Mkuu pole sana kwa ajali hii na mungu muweza wa yote akupe nguvu katika kipindi hiki kigumu na amjalie afya njema rafiki yako ambaye hali yake si nzuri.
Pole sana ndugu, kweli hapo ni Mungu tu amekuokoa! Lakini embu fanya check up ya uhakika licha ya kwamba unasema unamaumivu kidogo tu, wakati mwingine athari huwa ndani kwa ndani. Siombei mabaya lakini nina ndugu yangu alitoka kwenye ajali mzima kabisa lakini kumbe utumbo ulichanika kidogo na hakujua, hakwenda hospital, leo ni marehemu. Ndugu jiridhishe kwa check-up thabiti.
Pole sana MJ, God is always great mshukuru kwa kukuepusha na ajali tupo pamoja wote katika kipindi hiki na tunawaombea mpone haraka wewe na hao jamaa zako wengine mliopatwa na hiyo ajali sala ni muhimu sana
Mmmmmmh poleni sana mazee, Mungu ni mwema kweli, hamna budi kwenda kwa church mkatoe hata shukrani za pekee kwa makuu aliyowatendea, hio ilikuwa ajali mbaya sana na bila mkono wa Mungu basi kusingetoka mtu.Ushauri kwa wenzngu mnao endesha magari higway ni vema kuwa makini na mdereva wa malori na mabasi makubwa, ni vema mkae nao mbali sana na unapomuona anakuja mbele punguza mwendo kidogo maana huwa wanadharau sana magari madogo hawa majamaa, pia msisahau kufunga mikanda.
Nipo Morogoro mjini naelekea hospitali kufanya uchunguzi wa thabiti, gari imekwisha letwa hapa Morogoro kwa jaili ya utaratibu mwingine! nawashukuru wote mnaozidi kutuombea; nimepokea taarifa za aliyekimbizwa hospitali kuwa matumaini ya kuishi i makubwa anaendelea ku recover vizuri! tuzidi kumuobea huyo mpiganaji.
pole sana
ni muda mzuri wa kumrudishi amungu utukufu
tubu dhambi zako na utende kwa mapenz yake kwa sababbu muujiza aloutenda kwako ni mkubwa
mungu anakupenda kaka
badili njia safisha mapito !!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.