Nondo za Charles Kimei bungeni kuhusu uchumi wa Tanzania

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,621
46,266
Lengo la serikali la mfumuko wa bei wa 3% kwa wakati wote halina mashiko sana kwa sababu mfumo wa bei unatakiwa uendane na uhalisia wa hali ya ajira pamoja na hali ya rasilimali fedha na ardhi.

Lengo la mfumuko wa bei Marekani ambako asilimia kubwa ya raia wana ajira linakuwa tofauti kabisa na nchi ambapo asilimia kubwa ya raia hawana ajira au wana ajiri za kujishikiza na kufanya kazi masaa machache.

Kuweka lengo dogo la mfumuko wa bei ni kuzuia pia ukuaji wa ajira kwa sababu ya inakubidi uweke sera za kiasi kidogo cha mzunguko mdogo wa fedha katika uchumi.

Kutokana na miongozo ya BoT kuhusu kiwango cha mikopo chechefu Mabenki Tanzania yanakimbizana kupata wateja wa sekta zenye risks ndogo kama consumers loans kutoka kwa waajiriwa rasmi wa serikali na mashirika makubwa ya sekta binafsi kitu ambacho mchango wake katika kukuza uchumi ni mdogo. Benki zinatakiwa kutoa mikopo hata kwa biashara zinazoibukia.

Ni kama vile Tanzani hatuna benki za kibiashara(commercial banks) na badala yake tuna Benki za hifadhi zaidi(savings banks). Hii ni kwa jinsi ambavyo benki zinajikusanyia na kurundika mitaji kwa kiwango kikubwa wakati kuna sekta kubwa ya biashara yenye uhitaji wa mikopo lakini haikopeshwi kwa kuogopa risks.

Benki za serikali au zenye mitaji kutoka serikalini zijiongeze kusaidia kuibua biashara mpya na kuziwezesha biashara mpya za kiotofauti zinazoibuka (startups) kupata mikopo,kukua na kufanya vizuri kwa sababu ndio njia mojawapo muhuimu ya kuuchangamsha na kukuza uchumi badala ya kufanya mambo yale yale kama kugawa majiko.

Inashangaza na kutafakarisha tunasifiwa sana na taasisi mbalimbali uchumi wetu kukua kwa asilimia 5 ila hatukusifiwa ulipokuwa ukikua kwa asilimia 6 hadi 7 ambapo hata hautajifikia lengo lengo la asilimia 8 serikali ililojiwekea.
 
Huyo ndo maana huo uwaziri hapewi, theory nyingi kuliko practical impacts. Aone mwenzake CRDB anavyoipeleka kasi saivi, sio kama kipindi chake
 
Yaani anaamini kweli serikali imetimiza inflation ya 3%!!? Kimei mambo yake!
Hajasema serikali imetimiza inflation ya 3%, anachosema serikali kuweka lengo dogo la inflation haina mashiko kwa uchumi wenye unemployment kubwa sana kama hapa kwetu na pia hakuna hata mchumi anayejua ni kiwango gani cha inflation ni sahihi sana.
 
Ni sawa na kumsifia Mo yuko Practical zaidi kuliko baba yake aliyemrithisa mali na miondombinu yote muhimu ya kukuza MeTL aliyoiunda na kuiweka from scratch.
Kimei hakuweka foundation yeyote CRDB kwa taarifa yako. In fact, Msekela alivyoingia alianza restructuring mpya ya administration kwenye CRDB. Kulikuwa hapafai, Kimei alijenga hadi tawi sehemu hakuna wateja huko Chato kwa ujenzi wa Hadhi ya Regional structures, huyo mtu unaona ana akili timamu kweli..?
Ndo maana alidanganywa na MZ, agombee ubunge atampa uwaziri, akaishia kupiga makofi tu mabench hadi 25 ifike atolewe. In short, mzee kimei ni inept na incompetent.
 
Kimei hakuweka foundation yeyote CRDB kwa taarifa yako. In fact, Msekela alivyoingia alianza restructuring mpya ya administration kwenye CRDB. Kulikuwa hapafai, Kimei alijenga hadi tawi sehemu hakuna wateja huko Chato kwa ujenzi wa Hadhi ya Regional structures, huyo mtu unaona ana akili timamu kweli..?
Ndo maana alidanganywa na MZ, agombee ubunge atampa uwaziri, akaishia kupiga makofi tu mabench hadi 25 ifike atolewe. In short, mzee kimei ni inept na incompetent.
Malalamiko yako yamefika, jikite kwenye hoja zake badala ya yeye binafsi na utendaji wake wa CRDB ambao haujakuridhisha.
 
