"Shetani"alirubuni viongozi watatu wa Chadema wakaasi mamlaka na kupanga hujuma.Mamlaka ikaamua waadhibiwe kwa kutupwa kwenye "jehanamu"ya dunia ili kama wanataka kwenda kuishi na "shetani" (ccm) wawe huru ila nafasi ya kutubu ikatolewa. Leo viongozi hao wakaitisha press conference kusema yaliyo moyoni.
"Shetani" kwa kudhani viongozi hao watakamilisha kazi yake aliyowatuma ya kuiharibu Chadema kwa kuitusi na kusema maneno ya kugonganisha watu akahakikisha press hiyo inarushwa hewani ili watu wote wasikie na mkakati wake ufaulu.
Bila kujua kuwa wokovu umewashukia viongozi hao wawili na wamejitambua walilotenda na maumivu waliyowa watu waliokuwa wanawapenda, "shetani" akaaibishwa baada ya hao viongozi kusema hawaondoki Chadema na kuwa kujikwaa sio kuanguka.
Sasa nawashauri Kamati kuu kupokea utetezi wao na kama utakuwa katika hali ya unyenyekevu kama tulioona leo basi wasifukuzwe Chamani ila wapewe onyo kali kama taratibu zilivyo. Nafasi ya kurudi uongozini ipo tuu mradi matendo yao yatadhihirika kuwa yako sawa.
Kiukweli ni kuwa "Shetani" ameaibika kwa mpango wake wa muda mrefu kubomolewa bila kutegemea.