Namwonea huruma Rais wa 2015 awe CCM au UKAWA

Namwonea huruma Rais wa 2015 awe CCM au UKAWA

Kibo10

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
11,278
Reaction score
8,868
Serikali hii ya ccm kuna watu wanaipongeza kwa kupunguza madeni ya walimu, wanachosahau serekali hii hii...inatakiwa kulipa madeni ya wabunge ambayo wanadai kwa muda mrefu sasa,Waheshimiwa wengi mpo hapa kujeni mseme kama nadanganya.

Haya nayasema si kwa bahati mbaya ila nilisikia jana Naibu Spika, Job Ndugai, akilalama waheshimiwa mifuko yao ni meupe hawana fedha,walimu wamepunguzwa kutoka bilion 60 na sasa wanadai billion 4 Lakini cha kusikitisha leo hii Muhimbili hamna dawa hata moja hazina kweupeee...serekali imekuwa mufilisi lakini kuna mazuzu wanajisifu.

Nimejiuliza hivi JK atapata wapi pesa za kuwalipa hawa wachina na wazungu kama wamechoka kumkopesha? maana sasa hawamkopeshi tena nasikia wanataka chao tu....namwonea huruma sana Rais wa 2015 atakavyochukuwa nchi ikiwa sakala awe wa Ukawa au hata wa hao CCM!
 
Le Prof sio ajabu akaipiga mnada na ya magogoni sheikh maana kwingine kote keshamaliza

Tena ataipiga bei ili alipe madeni ya wauguzi na wabunge
Maana deni ni deni tu dawa yake kulipa!
 
Kuwa ccm ni shida,ona wanavojibu hoja hovyo hovyo.Hivi ukiwa ccm lazima akili zako uweke mfukoni halafu ujazwe upepo?Taifa litaendelea kwa fikra mbovu kiasi hiki?
 
Le Prof sio ajabu akaipiga mnada na ya magogoni sheikh maana kwingine kote keshamaliza

Rejea msemo wa waswahiri'kimfaacho mtu ndio chake,watu wa Ccm wanaamini Ikulu ya magogoni niyakwao kama vile viwanja vya mpila na ofisi za Ccm bila kujua 2016 wataanza upya kutafuta viwanja wajenge ofisizao huku wakiwa wapinzani
 
bwana kibo10 umenena kamanda, hata hao mazuzu wa nnauye wanaokukejeli ukwel wanaujua, kiukwel rais ajae atapata shida sana hasa akiwa mwadilifu ataumoza kichwa jinsi gan apunguze ukali wa maisha ya watz maana huyu jamaa hana jinsi tena ya kutupunguzia ukali wa maisha, alichobakiza ni kulandalanda dunian kote ili kuongeza den la taifa aweze japo kuwalipa washikji zake mpaka imefikia kipndi anahisi siku haziendi anataman achie ngazi ha kesho maana hana mbinu mbadala za kutuokoa.
 
kama akiwa rais kutoka ccm ndio itakuwa tabu lakini Rais akitoka upinzani jambo la kwanza ni kuchukua mali zote walziojilimbikizia viongozi wa ccm kulipia madeni
 
Kuwa ccm ni shida,ona wanavojibu hoja hovyo hovyo.Hivi ukiwa ccm lazima akili zako uweke mfukoni halafu ujazwe upepo?Taifa litaendelea kwa fikra mbovu kiasi hiki?

Yani hiki kizazi cha njoka ni hasara mkuu
 
bwana kibo10 umenena kamanda, hata hao mazuzu wa nnauye wanaokukejeli ukwel wanaujua, kiukwel rais ajae atapata shida sana hasa akiwa mwadilifu ataumoza kichwa jinsi gan apunguze ukali wa maisha ya watz maana huyu jamaa hana jinsi tena ya kutupunguzia ukali wa maisha, alichobakiza ni kulandalanda dunian kote ili kuongeza den la taifa aweze japo kuwalipa washikji zake mpaka imefikia kipndi anahisi siku haziendi anataman achie ngazi ha kesho maana hana mbinu mbadala za kutuokoa.

Umenena kamanda!
Hawa walevi wa ccm wala hawanitishagi mkuu ninawamudu vizuri tu kamanda!!
 
Back
Top Bottom