Kimei hakuweka foundation yeyote CRDB kwa taarifa yako. In fact, Msekela alivyoingia alianza restructuring mpya ya administration kwenye CRDB. Kulikuwa hapafai, Kimei alijenga hadi tawi sehemu hakuna wateja huko Chato kwa ujenzi wa Hadhi ya Regional structures, huyo mtu unaona ana akili timamu kweli..?
Ndo maana alidanganywa na MZ, agombee ubunge atampa uwaziri, akaishia kupiga makofi tu mabench hadi 25 ifike atolewe. In short, mzee kimei ni inept na incompetent.
Katika hotuba ya ufunguzi wa tawi la Chato, Kimei alitamka waziwazi kwa Rais kuwa wao (CRDB) waliona kwamba Chato haikuwa na hadhi ya kuweka tawi lakini kwa utafiti na busara za Rais Magufuli amewaonesha kuwa panahitaji kujegwa tawi na imefanyika.
Hiyo statement ilimaanisha maamuzi ya ujenzi wa hiyo structure yalitoka nje ya utawala wa benki yenyewe.
 
Benki za Tanzania zimechangia uchumi wa Tanzania kutokukua tofauti na benki za kenya Kwenye kuchangia uchumi wa Kenya .

Leo sekta ya kilimo na madini ndiyo eneo lenye kuajiri watanzania wengi lakini ajabu benki bado hazitoi ushirikiano wa kutosha kwa njia ya mikopo.
Benki zinashindwa nini kuajiri wataalamu wa kilimo na madini wakatoa ushauri wa kitaalamu kwa wateja wanaotaka mikopo ili kuwe na ufanisi katika matumizi ya mikopo?
 
Benki za Tanzania zimechangia uchumi wa Tanzania kutokukua tofauti na benki za kenya Kwenye kuchangia uchumi wa Kenya .

Leo sekta ya kilimo na madini ndiyo eneo lenye kuajiri watanzania wengi lakini ajabu benki bado hazitoi ushirikiano wa kutosha kwa njia ya mikopo.
Benki zinashindwa nini kuajiri wataalamu wa kilimo na madini wakatoa ushauri wa kitaalamu kwa wateja wanaotaka mikopo ili kuwe na ufanisi katika matumizi ya mikopo?

View: https://m.youtube.com/watch?v=Kt2cRzvcbEk&embeds_referring_euri=https%3A%2F%2Fwww.jamiiforums.com%2F&source_ve_path=MjM4NTE&feature=emb_title

Watanzania aliewaroga kafariki na mafisadi kutwa yanawanyunyizia dawa, mmbaki hivyo hivyo.

Hivi mmesikiliza hiyo report.

Bank ya TIB Bashe alikuwa kutwa anapiga makelele bungeni wapeleke hela kwenye mikopo ya kilimo, mama yenu karidhia. Hela imeenda kwenye kilimo mafisadi wameenda kuikomba yote kwa miaka miwili bank wametengeza hasara ya billion 195 ya mikopo chechefu hela yote imepotea.

Hela zenyewe na wao bank walikopa kama bonds kiasi cha billion 205. Bond zime mature hawana hela ya kulipa. Hilo deni lina government guarantee, so linarudi hazina kama deni la nchi.

Sasa unazungumza mkopo gani tena wa kwenda kwenye kilimo.

Hiyo kampuni ya mbolea TFC mama yenu kaipa billioni 500 mafisadi na wabunge ndio wakopeshwaji wakubwa mpaka leo hawajalipa madeni, mtaji wote waliopewa umepotea kampuni imefilisika.

Habari zenyewe za upigaji amfuatilii halafu mkitoka hapo wale waliokuwa wanaipigania nchi dhidi ya mafisadi kama jemedari Magufuli kutwa mnawatukana.

Hutaki kujua mtaji waliopewa kampuni iliyoanzishwa na serikali ili inunue mafuta ya kuagiza mtaji wameuangamiza vipi na hayo mafuta yakiingia hakina nani wananunua kwa bei ya kutupwa hadi kampuni kufilisika.

You people live in your world, hiyo nchi miaka minne ya huyo mama imepigwa balaa na bado; mama mpaka 2030.
 
Kimei hakuweka foundation yeyote CRDB kwa taarifa yako. In fact, Msekela alivyoingia alianza restructuring mpya ya administration kwenye CRDB. Kulikuwa hapafai, Kimei alijenga hadi tawi sehemu hakuna wateja huko Chato kwa ujenzi wa Hadhi ya Regional structures, huyo mtu unaona ana akili timamu kweli..?
Ndo maana alidanganywa na MZ, agombee ubunge atampa uwaziri, akaishia kupiga makofi tu mabench hadi 25 ifike atolewe. In short, mzee kimei ni inept na incompetent.
Ni swala la muda tu hata NBC itaipiga kumbo CRDB kwa maana NMB iko level nyingine kabisa.
 
