Asante mkuu Elli kwa kuliona hilo.
Hapo kwenye red kibanda amewekwa mkononi na RA kwa hiyo sio mtu wa wa kumuamini hata kidogoHivi nyie hamjui kuwa kuna makundi mawili ya waandshi wa habari? Liko kundi linalopinga ufisadi; halafu lile linalowaunga mkono watuhumiwa wa ufisadi. Makundi yote mawili yanapata mshiko. Sasa akili kwenu wanaJamii . Ninachoweza kuwaambieni ni kuwa nchi yetu kwa sasa inapotoshwa na vyombo vya habari ingawa kwa hakika vyombo hivi vinafanya kazi kubwa 'positively' ndani ya jamii. Lakini wapo waandishi wa habari ambao pamoja na kuchukia ufisadi wamewekwa mkononi na mafisadi kwa sababu ya fedha. Aidha, wale nao wanaochukia ufisadi wanapewa fedha kupinga ufisadi. Kazi kubwa kweli kweli. Wako waandishi wa habari waliojengewa majumba na kununuliwa magari, katika pande zote mbili.
Tanzania Daima nilishalistukia siku nyingi halina tofauti na Mtanzania,Rai .......
Asante Mpwa, niliona hii habari ni ya kizushi flani hivi, yaani ni sawa na ugomvi wa wanawake majumbani ( sio kwamba nina nia mbaya na wanawake) halafu mmoja akimbilie polisi kuchukua RB kuwa mwenzie kamtishia kumuua, si RB zipo tu, si polisi wapo wapo tu, hata usiku wa manane unaweza kwenda na ukawakuta japo watakua wamesinzia kidogo
RA mwacheni kwanza. Tutamnyongea katika uwanja wetu wa Tahrir -- yaani Jangwani -- siku itakapowadia. Lakini hata hivyo nasikia serikali inataka kuanza kugawa viwanja pale jangwani kwa hofu ya kutokea mikusanyiko ya kuiondoa siku itakapofika!
Hii story haina mantiki hasa kweli kama mwandishi angekuwa mtu makini, maswali yafuatayo au mambo yafuatayo ni muhmi kujiuliza na kuyafahamu; Iwapo watu wana uwezo wa kufoji sahihi hata za viongozi wakubwa, mihuri na nyaraka mbalimbali hadi kukwapua kwenye mabenki na sehemu nyingine nyeti ( kama ilivyowahi kuripotiwa sehemu mbalimbali nchini na nje ya nchi) bila kutumia nguvu ya aina yoyote, iweje huyu atumie nguvu kama sio Uongo???
Pili, kulikuwa na umuhimu gani hasa wa kumfuata TABU badala ya kutumia mbinu kibao ambazo zipo? yaani huyo anaehitaji hiyo sahihi alikua mjinga kiasi gani hadi amfuate Katibu wa RA huku akijua fika uhusiano wa karibu kati ya Tabu na RA ( kama ilivyowahi kuripotiwa kwenye vyombo vya habari nchini).
Tatu, je ni vigumu sana kuipata sahihi ya RA hadi aende ofisini kwake? yaani hakuna nyaraka nyingine zozote ambazo RA ameweka sahhihi ni hadi ofisini kwake?
Nne, kwa nini amsubiri wakati anatoka ofisini huku akijua fika kuwa hawezi kuwa anatembea na document zenye sahihi, hapa huyu mtuhumiwa ambaye mimi naamini hayupo, ni mjinga kiasi gani amsubiri Tabu atoke ofisini ndio amfuate??
Tano, angewezaje (Mtuhumiwa hewa) kutoa pesa kidogo hivyo (5M) hali akijua nafasi ya Tabu na kipato chake, kweli Tabu angekuwa radhi kutoa sahihi ya Bosi wake kwa Million tano tu??? labda kama hawafahamu vizuri.
Mwisho, ni vyema unapotunga stori, jiulize kwanza baadhi ya maswali mwenyewe, yaani, jiweke kwenye position ya msomaji na sio kuvutiwa na hisia zako tu. Naombeni ushauri kwa haya machache. Asante
hivi mtu akisema uongo hauwezi kumchukulia RB polisi? Au kusema uongo sio kosa la jinai, mbona mtu akisema uongo mahakamani anapewa adhabu?
Mkuu Elli; Thanks, umemaliza kila kitu. Hiyo haina vigezo vya kuita habari achilia mbali kuiweka mbele.
Gazeti nchi hii la kila siku ni Mwananchi tu, haya yetu ya kibongo hovyo tu, yako kwenye personalities badala ya issues.
Nilishaandika huko nyuma na narudia Kibanda ni aibu nyingine kwenye tasnia ya habari nchini kwa sasa na hata anapokanusha hapa ni kujipa ujasiri uso soni.
Nasoma T/Daima kwa article za watu wawili tu, nao Asbert Ngurumo na Mwanakijiji, zaidi ya hapo ni utumbo tu.
Kwani hilo gazeti linamilikiwa na nani? je mmiliki anahusikaje na habari za kumsafisha RA? Hivi mnataka watu waamini kuwa mmiliki hahusiki na kama hahusiki na hizo habari unazodai kuwa za kumsafisha RA amechukua hatua gani? Tusije tukawa tunajidanganya kumbe hata tunaodhani hawapo kumbe wamo mmesahau ya mchungaji Mtikila kupewa pesa na RA? Hivi kweli kuna mtu aliweza kulifikia suala kama lile lingewezekana? Mimi nisingefikiria kuwa linawezekana sijui wewe mwenzangu........................