Castr
JF-Expert Member
- Apr 5, 2014
- 31,981
- 64,006
Mwandishi, umeandika uzi mrefu wa kuvuta hisia kweli kweli, nakupongeza kwa hilo. Ila tuijadili kesi hii kwa kifupi tuweke hisia pembeni;
1) Hata kama mtu ametokea kijijini, huwezi kudanganywa kirahisi kiasi hicho na ukakubali kosa. Labda awe sio mzima kiakili.
2) Hakimu ana kosa gani hapo??? Mtu kakiri kwamba ametenda kosa, kuna kipi cha ziada cha yeye hakimu kung'ang'ania ushahidi wa ziada??? Sheria inasema mtuhumiwa akikiri kosa mara tatu basi hakimu anatakiwa kutoa hukumu moja kwa moja.
3) Kuna ushahidi gani ukiachia maneno, kuthibitisha kwamba hilo kosa hajatenda mtuhumiwa???
4) Hukumu ya kulawiti mtoto wa chini ya miaka 8 ni maisha na sio miaka 30.
2) Hakimu na baraza la wazee katika kushauriana ilitakiwa washauriane huku mezani kuna vielelezo. Mleta uzi anasema vielelezo havikuwepo, kama ni kweli havikuwepo hii inamaanisha hakimu ametoa hukumu ila hajacover angle ya 'beyond reasonable doubts'