Barubaru
JF-Expert Member
- Apr 6, 2009
- 7,161
- 2,323
Wanajamii.
Kama waTanzania hususan wale waliotoka Bara (Tanganyika) msingekuwa watu wa kulalamika na kulaumu kwa kila jambo na kusahau kabisa kuwa wazalendo na kushukuru kwa kile kidogo mnachopata na kujewekezea.Nitakuwa mbadhilifu wa Fadhila kama sikusema kuwa Tz imejitahidi sana kuweka miundo mbunu bora ya kujenga uchumi imara wa Tz.
Hapo awali nilizungumzia WAANDISHI wa habari wa Tanzania wamekosa uzalendo kwa nchi yao. Napenda kusimamia kwa kauli hii kwani nimeona mengi kwa hizi siku sabaa nilizokaa tanzania.
Ningependa kuwarudisheni katika Uchumi utaona Sera bora za kukuza uchumi wa nchi yoyote ile na hususan nchi masikini ni kuweka miundo mbinu Bora ya Usafiri kama barabara, Kuwa na nishati ya uhakika na kuwa na Sera bora za uwekezaji ikiwemo pamoja na Amani na utulivu wa sehemu hisika na vivutio natural kwa wawekezaji kama madini, ardhi safi n.k.
Kwa hayo hapo juu utaona Tanzania hususan Tanganyika wamebarikiwa kila kitu kasoro kulikuwa hakuna miundombinu Bora ya barabara na Nishati ya stima yyenye uhakika.
Kwa kipindi kifupi sana nimetembelea Mwanza kwa kupita barabara kupitia geita, Buseresere, Bwanga, Chato mpaka Muleba na kukomea kamachumu. Na kurudi nilipitia Biharamulo, Lusaunga, Nyakanazi, Lunzewe, ushirombo mpaka kahama, nzega na kuingia Tabora na baadae kurudi mpaka Mwanza kupitia Nzega, Tinde, shinyanga kufika Mwanza.
Jana niliingia Mtwara na leo nimetembea mpaka Kilwa kilanje lanje mpaka Ngurukuru kuona Kiwanda cha Rufiji Cement . Hakika Rais Kikwete amejitahidi sana kuweka miundo mbinu bora ya barabara za lami. Takriban lami imetawala kwingi kinachosubiriwa ni upatikanaji wa nishati ya Stima.
leo ningependa kuwashauri waTz acheni kulalamika Mtwara kuna fursa nyingi sana za uwekezaji. Kwani pamoja na kuwa na Gas na hivyo kuwa na umeme wa uhakika, lakin pia kuna mables ambazo ni malighafi safi kwa utengenezaji wa Saruji, Ardhi ni bora sana kwa kilimo cha alizeti, ufuta, korosho. Vile vile kuna beach nyingi sana na nzuri sana kuanzia msanga mkuu na maeneo yote a mikindani mpaka Lindi.
Lakin kubwa zaidi ni kuwa kuna Bandari kubwa sana. Kwani i lango kuu l kusafirishia bidhaa na la kupokelea malighafi za viwanda. Nilikuwa nikipitia sera ya Tz kuhusu Mtwara Corridor nimezipenda sana na kuona kuwa kuna mengi sana sio tu ya kujifunza lakin pia kuwekeza.
Nawashauri wana JF. Mkumbuke kuwa mtaji mkubwa wa kiuchumi ni AKILI ZENU, mengine yote ni matokeo. Acheni kulalamika umaskini wakti fursa zipo nyingi sana zipo kwenu. Kuna mahotel mazuri sana ya kulala vile vile kuna Makonde beach club, maisha Club, safari Lounge na mengine. Vile vile kuna Radio mbili maarufu Pride FM na Safari Radio. Zote hizo zinatoa taswira safi sana kwa mji wa Mtwara. Flight za uhakika nimekuja na 540. lakin hata precission nao wanakuja mara mbili kwa siku.
Namaliza kwa kumpongeza sana sana Rais Kikwete kwa kuweka na kujenga Msingi mkuu wa kuinua uchumi wenu kwa kutengeneza barabara bora na kuanza project ya kuhakikisha Umeme unakuwa wa uhakika.
