Nakwenda Dodoma kuhakikisha kuwa Mama Samia anaukwaa Uenyekiti wa CCM bila tatizo lolote. Mama anaweza

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Nimekatisha safari yangu ya kwenda nyumbani Songea, Ruvuma. Nimegeuzia Masasi, Mtwara. Nimeamua kuingia mstari wa mbele bila kelele kuhakikisha kuwa Mama Samia anaukwaa Uenyekiti wa CCM bila vikwazo vyovyote. Nikiwa Masasi, nilipokea taarifa za kiintelijensia kuwa kuna baadhi ya makada wabobezi na wa kawaida wa CCM wanajipanga wakiwa Dodoma na kwingineko kuhakikisha kuwa Mama anakwama au anayumba.

Kwasasa nakaribia Morogoro Mjini. Nakwenda Dodoma kwa 'kazi maalum' ya kichama. Nakwenda kumsafishia njia Mama Samia ili mwishoni mwa mwezi huu aukwae Uenyekiti wa CCM bila mawaa wala balaa. Mama Samia anaweza. Mama Samia anafaa. Ni msikivu; mwenye huruma na haki. Mama Samia ni mwenye kusikia na kusikilizwa; kutafiti kabla ya kusema na kufikiri bila kuhema. Mama Samia anaipenda demokrasia.

Akiwa Mwenyekiti wa CCM atafungua uwanja wa demokrasia ya vyama ili wanasiasa wa zamani na wa sasa tuingie kucheza bila kuumiza. Wanasiasa tuingie uwanjani kuoneshana ukomavu wa hoja za haja na mbinu katika medali za kisiasa za kisasa. Atafungua mikutano ya hadhara yenye hadhira bila hasira na maandamano ya kutokukubaliana bila hiyana. Mama anaweza kufungua ukurasa mpya wa kisiasa nchini.

Kesho asubuhi, naanzia ndani Bungeni kumsikiliza mubashara akilihutubia Bunge na Taifa kwa ujumla. Watanzania wanasubiri maneno yake yatakayofuatiwa na matendo yake. Baada ya hapo, Uenyekiti wa CCM unafuata. Safu mpya itasukwa. Chama kitasonga mbele bila kelele. Mapambano yataendelea.

Wabunge waachwe wademke hadi wachemke!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kuelekea Dodoma)
 
Kuna haja ya kutengenisha hz kofia lazima chama kiwe na mwenyekiti ambae atadeal na kazi za Chama na kuwe na Kiongozi ambae atadeal na Nchi

Mama hawezi kudeal na Chama kwa tunapoelekea chama kinataka mwenyekiti ambae ni tough kudeal na hawa wanachama (wabunge) ambao wameonyesha kabisa hawana nidhamu mama yupo too soft to handle
 
Kuna haja ya kutengenisha hz kofia lazima chama kiwe na mwenyekiti ambae atadeal na kazi za Chama na kuwe na Kiongozi ambae atadeal na Nchi
Kuna mtu alijitangaza atakuwa Waziri mkuu kama mgombea fulani angeshinda lakini haikuwa hivyo. Kuna hatari kubwa ingetokea kama angeshinda
 
Kundi la mwenda zake ndo wanaosumbua , alafu mbaya wengi ni wa juzi, kisa walikua karibu na mwenda zake Basi wanaona wanakijua chama vizuri, ila all in all hawawezi chomoka, Kuna mzee wa msoga watapigwa chenga la mwili na roho ,
 
Napenda sana litokee kundi moja ndani ya CCM litake mabadiliko ya kutenganisha kofia ya Rais na Mwenyekiti wa Chama. Yaani mwenyekiti aongoze chama na kuisimamia serikali kwa kupush yaliyomo kwenye ilani yatekelezwe. Na Rais wa nchi awajibike kutimiza ahadi za chama na kuwajibika kwa chama na wapiga kura ili kutanua wigo wa Demokrasia ya uwajibikaji.
 
