Namshauri Rais afute vitambulisho vya wamachinga

Namshauri Rais afute vitambulisho vya wamachinga

Ifike wakati watanzania tuache ujinga kama watu hawataki kutoa elfu ishirini kwa ajili ya kitambulisho kitakacho wa exempt kulipa kodi ambayo ingekuwa kubwa zaidi basi hao watu wasidai maji, umeme, barabara wala hudumu yoyote toka serikalini , haiwezekani watu wachache watozwe kodi kwa ajili ya 60% ya watanzania wengine. Hivi ikitokea tunyimwe msaada tutaishiji kama nchi? Mbona watu mnaendekeza uvivu, ujinga na ukosefu wa ubunifu wa kutafuta pesa. Watu wanatoa sababu kibao lakini wanasahau uvivu na ujinga wa watu wasiolipa kodi. Hii nchi ingekuwa chini ya wakoloni au hao wazungu wanaotupa misaada wote tungelipa kodi hata kwa fimbo.
Duh kiongozi naona umesema kwa uchungu sana. Wazungu wanatozana kodi kubwa kweli ila huku kwetu watu hawataki kulipa kodi tumebaki wafanyakazi ndio tunalipishwa mzigo wa kodi wakati wengine wanatesa tu. Kwa wafanyakazi hakuna pa kukwepea. Bora hata ije kodi ya kichwa ili kila kichwa kilipe kodi tujue moja.
 
Well said,mama mkaanga mihogo ambae mtaji wake ni elfu ishirini unamwambia anunue kitambulisho?Vitambulisho ni unyonyaji kabisa.
Hao wote wamekuwa wakilipa ushuru wa 1000 kwa halmshauri kwa siku sasa kama watalipa 20000 kwa mwaka mzima uone kama ni nafuu?
 
Hao wote wamekuwa wakilipa ushuru wa 1000 kwa halmshauri kwa siku sasa kama watalipa 20000 kwa mwaka mzima uone kama ni nafuu?
Wale wanaochoma mahindi au kukaanga mihogo kumbe huwa wanalipa ushuru ?Wa elfu moja?kumbuka kutoa elfu ishirini papo kwa hapo ni ngumu.
 
Inaonekana una muda. Swali gani hili.
wewe unasema lengo la vitambulisho ni kwa ajili ya kutoa kodi...lakini kitambulisho kimetoka ikulu ndo maana nikauliza..ikulu inakusanya kodi ?
 
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app
ITAPENDEZA ZAIDI KAMA HIZI NGUVU WATAZITUMIA KWENYE ZOEZI LA UTOAJI WA VITAMBULISHO VYA URAIA AMBAVYO WATANZANIA WOTE WAMESHAVILIPIA KWA KODI ZAO.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ushasema mfanyabiashara!! Mbona unaujichanganya hata hujui category za biashara. Au kwa kuwa kiongozi wa malaika ndio katoa hivyo vitambulisho? Acheni upumbavu kushabikia hata ujinga, kisa tu mfalme ndio kafanya. Poleni sana, kama mmeshindwa kuendesha nchi jiondoeni tu, sio mpaka mje muondolewe.
Mlidhani kununua upinzani ndio kukusanya kodi, mlidhani kuzuia mikutano ya siasa ndio kuboresha maisha ya mtanzania, mlidhani kuchota hela za hazina bila kibali cha bunge, ndio kuongeza ajira kwa watanzania, au mlidhani kuzuia bunge kurushwa live ndio kuongeza viwanda? Mkaenda mbali mkaanza kugombana na matajiri, wafanyabiashara wakubwa, wawekezaji wa kila sekta, wawe wazawa au wageni ndio mkajua itaweza kulipa deni la taifa?
Poleni sana, naona mwisho umefika. Sasa mmerudi kuwatisha wananchi, tunajua mpango ulioko nyuma. Mkifanikiwa hili basi mtawale milele!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Utakuwa mzururaji
 
rais anawapenda mno wamachinga na wafanyabiashara wadogo ndio maana amewaletea hivyo vitambulisho bure ili wasisumbuliwe na mgambo

Acha kudanganya watu wewe pamoja na kujidanganya mwenyewe....

Hivyo hata siyo vitambulisho vya kuwatambua wafanyabiashara, hizo ni kadi za CCM toka kwa M/kiti wa CCM Taifa...!!
 
Ifike wakati watanzania tuache ujinga kama watu hawataki kutoa elfu ishirini kwa ajili ya kitambulisho kitakacho wa exempt kulipa kodi ambayo ingekuwa kubwa zaidi basi hao watu wasidai maji, umeme, barabara wala hudumu yoyote toka serikalini , haiwezekani watu wachache watozwe kodi kwa ajili ya 60% ya watanzania wengine. Hivi ikitokea tunyimwe msaada tutaishiji kama nchi? Mbona watu mnaendekeza uvivu, ujinga na ukosefu wa ubunifu wa kutafuta pesa. Watu wanatoa sababu kibao lakini wanasahau uvivu na ujinga wa watu wasiolipa kodi. Hii nchi ingekuwa chini ya wakoloni au hao wazungu wanaotupa misaada wote tungelipa kodi hata kwa fimbo.
Na wewe unatakiwa uongee kwa ustarabu ungekuwa unajua principles za taxation?? Kwanza kwanini waweke flat rate. Halifu sio lazima kila mtu alipe Jodi directly kodi zingine zinatakiwa ziwe za ku encourage busineses and Investments. Mi naona hapa uchaguzi umekaribia, zinatafutwa Fedha za chama fulani hapa.
 
Na wewe unatakiwa uongee kwa ustarabu ungekuwa unajua principles za taxation?? Kwanza kwanini waweke flat rate. Halifu sio lazima kila mtu alipe Jodi directly kodi zingine zinatakiwa ziwe za ku encourage busineses and Investments. Mi naona hapa uchaguzi umekaribia, zinatafutwa Fedha za chama fulani hapa.
Wamezikosa, ila kura tutalinda hata mishale!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ila wanapaswa kina flani WAANDAMANE KUUNGA MKONO VITAMBULISHO PASI KUJALI UHALISIA ULIOANDIKWA KWENYE BANGO HILI
 
KIJIJINI KWETU TUMEAMBIWA YEYOTE ANAEENDA KUUZA CHOCHOTE SOKONI IWE MCHICHA,EMBE,CHOCHOTE,alipie 20,000 apewe kitambulisho.,la sivyo muda ukiisha hakuna atakaeruhusiwa kuuza chochote sokoni bila kitambulisho!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ifike wakati watanzania tuache ujinga kama watu hawataki kutoa elfu ishirini kwa ajili ya kitambulisho kitakacho wa exempt kulipa kodi ambayo ingekuwa kubwa zaidi basi hao watu wasidai maji, umeme, barabara wala hudumu yoyote toka serikalini , haiwezekani watu wachache watozwe kodi kwa ajili ya 60% ya watanzania wengine. Hivi ikitokea tunyimwe msaada tutaishiji kama nchi? Mbona watu mnaendekeza uvivu, ujinga na ukosefu wa ubunifu wa kutafuta pesa. Watu wanatoa sababu kibao lakini wanasahau uvivu na ujinga wa watu wasiolipa kodi. Hii nchi ingekuwa chini ya wakoloni au hao wazungu wanaotupa misaada wote tungelipa kodi hata kwa fimbo.
Si ndo tuambiwe kwamba hiyo 20,000 tutakayolipia kila mwaka itakuwa KODI sio gharama yakutengeneza kitambulisho

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huenda aliwaza vizuri lakini utekelezaji wake imekuwa ni karaha kwa wafanya biashara wadogo. Watendaji wa serikali wanatumia nguvu kubwa sana kukazimisha watu kununua vitambulisho hivyo. Sehemu nyingine watumishi wametishiwa hadi kufukuzwa kazi wasipofanikiwa kuuza vitambulisho hivyo.

Hapa ilipaswa kujuliuliza kwanini vitambulisho hivyo havinunuliwi? Jibu ni fupi tu wafanyabiashara wengi wana mitaji midogo sana hivyo kwa lugha nyingine wao ni masikini kabisa. Sasa kwenda kuchukua 20,000/= kwa masikini kwa kisingizio cha kitambulisho hiyo ni sawa uuaji. Ukiangalia baadhi ya wafanyabiashara wanaolazimishwa kununua vitambulisho hivyo mitaji yao ni chini ya 20,000/= halafu analazimishwa kununua kitambulisho cha 20,000/= ambayo hana. Hivi shoe shiner na muuza karanga kwa mfano mitaji yao ni shilingi ngapi hadi walazimishwe kununua kitambulisho?

Kwakuwa hili lilikuwa ni wazo binafsi la rais kama alivyoeleza yeye mwenyewe na kwakuwa ni yeye ndiye aliyevitengeneza na kwakuwa ni yeye ndiye aliyepanga bei namshauri avifute kabisa vitambulisho hivyo kwani vina mshushia hadhi sana miongoni mwa wafanyabiashara wadogo masikini na wananchi kwa ujumla. Vinginevyo ili kuwasaidia ni bora avitoe bure. Ikumbukwe madhara yoyoyte watakayopata wamachinga, watumishi na wananchi kwa ujumla lawama zote zitaelekezwa kwake rais kwakuwa yeye ndiye mwenye vitambulisho hivyo.

Ni vizuri rais ajue kuwa watendaji wake wanafanya kazi kwa nidhamu ya woga sana na kujipendekeza ili kumfurahisha yeye hivyo wanaoumia ni wananchi kutokana na hatua wanazochukua dhidi ya wananchi. Ni watendaji wasioweza kutoa ushauri pale wanapoona mambo magumu zaidi ya kutumia nguvu ili kila mmoja aonekane anaweza.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mleta uzi labda tu nikwambie kitu usichojua ni kwamba serikali inauhitaji mkubwa sana wa hela pili wanaandaa data base ya walipa kodi. Naomba niishie hapa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi jumla ya vitambulisho vyote vilivyotolewa na rais kwenda mikoa yote Tanzania ni vingapi? Kwa idadi yoyote lengo kuu la hivyo vitambulisho lilikuwa ni kukusanya pesa nyingi kwa sababu maalumu na kuwa kibano kwa wenye navyo kwa siku za usoni. Hayo mengine ni hadaa tu.
 
Back
Top Bottom