Sijui uhalisia wa hii post lakini kama kuna kosa kubwa utafanya katika maisha yako ni hilo unaloliombea ushauri
-anaweza kuona dalili na akatia timu lakini kubali kifuatacho ITV
-anaweza kuwa mweledi na mwenye msimamo akakufukuza kazi
-anaweza kuwa ni fisi maji ukaishia kuumia
Epuka mahusiano na mtu anayekulipa mshahara
Yaani mshana jr; Umempa ushauri murua kabisa. Ulienda kutafuta kazi, ukakuta wenzio waliokutangulia. Iweje weye ujione ndo champion kidume??
Tulizana na uutulize huo mzuka. Huenda hii ndo njia ya kukumwagia kibarua. Penzi halihitaji kusukumwa huwa linajiotea lenyewe, Hakuna penzi la kichina duniani.
Boss kutaniana na wafanyakazi mbona kawaida tu. Usimchukulie rahisi kihivyo. Mpe zawadi yake siku ya BD ondoka zako jifanye hujisikii vizuri na keshoye chelewa kazi uone reaction yake ndipo uamue