Ni takribani mara ya tatu sasa ambapovituo vinavyouza nishati ya mafuta (petrol,diesel) vimesuasua hasa baada ya bei mpya kutangazwa na ewura. Nakumbuka ilikuwa july mwaka huu ambapo mabo yalikuwa mabaya zaidi juu ya suala hili. Pamoja na haya yote serikali ilishindwa kutoa tamko la karipio kwa wamiliki na wauzaji wa nishati hii.
wakafanya danganya toto kuwa BP imefungiwa kwa kukiuka agizo la serikali lakini baada ya muda mfupi tukaona vituo vya BP vinauza mafuta kama kawaida.
Haya yote yamesababishwa na sera hii ya serikali ya ubinafsishaji ambapo serikali iligawa kila kitu bila kufikiria hatma ya haya yote. iliua TIPA iliyokuwa inaingiza crude oil na kuisafisha hapa nchini ambapo bei ya mafuta ilikuwa ndogo sana wakati ule. Serikali hii hii ikaua TPDC ikizani kuwa ndiyo inajenga sasa haya ndo matokei yake.
Hiyo n sekta moja tu sasa hebu fikiria siku hawa VODACOM,AIRTEL,TIGO ZANTEL NA SASATEL wakigoma ni wangapi ambao bado wanatumia ttcl na coverage yake kwa Tanzania ikoje? wenye vyombo vya usafirishaji nao wakigoma ni makampuni mangapi ya umma ambayo yapo na yanaendelea kutoa huduma hii?
Jamani hata kama ni ubinafsishaji baadhi ya sekta serikali lazima ziwe za serikali bado na nguvu na si kuleta mchezo kwa sekta nyeti kama hizi za mawasiliano na usafirishaji.
wakafanya danganya toto kuwa BP imefungiwa kwa kukiuka agizo la serikali lakini baada ya muda mfupi tukaona vituo vya BP vinauza mafuta kama kawaida.
Haya yote yamesababishwa na sera hii ya serikali ya ubinafsishaji ambapo serikali iligawa kila kitu bila kufikiria hatma ya haya yote. iliua TIPA iliyokuwa inaingiza crude oil na kuisafisha hapa nchini ambapo bei ya mafuta ilikuwa ndogo sana wakati ule. Serikali hii hii ikaua TPDC ikizani kuwa ndiyo inajenga sasa haya ndo matokei yake.
Hiyo n sekta moja tu sasa hebu fikiria siku hawa VODACOM,AIRTEL,TIGO ZANTEL NA SASATEL wakigoma ni wangapi ambao bado wanatumia ttcl na coverage yake kwa Tanzania ikoje? wenye vyombo vya usafirishaji nao wakigoma ni makampuni mangapi ya umma ambayo yapo na yanaendelea kutoa huduma hii?
Jamani hata kama ni ubinafsishaji baadhi ya sekta serikali lazima ziwe za serikali bado na nguvu na si kuleta mchezo kwa sekta nyeti kama hizi za mawasiliano na usafirishaji.