Kama waTanzania hususan wale waliotoka Bara (Tanganyika) msingekuwa watu wa kulalamika na kulaumu kwa kila jambo na kusahau kabisa kuwa wazalendo na kushukuru kwa kile kidogo mnachopata na kujewekezea.Nitakuwa mbadhilifu wa Fadhila kama sikusema kuwa Tz imejitahidi sana kuweka miundo mbunu bora ya kujenga uchumi imara wa Tz.
Hapo awali nilizungumzia WAANDISHI wa habari wa Tanzania wamekosa uzalendo kwa nchi yao. Napenda kusimamia kwa kauli hii kwani nimeona mengi kwa hizi siku sabaa nilizokaa tanzania.
Ningependa kuwarudisheni katika Uchumi utaona Sera bora za kukuza uchumi wa nchi yoyote ile na hususan nchi masikini ni kuweka miundo mbinu Bora ya Usafiri kama barabara, Kuwa na nishati ya uhakika na kuwa na Sera bora za uwekezaji ikiwemo pamoja na Amani na utulivu wa sehemu hisika na vivutio natural kwa wawekezaji kama madini, ardhi safi n.k.
Kwa hayo hapo juu utaona Tanzania hususan Tanganyika wamebarikiwa kila kitu kasoro kulikuwa hakuna miundombinu Bora ya barabara na Nishati ya stima yyenye uhakika.
Kwa kipindi kifupi sana nimetembelea Mwanza kwa kupita barabara kupitia geita, Buseresere, Bwanga, Chato mpaka Muleba na kukomea kamachumu. Na kurudi nilipitia Biharamulo, Lusaunga, Nyakanazi, Lunzewe, ushirombo mpaka kahama, nzega na kuingia Tabora na baadae kurudi mpaka Mwanza kupitia Nzega, Tinde, shinyanga kufika Mwanza.
Jana niliingia Mtwara na leo nimetembea mpaka Kilwa kilanje lanje mpaka Ngurukuru kuona Kiwanda cha Rufiji Cement . Hakika Rais Kikwete amejitahidi sana kuweka miundo mbinu bora ya barabara za lami. Takriban lami imetawala kwingi kinachosubiriwa ni upatikanaji wa nishati ya Stima.
leo ningependa kuwashauri waTz acheni kulalamika Mtwara kuna fursa nyingi sana za uwekezaji. Kwani pamoja na kuwa na Gas na hivyo kuwa na umeme wa uhakika, lakin pia kuna mables ambazo ni malighafi safi kwa utengenezaji wa Saruji, Ardhi ni bora sana kwa kilimo cha alizeti, ufuta, korosho. Vile vile kuna beach nyingi sana na nzuri sana kuanzia msanga mkuu na maeneo yote a mikindani mpaka Lindi.
Lakin kubwa zaidi ni kuwa kuna Bandari kubwa sana. Kwani i lango kuu l kusafirishia bidhaa na la kupokelea malighafi za viwanda. Nilikuwa nikipitia sera ya Tz kuhusu Mtwara Corridor nimezipenda sana na kuona kuwa kuna mengi sana sio tu ya kujifunza lakin pia kuwekeza.
Nawashauri wana JF. Mkumbuke kuwa mtaji mkubwa wa kiuchumi ni AKILI ZENU, mengine yote ni matokeo. Acheni kulalamika umaskini wakti fursa zipo nyingi sana zipo kwenu. Kuna mahotel mazuri sana ya kulala vile vile kuna Makonde beach club, maisha Club, safari Lounge na mengine. Vile vile kuna Radio mbili maarufu Pride FM na Safari Radio. Zote hizo zinatoa taswira safi sana kwa mji wa Mtwara. Flight za uhakika nimekuja na 540. lakin hata precission nao wanakuja mara mbili kwa siku.
Namaliza kwa kumpongeza sana sana Rais Kikwete kwa kuweka na kujenga Msingi mkuu wa kuinua uchumi wenu kwa kutengeneza barabara bora na kuanza project ya kuhakikisha Umeme unakuwa wa uhakika.