Kuna demu ananishobokea sana, ila kila nikimgusia maswala ya mapenzi anabadilika kama chui..
Yani tukikaa week hatujaonana, basi siku akiniona anachangamka anani-hug na mabusu mengi mengi ... Yani hapa ndio nina data kabisa.. Tatizo ni moja tuu "hataki maswala ya mapenzi"
Kila siku kuniletea vizawadi na kunishukuru et hajawai kutana na rafiki wa kweli kama mimi.
Ni mwaka wa pili sasa naingiza gia lakini haingii kwenye line, mbaya zaidi kuna siku kanitongozeshea rafiki yake makusudi kabisa.. Anasema hapendi kuniona mpweke.... ila mimi simtaki rafiki yake namtaka yeye
Kiukweli naona ni bora kukatisha urafiki kabisa ili nisimuone ....