Nakumbuka Kenya

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Nimefanikiwa tena kufika laiser hill academy shule ambayo niliwahi kusoma shule ya msingi kwa kipindi sha miaka 3 kuanzia mwaka 1996 , nilipofika hapa nimekumbuka mengi na kuwaza mengi sana kila ninapoangalia mambo na vijimambo vingine .

Kwanza nilisikia mwalimu mmoja niliyekuwa namchokoza sana bwana omondi ameshafariki dunia , na wengine wengi ambao wameshaacha kazi , wengine wamekimbilia katika fani zingine na kuacha kazi ya kujitolea ya ualimu .

Nikakumbuka mara ya kwanza nilipokanyaga hapa laiser hill academy , mimi na wadogo zangu 2 wote tulinunuliwa vitu kutoka Tanzania nakumbuka ilikuwa mkoani arusha , vitu ambayo tumezoea kuvitumia toka enzi hizo .

Baba yetu alipotuacha hapa na kutukabidhi kwa mkuu wa bweni letu mambo yalibadilika , yule mkuu kwa jina aliitwa Mr Otwanee , alitoa vitu vyote vilivyoandikwa made in Tanzania na kutupa vya kikenya .

Kisha tulienda kukaribishwa mlo wa jioni , humo ndani tulikutana na vitu kama sukuma wiki , na vyakula vingine ambavyo vilikuwa ni vigeni sana kwetu na hatukuwahi kufikiria kwamba tunaweza kubadilikiwa .

Siku moja tulitoka kwenda katika mbuza za wanyama karibu na Nairobi , kabla ya kwenda kule unatakiwa kununua vitu kama vyakula , vinywaji na kadhalika , tulipotoka shule tulipelekwa super market Fulani inayoitwa Nakumat .

Ukifika Nakumat kila unachoangalia ni made in Kenya kuanzia sausage , biskuti , juice na kadhalika , ni tofauti sana na mtoto anayesoma st maries akitoka weekend anapelekwa GAME mlimani city anaenda kununua apple za afrika kusini , mashati ya kikenya , mafuta ya kongo .

Tuliporudi nyumbani tulianzisha ugomvi na mama , kwa sababu tulishazoea vitu na mali za Kenya , ukiletewa nguo unaangalia imetoka wapi , viatu kama ni bora ya Kenya , colgate kama ni kutokea Kenya NIDO , OMO , Sausage na vitu vingine vidogo vidogo .

Ndio maana ukitembelea tovuti za wakenya kama www.mambogani.com unaona kila memba ana lebo ( AM PROUD TO BE KENYAN ) kweli lazima mtu awe proud si kila kitu anatumia chake ? wasi wasi na mashaka ya nini ?

Uwe na siku njema
 
kuna uwezekano kuwa wewe ndiye mwenye hii profile ya "shy"?....mmmmmh!...ila ahsante!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…