Nancy Nyalusi afanya Ziara ya Kikazi Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo - Iringa

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,886
938
MHE. NANCY NYALUSI AFANYA ZIARA YA KIKAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA KILOLO - IRINGA

MBUNGE wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa (CCM) Mhe. Nancy Nyalusi amefanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya Kilolo mkoani Iringa katika kijiji cha Ng'uruwe ambapo amachangia Shilingi Milioni 1 kwenye ujenzi matundu ya choo kwenye Shule ya Msingi Masege kama sehemu ya mkakati wake kusaidia juhudi za Serikali kuweka mazingira mazuri kwenye maeneo ya kujifunzia kama shule.

Ziara hiyo ni muendelezo wa Mbunge huyo kwenye maeneo mbalimbali mkoani Iringa ikiwa ni utekelezaji shughuli zake za kibunge.

"Nimekuja hapa wilayani Kilolo katika eneo hili na kwenye shule hii kujionea mwenyewe ni kwa jinsi gani nami kama Mbunge naweza kuwa na mchango katika kuboresha mambo hatimaye sote tukawa kwenye mazingira mazuri" - Mhe. Nancy Nyalusi alisema.

Katika hatua nyingine Mbunge huyo amewahimiza vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kuacha kubweteka na badala yake kuchangamkia fursa za mikopo ambazo Serikali ya awamu ya sita ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imeziweka kupitia mikopo inayopatikana kwenye Halmashauri zote nchini.

"Jamani Serikali yetu imeweka mikakati mizuri sana kusaidia makundi haya ya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kupitia mikopo ya Halmashauri zetu, Rais wetu anatupenda sana tusiache bahati hii ndugu zangu" - Alisisitiza Mhe. Nyalusi.

#KaziIendelee
#CCMIringa
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2023-02-22 at 12.58.45.jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-22 at 12.58.45.jpeg
    96.5 KB · Views: 3
  • WhatsApp Image 2023-02-22 at 12.58.44.jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-22 at 12.58.44.jpeg
    75.5 KB · Views: 5
  • WhatsApp Image 2023-02-22 at 12.58.46(1).jpeg
    WhatsApp Image 2023-02-22 at 12.58.46(1).jpeg
    70.9 KB · Views: 3
Jf inashushwa hadhi kwa kiwango cha kutisha. Hii habari inatusaidia nini sisi wa Kyela?
KENGE
 
Sio Ng'uruwe ni Ng'uruhe wewe maamuma. Mbona sisi wakazi wa Ng'uruhe hatujamuona hapa au alienda sehemu Gani?
 
Sasa Mbunge wa Viti Maalumu analisaidia vipi Jimbo? Si Mbunge wa Jimbo yupo?
Mbunge wa viti maalum hushughulika na makundi maalum, pili shule ni jukumu la kila Mtanzania hivyo hajakosea.

Amefanya kama mdau wa maendeleo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom