Nampenda sana lakini ana mke

Nampenda sana lakini ana mke

Si umesema hutaki kuolewa au, unataka ushauri ganii
Haya kaolewe mke wa pili basi, na usubiri ataletwa na watatu
 
We ni mchepuko vumbi kwa ufupi kama hujui maana yake njoo inbox nikuogeshe na sabuni.
 
Ushauri wa nini wakati hutaki kuolewa na mtu mwenye mke hapo sep
 
Tafuta mahali pengine ujiweke taratibu taratibu umuache huyo
 
Pole kwa mazito yaliyo kukuta, hizo ni mmoja ya changamoto katika suala zima la mapenzi.
Kwa mtazamo na ushauri wangu kwa ujumla,

Haijalishi ni kiasi gani umempenda moyoni, lakini ni vyema ukasahau yaliyo kukuta na kuendelea na maisha yako,
Na isitoshe kwa umri uliyokuwa nayo ( 21 ) bado ni mdogo, hivyo unahitaji ufanye mambo yako ya maana na ni vyema ukaolewa ukiwa na miaka ( 25 ) - ( 35 ) hicho ni kipindi ambacho mwanamke amekomaa kiakili na kuweza kufanya maamuzi sahihi katika mambo yake, na hata kuwa imara kwenye ndoa na masuala yote ya uzazi.

Hii inaonesha mwanaume uliye nae kwa sasa hakupendi, kwa sababu yeye tayari ana mke wake na watoto, kutokana na ile tamaa ya ngono, ameona akuchukue wewe ikiwa bado mdogo, kifupi amekufanya hawara wake, sidhani kama anayo mapenzi ya dhati kwako, zaidi ya kutaka kukuchezea tu!!!

Cha kufanya, kaa umueleze ukweli kuwa haupo tayari kuolewa nae, wala kuendelea nae kimapenzi, ila usimchukie ongea nae, Cheka nae, kama kawaida zungumzeni vizuri muwe kama marafiki na si wapenzi/ wapendanao.
Na jaribu kuwa mwangalifu baada ya kuchukua uamuzi wa kumuacha maana anaweza akakulaghai tena kwa maneno mazuri, na kujifanya anahitaji huruma yako kusudi mrudiane, angalia hili, sisima imara, jipe moyo yote yanawezekana kilichobaki ni kuchukua maamuzi sahihi,
Najua umesema bado unampenda ila hutaki kuolewa nae,
Hii kauli inaonesha ni jinsi gani bado upo kwenye kundi la vijana, nikiwa na maana ya kwamba, ni akili ya ujana bado ila kadri unavyokuwa na kuoata akili ndivyo utakavyo elewa kuwa ulikuwa unakosea kuongea hiyo kauli,
 
  • Thanks
Reactions: irk
Watoto wa tanga hawaliagi ovyo kwenye mitandao we itakua umetokea marangu umekaa kidogo tanga wajifanya mtu wa tanga,usiabishe huu mkoa mama.
 
Habari zenu, naitwa Issabella natokea Tanga nina umri wa miaka 21, Nina boyfriend ambae nipo naye takribani miaka miwili sasa, katika mahusiano yetu hajawahi kuniambia ana mke wala watoto na hajawahi kunionyesha dalili yeyote ile kama ana mke.

Lakini siku kadhaa niliambiwa na rafiki yake kuwa mtu ambaye nipo naye ni mume wa mtu, na nikweli nilithibitisha nikaona kweli ana mke, nimemuuliza amekubali na ameniambia hajaniambia kwasababu aliogopa nitamuacha lakini bado ananipenda na atanioa......ushauri kwenu nifanyaje?

Nimuache au niendelee naye? Kiukweli mimi pia bado nampenda sana lakini sipo tayari niolewe na mtu ambaye ni mume wa mtu. Naombeni ushauri wenu plz


pole sana kwa kutumika miaka miwili kama kibadilishia ladha...ni kwamba unampa uroda mme wa mtu..na jua yeye nd0 anakufaidi kwani anakula pawili,,,leo wli kesho pilau basi tuu apate raha
 
Tafuta wako..huyo mpk kakuficha maana yk we ni wa kutumia tu aka mchepuko..chondechonde usije ukarudi kuomba ushauri hapa ooh mume wq mtu kanitenda..ooh nna mimba ya mume wa mtu nifanyeje
 
Issabella, umri wako bado ni mdogo sana kuanza kujichanganya. Soma mfano huu halafu fanya maamuzi.

Upo mkoani Dodoma unapanda gari kwa lengo la kwenda Dar. Kondakta wa basi anakuambia, dada nijuavyo mimi ni kwamba basi letu linaenda Kigoma, siyo Dar. Unamwuliza dereva, ati gari linaenda Kigoma na siyo Dar? Dereva anakujibu waziwazi kuwa ndiyo linaenda Kigoma lakini baki tuu dada usishuke. Nitakupeleka Dar mimi mwenyewe kwa gari hili hili. Kondakta anakukonyeza kuashiria kuwa usimwamini dereva wake kwani utaratibu wa gari ni Dodoma-Kigoma.

Utafanyaje hapo Dada yangu? Utahitaji ushauri? Kwenye masikio na asikie sasa.
 
Back
Top Bottom