Namuonya Mwigulu Nchemba - Kitila Mkumbo

Namuonya Mwigulu Nchemba - Kitila Mkumbo

Kuna jambo linaendelea hapa ambalo bado wengi hatujalitambua. Yote tanayotokea CDM ikiwa ni pamoja na kuvuliwa vyeo Bwana ZZK na Dr Mkumbo,bado picha haijasomeka. Kuna "conspiracy theory" ambayo it will take time for us to learn it. Haiwezekani Kitilya aseme "inyeshe mvua au liwake jua ni lazima atamvaa katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Iramba Magharibi ama kupitia Chadema au kwa njia nyingine yoyote". That means kuna political game inayoendelea ndani ya CDM!

Ni mtazamo tu.
 
Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema aliyetimuliwa hivi karibuni Dr Kitila Mkumbo amemuonya vikali Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba kwamba akae mbali na yeye.

Dr Kitila amedai kushangazwa na machozi ya mamba ya Mwigulu ambaye kwa unafiki mkubwa eti amemsikitikia kwa yaliyomfika.

Dr Kitila amesema siku zote Mwigulu Nchemba amekuwa akimchafua lakini tangu atimuliwe uongozi Chadema Mwigulu amejifanya kumsifu sana na kumhurumia.

Dr Kitila amemuonya Mwigulu kwamba inyeshe mvua au liwake jua ni lazima atamvaa katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Iramba Magharibi ama kupitia Chadema au kwa njia nyingine yoyote.

Dr Kitila amemtaka Mwigulu kutambua kwamba yeye bado ni mwanachama wa Chadema.

katika ule waraka wao walisema watajitahidi kuwa mbali na ccm na kuungana na viongozi wengine wa chama ili waaminike, pia watajaribu kupunguza jazba pamoja na kugundulika na viongozi wa CDM ili wafanikishe malengo yao maovu ya kukiua chama
 
Nimeshangazwa sana na Kitila kwamba ndiye aliyeandika masengenyo yale.nilichomshangaa zaidi ni kutokujua kuwa yote hayo aliyokuwa anafanya yalikuwa na mkono wa CCM kupitia kwa Mwigulu.Ni ajabu kuwa pamoja na weledi wake ameshindwa kubaini hilo na kushangaa kusifiwa na Mwigulu!
 
Nikulizwa ni Mbunge gani humpendi kati ya Wabunge wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania-Jibu ni Mwigulu Nchemba


Nikiulizwa Mwanasiasa gani humpendi Afrika Mashariki jibu ni Mwigulu Nchemba

Nikiulizwa kiongozi gani wa Chama chochote cha siasa hapa Tanzania humpendi Jibu ni Mwigulu Nchemba!!



Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema aliyetimuliwa hivi karibuni Dr Kitila Mkumbo amemuonya vikali Naibu Katibu Mkuu CCM Mwigulu Nchemba kwamba akae mbali na yeye.

Dr Kitila amedai kushangazwa na machozi ya mamba ya Mwigulu ambaye kwa unafiki mkubwa eti amemsikitikia kwa yaliyomfika.

Dr Kitila amesema siku zote Mwigulu Nchemba amekuwa akimchafua lakini tangu atimuliwe uongozi Chadema Mwigulu amejifanya kumsifu sana na kumhurumia.

Dr Kitila amemuonya Mwigulu kwamba inyeshe mvua au liwake jua ni lazima atamvaa katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Iramba Magharibi ama kupitia Chadema au kwa njia nyingine yoyote.

Dr Kitila amemtaka Mwigulu kutambua kwamba yeye bado ni mwanachama wa Chadema.

ha ha haaaa!

jamani!!
 
Dr.Mkumbo anaweza kuja kufikia ngazi ya juu ya uongozi ndani ya nchi hii.

hongera kwa kujiweka huru Dr..!!!
 
wanafiki ndiyo walivyo , ukiharibu wanakushangilia ,ukifanya vema wananuna ! akili kichwani mwako dr kitila .
 
