Kiraka Kikuu
JF-Expert Member
- Oct 3, 2011
- 5,904
- 1,976
Nilifika harusini, na kukuta milango miwili, mmoja umeandikwa ndugu wa Bwana Harusi, mwingine wa bibi harusi; nikaingia wa Bwana Harusi. Mbele nikakuta milango mingine miwili, mmoja umeandikwa wanaume, mwingine wanawake; nikaingia wa wanaume. Mbele nikakuta milango mingine miwili, mmoja umeandikwa Wenye Zawadi, mwingine Wasio na zawadi, nikaingia mlango wa Wasio na zawadi, GHAFLA NIKAJIKUTA NIPO NJE YA JENGO