Benki za Tanzania zimechangia uchumi wa Tanzania kutokukua tofauti na benki za kenya Kwenye kuchangia uchumi wa Kenya .

Leo sekta ya kilimo na madini ndiyo eneo lenye kuajiri watanzania wengi lakini ajabu benki bado hazitoi ushirikiano wa kutosha kwa njia ya mikopo.
Benki zinashindwa nini kuajiri wataalamu wa kilimo na madini wakatoa ushauri wa kitaalamu kwa wateja wanaotaka mikopo ili kuwe na ufanisi katika matumizi ya mikopo?
Bank zimekimbilia kwenye kukopesha wafanyakazi tu ,kimsingi hizi bank zimekosa weledi ,mzee KIMEI kapingilia msumari ,hizi bank ni saving banks and not commercial banks
 
Kimei hakuweka foundation yeyote CRDB kwa taarifa yako. In fact, Msekela alivyoingia alianza restructuring mpya ya administration kwenye CRDB. Kulikuwa hapafai, Kimei alijenga hadi tawi sehemu hakuna wateja huko Chato kwa ujenzi wa Hadhi ya Regional structures, huyo mtu unaona ana akili timamu kweli..?
Ndo maana alidanganywa na MZ, agombee ubunge atampa uwaziri, akaishia kupiga makofi tu mabench hadi 25 ifike atolewe. In short, mzee kimei ni inept na incompetent.
Wewe huna hoja zaidi chuki zinakusumbua
 
Kimei hakuweka foundation yeyote CRDB kwa taarifa yako. In fact, Msekela alivyoingia alianza restructuring mpya ya administration kwenye CRDB. Kulikuwa hapafai, Kimei alijenga hadi tawi sehemu hakuna wateja huko Chato kwa ujenzi wa Hadhi ya Regional structures, huyo mtu unaona ana akili timamu kweli..?
Ndo maana alidanganywa na MZ, agombee ubunge atampa uwaziri, akaishia kupiga makofi tu mabench hadi 25 ifike atolewe. In short, mzee kimei ni inept na incompetent.
Kuhusu ujenzi CRDB Chato unamuonea, wakati wa ufunguzi alitamka wazi alipewa shinikizo na Magufuli
 
Lengo la serikali la mfumuko wa bei wa 3% kwa wakati wote halina mashiko sana kwa sababu mfumo wa bei unatakiwa uendane na uhalisia wa hali ya ajira pamoja na hali ya rasilimali fedha na ardhi.

Lengo la mfumuko wa bei Marekani ambako asilimia kubwa ya raia wana ajira linakuwa tofauti kabisa na nchi ambapo asilimia kubwa ya raia hawana ajira au wana ajiri za kujishikiza na kufanya kazi masaa machache.

Kuweka lengo dogo la mfumuko wa bei ni kuzuia pia ukuaji wa ajira kwa sababu ya inakubidi uweke sera za kiasi kidogo cha mzunguko mdogo wa fedha katika uchumi.

Kutokana na miongozo ya BoT kuhusu kiwango cha mikopo chechefu Mabenki Tanzania yanakimbizana kupata wateja wa sekta zenye risks ndogo kama consumers loans kutoka kwa waajiriwa rasmi wa serikali na mashirika makubwa ya sekta binafsi kitu ambacho mchango wake katika kukuza uchumi ni mdogo. Benki zinatakiwa kutoa mikopo hata kwa biashara zinazoibukia.

Ni kama vile Tanzani hatuna benki za kibiashara(commercial banks) na badala yake tuna Benki za hifadhi zaidi(savings banks). Hii ni kwa jinsi ambavyo benki zinajikusanyia na kurundika mitaji kwa kiwango kikubwa wakati kuna sekta kubwa ya biashara yenye uhitaji wa mikopo lakini haikopeshwi kwa kuogopa risks.

Benki za serikali au zenye mitaji kutoka serikalini zijiongeze kusaidia kuibua biashara mpya na kuziwezesha biashara mpya za kiotofauti zinazoibuka (startups) kupata mikopo,kukua na kufanya vizuri kwa sababu ndio njia mojawapo muhuimu ya kuuchangamsha na kukuza uchumi badala ya kufanya mambo yale yale kama kugawa majiko.

Inashangaza na kutafakarisha tunasifiwa sana na taasisi mbalimbali uchumi wetu kukua kwa asilimia 5 ila hatukusifiwa ulipokuwa ukikua kwa asilimia 6 hadi 7 ambapo hata hautajifikia lengo lengo la asilimia 8 serikali ililojiwekea.
Kimei yule ambaye hawezi kuongea Kiswahili vizuri?
 
Back
Top Bottom