Nani amemroga Profesa Palamagamba Kabudi?

Nani amemroga Profesa Palamagamba Kabudi?

Sikuwa mwanafunzi wa sheria UDSM,lakini kila nilipokuwa namwona prof Kabudi akichambua mada za kisheria, nilimkubali sana. Imani yangu kwake ilinitoka baada ya kutoa ushauri wa ajabu akiwa rafiki wa mahakama katika kesi ya mgombea binafsi. Nafikiri bila ushauri ule sasa hivi tungekuwa na mgombea binafsi.

Dawa yake ni hii; akiwapa mtihani andikeni majibu ya uongo ili mfeli wote.akiwaita kwa supu ndiyo mfanye vizuri, sifa yake itakuwa imebomoka
 
Ule mswada wa kununua mali chakavu umeanza kutekelezwa.

Huyu Palamagamba ni mwanasheria mwenye mawazo chakavu yanayofaa kutumiwa sasa na serikari kwa kufanya mambo ya dharura kama kufunika haki ya watanzania kujadili katiba na kuamua yale wanayodhani yanachangia kuleta hali mbaya ya nchi.

Usomi wa majina ni mbaya zaidi kuliko ujinga wa elimu. Huyu Palamagamba na Benson wanafaa kwa kughani mashairi tu.
 
Nilikuwa naye A Level kule Mirambo! Huyu alikuwa ni mwanamapinduzi kweli- aliamini wanaotetea 'status quo' ni michwara na aghalabu ni wadhanifu wasioweza kuona mambo kiyakinifu, aliwaita mabepari uchwara na waliopenda kuhoji kwa kiingereza aliwabeza watumwa na mara nyingi aliwafananisha na vibepari au vikabwela!

Huyu sio Kabudi tuliyemfahamu! Sidhani kuna Uchadema au UCCM katika hoja hii, ila Kabudi tuliyemfahamu siye huyu! KALOGWAAAAA
 
To be honest, I have Never admired Professor Kabudi as a legit intellectual in Tanzania. Huyu jamaa ni intellectually bankrupt!
 
Mimi simpendi tangu pale alipondisha haki yetu ya msingi kwa kutumia uanasheria wake kukataa
Indepent candidate.

Hawa ndiyo akina Yuda Isikarioti wa karne hii, inabidi tuwaepuka.
 
Prof. Palamagamba kabudi

images


Hii ndo SOurce ya NENO GAMBA

Na anawapala kikweli kweli magamba
 
KABLA BUNGE HALIJAAHIRISHWA MCHANA HUU MWANASHERIA MKUU NA ADUI /RAFIKI WA PAA LA MAGAMBA KABURI,NIMEMSIKIA AKIMSIFIA ETI ALIFANYA UCHAMBUZI YAKINIFU

WAKATI MNYIKA ANAMJIBU AG ALITAKA KUSEMA KUWA NA YEYE ALIKUWEPO KWENYE SEMINA YA PAA LA MAGAMBA KABURI ILA MAMA KINDA AKAMZUIA NA KUMUAMURU AENDE KWENYE HOJA

paaa la magamba kaburi
 
Pension ni kikwazo kikubwa kwa wanataaluma jamani....Akiangalia miaka yakufanya kazi na hazina yake ina kiasi gani anaona huu ndiyo wakati wa yeye kuziba mashimo yale yakizazi kijacho yataji solve yenyewe huko mbeleni.
 
Pension ni kikwazo kikubwa kwa wanataaluma jamani....Akiangalia miaka yakufanya kazi na hazina yake ina kiasi gani anaona huu ndiyo wakati wa yeye kuziba mashimo yale yakizazi kijacho yataji solve yenyewe huko mbeleni.

hahahahahaaaaaaaaaaaaaaaaaa! na hapo ndo vijana tunapoonekana kama ni dampo la matatizo ya siku zijazo. lazima tukomae sasa ili huu upuuzi usije wafikia wajukuu zetu
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Umenikumbusha kitu kimoja. Unajua ile sheria namba 5/4??? ya mazingira ya tanzania, jamaa alichukua ya ujerumani akaitafsiri word to word then bungeni akapigiwa makofi kishenzi kwa 'kazi nzuri' ya kuandika sheria nzur ya mazingira. Wizarani tulimshtukia mapema lakini kama ungesema wakati ule ingekuwa nomaaaaaaaaa!
 
Hii ndo ilikuwa njia panda yake...pale ndo nami nilipigwa na butwaa kuwa huyu gwiji wa constitutional law kawaje? lazima kageuzwa bidhaa, tena a cheap very well read bidhaa. ni aibu sana kwake na yote aliyoyasimamia tangu awali. you have to live and stick to your principles...sio kugeuka jiwe tena ghafla bin vuu tena wakati ule ambao mchango wako unategemea zaidi na jamii yako. Aibu kwako sana palamagamba kabudi tena sana!

...........toka alipoungana na serikali kupoka haki ya uraia wa mtanzania (ugombea binafsi) na kwenda kinyume na mawazo ya baba wa Taifa kuhusu haki ya uraia ambayo ni haki ya kuchagua na kuchaguliwa, nilijua kuna kitu kimemtokea Prof. lakini sijui ni kitu gani, ni suala la wakati tu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
nina wasiwasi na uraia wake.kama anatoka ngara atakuwa ni mkimbizi.Hana uchungu na nchi
 
Fununu zilizovuja kutoka Ikulu ni kwamba Prof. Palamagamba Kabudi ndiye aliyeanza kuandika muswada wa katiba kabla ya kurejeshwa serikalini kwa marekebisho, Na kitu alichokifanya ni kuunakiri (copy) muswada ule wa Kenya na kuhariri(Edit) baadhi ya vipengele hasa kwa kuongeza mambo ambayo rais na CCM walikuwa wakiyataka.

Ni wazi atatetea muswada huo. Kwa ujumla anajua anachokifanya, He is opportunistic, soon he will be awarded certain senior political post. Wapo wengi tu kama yeye ambao tulikuwa tunawaamini sana lakini wakageuka kabisa: eg Prof. Lwekaza Mukandara (Sasa VC), Dr.Benson Bana (Mshauri wa Rais-Uchumi), Dr.Masumbuko Lamwai (Mwanasheria wa CCM) nk.
 
Kuna wakati Prof.Baregu aliwaita baadhi ya ma Prof 'THERE ARE ACADEMIC PROSTITUTES" wachache walimuelewa na wengi walimdhihaki, ila alimaanisha kuwa wanataaluma wenzake wanakiuka miiko ya taaluma zao kwa kupewa fedha na ahadi na wanasiasa na kufanya yale wanasiasa wanayo yataka na sio kusimamia taaluma zao zinavyotaka.

Leo haya maneno na haya mambo yanajidhihirisha kabisa kwa maprof wengi wa Tanzania
 
  • Thanks
Reactions: Ame
nina wasiwasi na uraia wake.kama anatoka ngara atakuwa ni mkimbizi.Hana uchungu na nchi

Wacha ubaguzi wako wewe....kwani nani alikwambia wote wanaoishi Ngara ni wakimbizi? watch out your words. Ndo ubaguzi na siasa za kishenzi kama hizi tunazipiga vita zisiwe na nfasi ndani ya TANZANIA yetu huru tunayotaka kuijenga kwa katiba mpya.

Keep calm, carry on:embarassed2:
 
Back
Top Bottom