Nadhani huu uwe muda wa kutenganisha kofia mbili! Urais na Uenyekiti wa Chama! Rais apate muda wa kutekeleza majukumu ya kuwatumikia wananchi.
 
Una siku ngapi hujaposti humu? Naona Ni kihetehere tu kutaka kuposti leo... Wewe Ni Nani Hadi usikilizwe na timu CCM ? Wewe Kama Ni kanyumba ndogo yako ndio unafukuzia haya ruksa...
 
Kuna haja ya kutengenisha hz kofia lazima chama kiwe na mwenyekiti ambae atadeal na kazi za Chama na kuwe na Kiongozi ambae atadeal na Nchi

Mama hawezi kudeal na Chama kwa tunapoelekea chama kinataka mwenyekiti ambae ni tough kudeal na hawa wanachama (wabunge) ambao wameonyesha kabisa hawana nidhamu mama yupo too soft to handle
Ni hatari sana pindi wasipoelewana!
 
Nimekatisha safari yangu ya kwenda nyumbani Songea, Ruvuma. Nimegeuzia Masasi, Mtwara. Nimeamua kuingia mstari wa mbele bila kelele kuhakikisha kuwa Mama Samia anaukwaa Uenyekiti wa CCM bila vikwazo vyovyote. Nikiwa Masasi, nilipokea taarifa za kiintelijensia kuwa kuna baadhi ya makada wabobezi na wa kawaida wa CCM wanajipanga wakiwa Dodoma na kwingineko kuhakikisha kuwa Mama anakwama au anayumba.

Kwasasa nakaribia Morogoro Mjini. Nakwenda Dodoma kwa 'kazi maalum' ya kichama. Nakwenda kumsafishia njia Mama Samia ili mwishoni mwa mwezi huu aukwae Uenyekiti wa CCM bila mawaa wala balaa. Mama Samia anaweza. Mama Samia anafaa. Ni msikivu; mwenye huruma na haki. Mama Samia ni mwenye kusikia na kusikilizwa; kutafiti kabla ya kusema na kufikiri bila kuhema. Mama Samia anaipenda demokrasia.

Akiwa Mwenyekiti wa CCM atafungua uwanja wa demokrasia ya vyama ili wanasiasa wa zamani na wa sasa tuingie kucheza bila kuumiza. Wanasiasa tuingie uwanjani kuoneshana ukomavu wa hoja za haja na mbinu katika medali za kisiasa za kisasa. Atafungua mikutano ya hadhara yenye hadhira bila hasira na maandamano ya kutokukubaliana bila hiyana. Mama anaweza kufungua ukurasa mpya wa kisiasa nchini.

Kesho asubuhi, naanzia ndani Bungeni kumsikiliza mubashara akilihutubia Bunge na Taifa kwa ujumla. Watanzania wanasubiri maneno yake yatakayofuatiwa na matendo yake. Baada ya hapo, Uenyekiti wa CCM unafuata. Safu mpya itasukwa. Chama kitasonga mbele bila kelele. Mapambano yataendelea.

Wabunge waachwe wademke hadi wachemke!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (safarini kuelekea Dodoma)

Mnapokosea sana Ni kusahau kama wazee wamekwepa mishale Mingi sana, mbaya zaidi mnaona kama mnaweza kuwafundisha Siasa. Siasa zina wenyewe na wenyewe ndo hao vingunge wakina Mangula. Wewe endelea tu na Safari zako.

SSH Ni Mwenyekiti wa hicho chama. Wenzenu wamewazidi Hapo tu kusimama katika utaratibu waliojiwekea.

Mnacheza sana Ngoma za CCM badala ya kusimamia ajenda zenu. Mnaona Aibu gani kuandika sera zenu. Muda mwingine mnaandika kuhusu watu na kusaka cheap popularity.
 
Back
Top Bottom