Kuna jambo linaendelea hapa ambalo bado wengi hatujalitambua. Yote tanayotokea CDM ikiwa ni pamoja na kuvuliwa vyeo Bwana ZZK na Dr Mkumbo,bado picha haijasomeka. Kuna "conspiracy theory" ambayo it will take time for us to learn it. Haiwezekani Kitilya aseme "inyeshe mvua au liwake jua ni lazima atamvaa katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Iramba Magharibi ama kupitia Chadema au kwa njia nyingine yoyote". That means kuna political game inayoendelea ndani ya CDM!

Ni mtazamo tu.

Jamani Zitto ni msaliti, alichokifanya leo ni kutafuta huruma ya wananchi. Nilikuwa maeneo ya vijana wa Lumumba, nikajifanya nami mwanaLumumba, niliyoyasikia kuhusu Zitto yanatisha. Ningejitambulisha kama kamanda wa chadema, kwakusikia yale maneno ningesema ccm wanatengeneza mazingira ambayo ni unrest ndani ya chama. Zitto is a snake!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Huyo Mkumbo aache mzaha wa kipuuzi,
Pamoja na u dr wake hakujua kuwa huyo Zitto anayemuunga mkono anafanya kazi moja na Nchemba?
Akawalaghai watoto wa chekechea.
 
"Shetani"alirubuni viongozi watatu wa Chadema wakaasi mamlaka na kupanga hujuma.Mamlaka ikaamua waadhibiwe kwa kutupwa kwenye "jehanamu"ya dunia ili kama wanataka kwenda kuishi na "shetani" (ccm) wawe huru ila nafasi ya kutubu ikatolewa. Leo viongozi hao wakaitisha press conference kusema yaliyo moyoni.
"Shetani" kwa kudhani viongozi hao watakamilisha kazi yake aliyowatuma ya kuiharibu Chadema kwa kuitusi na kusema maneno ya kugonganisha watu akahakikisha press hiyo inarushwa hewani ili watu wote wasikie na mkakati wake ufaulu.
Bila kujua kuwa wokovu umewashukia viongozi hao wawili na wamejitambua walilotenda na maumivu waliyowa watu waliokuwa wanawapenda, "shetani" akaaibishwa baada ya hao viongozi kusema hawaondoki Chadema na kuwa kujikwaa sio kuanguka.
Sasa nawashauri Kamati kuu kupokea utetezi wao na kama utakuwa katika hali ya unyenyekevu kama tulioona leo basi wasifukuzwe Chamani ila wapewe onyo kali kama taratibu zilivyo. Nafasi ya kurudi uongozini ipo tuu mradi matendo yao yatadhihirika kuwa yako sawa.
Kiukweli ni kuwa "Shetani" ameaibika kwa mpango wake wa muda mrefu kubomolewa bila kutegemea.

Shetani umeshindwa uendr kuzimu kwenye moto mkali. Hatoki mtu hapa! CHADEMA yatosha
 
Kitila ni muungwana.

Alikiri makosa na kuomba msamaha kwenye CC ya chadema. Nina hakika pia ataomba msamaha katika maelezo yake ya utetezi atakayowasilisha mbele ya CC.

Tamko la Kitila limejaa uungwana. Ni mtu aliyetambua makosa yake na sasa anatubu. Nashauri huyu asamehewe ila abaki kuwa mwanachama tu.


Zitto pia atafanya vivyo hivyo.

Tatizo la zitto ni unafiki, yaani huku uraiani hataki kuonekana amekosa. Akienda huko kwenye vikao anaomba msamaha. Ni mnafiki wa kutupwa.

Alichokifanya leo ni kujitungia tuhuma nyingine tofauti na zile alizopewa kwenye CC. Halafu akaanza kuzijibu mwenyewe ili aonekane hana makosa.

Tamko la Zitto bado limekaa kishari shari na unafiki mwingi.

Nashauri huyu aondolewa tu kwani mtu wa namna hii ni hatari sana.

kwenye bluu hapo umezingatia asili na tabia ya watu wanaotokea Kigoma?????
Ubishi
 
Back
Top Bottom