kutaifanya CHADEMA iwe imara na kinyume chake!

Elewa! Mimi na wewe tukiwa na mshikamano kwenye mambo ya msingi huo ndio uimara na taswira ya CHADEMA na tukiwa tunagawanyika gawanyika ndio udhaifu wa CHADEMA, na matendo huzungumza zaidi ya maneno.

Elewa! Tukiwa tunaonesha uwezo wetu katika kudhibiti na kutatua migogoro ndani na nje yetu huo ndio uimara wetu na tukiwa tunashindwa kufanya hivyo ndio udhaifu wetu, na matendo yanaongeea zaidi ya maneno.

Elewa! Tukiwa tunaongea hoja za msingi kila mara ndio uimara wetu na tukiwa tunaongea mambo tu ili mradi ndio udhaifu wetu, na matendo huzungumza zaidi ya maneno!.

Elewa! Tukionesha jazba (udhaifu) ndio tunaonesha taswira ya chama na tukionesha hekima (uimara)ndio tunaonesha taswira ya chama na matendo huzungumza zaidi ya maneno!

Elewa! Tukionesha chuki na visasi katika jamii yetu ndio tunaonesha taswira ya chama (udhaifu) na tukionesha busara na ustaarabu (uimara) tunaonesha taswira ya chama vile vile!

Elewa! Tukiwa tunatenda uadilifu katika jamii zetu tunatoa taswira ya chama chetu katika muelekeo huo na kinyume chake.

Haiingii akilini na wala haina maana kusikia mke na mume wanapigishana kelele mara kwa mara ndani ya nyumba mara chupa zinarushwa halafu wakitoka nje wanasema "ndoa yetu imara ati" matendo yanaongea zaidi ya maneno! (ni mfano tu jamani). Na mimi na wewe ndio tunaamua tufanye nini ili tutoe taswira gani!

Wakati tunafunga mwaka, wewe unayesema CHADEMA ni imara, jiulize, umetoa mchango gani katika uimara huo au wewe mwenyewe ni imara kiasi gani na katika jambo gani! Kwa sababu CHADEMA ni mimi na wewe. Zaidi ya hapo mimi niseme CHADEMA si imara kama ambavyo tunazungumza. Tunatakiwa tuiimarishe 2014 vilivyo kwa matendo, na ni mimi na wewe na wala sio fulani na fulani!.

Uimara wako +uimara wangu + uimara wa jamaa= uimara wa chama

Udhaifu wako+ Udhaifu wangu+ Udhaifu wa jamaa = udhaifu wa chama.


ccm ni chama chakavu......
 
uadilifu ni kutembea na wake za watu?
Msikamano ni kutaka kuanzisha taifa la kaskazini?
Hoja za msingi ni kuhalalisha gongo?
Unazungumzia cdm hii nayoifaham au labda sijakuelewa?

We are only responsible for what we say and write, what you understand thereafter is your business
 
unaweza ukathibisha kwa ushahidi ni nani anatembea na mke wa mtu mkuu?na huyo mke mumue wake ni nani? Na anasemaje kuhusu mke wake kutembea na mume mwingine?na je huyo mke anakiri yeye ni mke wa mtu?na huyo mumewe anakiri kuwa huyo ni mkewe hadi sasa?, na huyo mumewe kachukua hatua gani? Halafu baada ya kujibu hayo nenda kawaulize wakubwa zako ninini maana ya mke wamtu? Na mke wamtu anakuwa na sifa gani za kumfanya awe mke wa mtu ili akiwa na mwanaume mwingine ionekane kweli kaibiwa? Naomba majibu sahihi mkuu ''PERI'' na usichengeshe maelezo yako.



kweli we ni chausikukitamu
 
Mimi ntapiga kampeni kwa wanafunzi mwakani kura zao kwa chadema
 
Nilikuwa simuelewi betlehem ila sasa nimeshamuelewa. Ila wanachama wa aina yako ni aibu sana na hasara kwa chadema. Inawezekana wewe ni chadema chumbani ndio maana unamtukana nja kumvua uanachama kamanda mwenzako kwa kutoa wazo tofauti na akili yako.

Haha! Sasa Kama yeye ni Chumbani wewe ni wapi? Kitandani? Au Chooni?
 
Last edited by a moderator:
Michango gani wakati walio na mawazo tofauti na wewe ni wasaliti?watu wameigeuza chadema NGO ya kupatia pesa kwa wafadhili na wanagawana mchana kweupe?40,000,000.kwa DR SLAA.80,000,000.MR MBOWE kutoka kwa Mr MENGI kugharamia mkutano mkuu wa chama 2009 zilitolewa bila maelezo na baadae zikadaiwa eti ndiye aliyekikopesha chama.Hawa ndio wachangiaji wakuu?milioni 11,000,000 kila mwezi katibu mkuu Dr Slaa kutoka chadema!hau anajitolea?Ni heri ya Zitto alikataa posho na pesa yote ya chama,akawa anafanya kwa kujitolea,leo eti msaliti,shukrani ya punda...

Nataman nkutukane ww na huyo kibaraka wako anaitwa zitto

Akat zitto anawadanganya akina shoza na mtela mlisema chadema inamuogopa sasa kaekwa mtu kati mnnaanza anaonewa,hivi ninyi ni viumbe gan? Hamna maana
 
Mkuu Bethlem umeandika kitu cha busara sana na ninaweza kusema ni cha kifilozofia pia, kwani uko sahihi kuwa chama ni kitu cha kufikirika yaani concept na huvaa uhalisia pale ambapo watu wanaokubaliana na wazo hili wanapoamua kuchukua hatua na kwa vitendo kutekeleza wazo hili. Ukishaelewa hili unakuwa umepiga hatua kubwa kimawazo kuliko watu ambao hufuata mkumbo bila kuelewa chanzo halisi. Mfano wako wa ndoa pia ni mfano mzuri na umeleta mjadala mzuri na ushauri wako ni wa kuzingatiwa na wanachama na viongozi wa Chadema.
 
kwanini viongozi wa wilaya hawalipwi ila dr.slaa na viongozi wa juu wanajilipa?

Kwasababu chadema ni kampuni na Managers ni hao walioko juu, huko wilayani ni vibarua waendelee kujitolea tu chama hakina hela.
 
Nataman nkutukane ww na huyo kibaraka wako anaitwa zitto

Akat zitto anawadanganya akina shoza na mtela mlisema chadema inamuogopa sasa kaekwa mtu kati mnnaanza anaonewa,hivi ninyi ni viumbe gan? Hamna maana

...ngoja tulifukuze kabisa hilo li zzk lao,maana tumechoka sasa na hawa wazushi...
 
Akili za kuungaunga bana.sasa ngonjera za nini hapa,umeangalia vina kuliko theme.

Ndugu,hawa wafuasi wa traitor zitto yaani wanatapa tapa kweli,wangekuwa wapo karibu ilitakiwa kuwachapa vibao kwa kubwabwaja kwao. Any way siyo mda mrefu tutawapa zitto wao ili waanzishe chama chenye yote watakayopenda wao.
 
Back
Top Bottom