Gama
JF-Expert Member
- Jan 9, 2010
- 13,266
- 4,716
Nimekuwa nikisoma taarifa mbalimbali juu ya maajabu yanayoonekana kwenye kaburi la Chifu Kiyeyeu pale Iringa. Nimepokea kwa masikitiko habari za kuwa kaburi hilo limehamishwa ili kupisha upanuzi wa barabara na kupitisha waya wa umeme. Nimesikitishwa kuona kiuwa nchi hii ina taasis nyingi zinazojihusisha na mambo ya kale lakini hakuna taasis hata moja iliyokemea kitendo cha kulihamisha kaburi hili. Binafsu kama mwana historia nilidhani taasis mbalio mbali kama makumbusho ya taifa, wizara ya utamaduni, ofisi ya utamaduni ya wilaya, ofisi ya mkuu wa mkoa na NGOs wangetia juhudi kuona kuwa kaburi hili linaorodheshwa katika moja ya maaajabu ya dunia na hata kuwa kivutio cha utalii. Kukubali kuliondoa kaburi hili kwa ajili ya mambo yaliyokuwa na mbadala ni ukosefu wa hekina na busara na kutokuwajibika kwa taasisi zetu ambazo kutwa kucha zinaogelea katika kodi za wananchi. Natoa wito kwa serikali kuacha vitendo vya uharibifu wa mambo muhimu yanapaswa kuwepo ili hata vizazi vijavyo viweze kuona.