Najuta Kusoma hadi chuo Kikuu

Najuta Kusoma hadi chuo Kikuu

Habari zenu ndugu,

Ni kipindi kirefu nimekua nikiangaika kutafuta ajira pasipo mafanikio.Nimefanya interview zakutosha lakini nimekua nikiambulia ahadi tu za kupigiwa simu toka kwa ma hr ambazo hazina ukweli wowote.Kitu kikubwa kinachotukosesha ajira sisi vijana ni kipengere cha experience ambapo waajiri wengi wanahitaji uzoefu usiopungua miaka mitatu na kuendelea.Swali ni je nawezaje kupata huo uzoefu wakati ofisi nyingi hazitaki kuniajiri na hata ninapoomba kujitolea naambiwa nafasi hakuna ?kwa kifupi ndugu zangu nimekata tamaa kabisa kama siku moja nitakuja ajiriwa na najutia miaka mitatu niliyoipoteza chuoni pamoja na ada niliyoitumia kwani laiti ningejua ni bora ile ada ningeitumia kwenye kujiajiri kuliko kupote pesa na muda wangu.
Yani hapa nasubiri miujiza ya mwenyezi Mungu tu kwakweli.
Eeeh Mungu tuangalie waja wako,tuko kwenye kipindi kigumu sana.
wapi imeandikwa kuwa kila mwenye elimu ni lazima aajiriwe?

btw, lengo kuu la elimu ni kuondoa ujinga na kuongeza maarifa kichwani!

maarifa hayo ndio yatakufanya uweze kupambana na mazingira katika hali yoyote ile, ikiwemo hii ya ukosefu wa ajira..

mkuu, kama wewe wa higher learning unalia, je mwenzio uliyemwacha nyuma kwa kufeli kidato cha nne ama la 7, atakuwa na hali gani sasa?

tafadhali tumia elimu yako kuongeza tabasamu usoni mwako.. sio huzuni..
 
Tatizo la ajira nchini ni kubwa ila mimi nitapingana na mawazo ya wadau kidogo,mimi nimebaahatika kuwafanyia usahili zaidi ya watanzania elfu mbili mpaka sasa na nimegundua kuwa kuna tatizo kubwa katika mifumo yetu ya elimu,unakuta mtu ana masters lakini ukimuuliza maswali rahisi tu yanayolenga kupima uwezo wake binafsi inasikitisha,wengine lugha ya kiingereza ambayo ni msingi kwa kampuni nyingi za binafsi ni matatizo
My take is ukikutana na mtu aliyeomba kazi sehemu zaidi ya tano bila kupata ana matatizo na wewe unaejuta unaweza kuwa mmoja wao.
Mtu kubali kuanza chini ujenge uzoefu na utagrow in three years katika level unayotaka nina mifano hai kabisa,kama huna habari makampuni yanatumia mamilioni ya shilingi kwenda nchi za nje kutafuta watanzania wanaosoma huko kuja kufanya kazi tanzania na eanachukua fresh graduates tusilalamike bila sababu

Sikubaliani na wewe hata kidogo...kazi haipimwi kwa mtu kujua kiingereza na kama alikua hajui kiingereza alifikaje chuo...na kama kiingereza ndio kujua kazi wachina hawa wasingepata tenders na ajira nchi za kiafrika kwani asilimia 90 wanazungumza kichina, na pia ili suala halipingiki kazi ni kuhonga au kua na God Father hapa bongo au tuambie hao watu uliobahatika kuwafanyia interview hakuna wengine umeambiwa na mkubwa wako hawa wape kazi ingali hata kabla kukutana nao wewe, UONGOOO!??Tusidanganyane bwana wee mpe mtu moyo wa kuendelea kutafuta ila usimwambie lugha ya kiingereza ndio tatizo mie nakataa mara 800!!!
 
Be strong and of good courage. it is written!
Tusimlaumu huyu ndugu; mwingine ana mawazo na plan nzuri tu za kujiajiri ila kitu Mtaji hana na pakuanzia hapaoni!ndugu yetu kwanza anahitaji kitu kinaitwa 'psychotherapy' baada ya hapo unaweza kumshauri kitu akakuelewa! Pole sana ndugu, ila usikate tamaa, wazung wanasema "every successful man has a sad story". Kwa upande wangu mimi ntkuambia hiyo yako sio sad story kabisa!
 
Nlihangaika sana kutafuta ajira,nkatafuta mahali pa kujitolea,nlifanya kazi kwa bidii sana huku nkiwa silipwi hata kumi.Mara nyingi nlitoka saa mbili usiku,na ikilazmika nafanya hadi saa tano usiku.Hatimaye wakaniajiri kutokana na ule moyo nlikuwa nao wakufanza kazi.Nakushauri tafuta mahali pakujitolea,fanya kazi kama unalipwa,fanza kwa moyo,acha kunungunika kwenye kazi,fanya kazi yeyote ile ktk kitengo hcho,nakuhakikishia hakuna mwajiri asipenda mtu mchapakazi,atakuajiri tu.
 
Wewe umepita tu shule ila hujaelimika! Akili yako haina tofauti na Gari ya kwanza iliyotengenezwa na Henry Ford ambayo haikuwa na gear ya rivasi (reverse)!
 
Mimi huwa ninashangaa kidogo, hivi lengo halisi la kupata elimu(kusoma)huwa ni kuajiriwa?
Mtu anajuta kusoma hadi chuo kikuu kisa hajaajiriwa!!??

Eti mkuu, au mimi fikra zangu ndio zimepotoka, watu wa karibu yangu huwa wananishangaa sana nikisema kuwa nitasoma fani, sio kwa kuangalia kuwa fani husika ina soko, ila kwa sababu ninaipenda hiyo kitu, I want to be deep about it and I will do it regardless of payments.
ua in my mind,,,,,because being deep into it will make u competent in a way u can employ your self
 
Sikubaliani na wewe hata kidogo...kazi haipimwi kwa mtu kujua kiingereza na kama alikua hajui kiingereza alifikaje chuo...na kama kiingereza ndio kujua kazi wachina hawa wasingepata tenders na ajira nchi za kiafrika kwani asilimia 90 wanazungumza kichina, na pia ili suala halipingiki kazi ni kuhonga au kua na God Father hapa bongo au tuambie hao watu uliobahatika kuwafanyia interview hakuna wengine umeambiwa na mkubwa wako hawa wape kazi ingali hata kabla kukutana nao wewe, UONGOOO!??Tusidanganyane bwana wee mpe mtu moyo wa kuendelea kutafuta ila usimwambie lugha ya kiingereza ndio tatizo mie nakataa mara 800!!!

uzuri wa Jf watu wanapingana kwa hoja,,,,mdau kimilanzoka tunasubir argument
 
Last edited by a moderator:
Umenikumbusha wakati nataka kwenda chuo, niligombana sana na mzee wangu, alitaka nisome electrical engineering sababu inalipa, nikasema sisomi kitu ambacho sikipendi ng'o. Nikaenda kuibuka na kozi hata hawakuwa wanaelewa nitaajiriwa wapi, lakini ndio kitu nilikuwa napenda, sijawahi regret aisee.

Hakuna kitu kizuri kama kusoma kitu unachopenda, hata darasani huhangaiki sana na mambo yakiwa magumu hulaumu mtu, kiroho safi.

Eti mkuu, au mimi fikra zangu ndio zimepotoka, watu wa karibu yangu huwa wananishangaa sana nikisema kuwa nitasoma fani, sio kwa kuangalia kuwa fani husika ina soko, ila kwa sababu ninaipenda hiyo kitu, I want to be deep about it and I will do it regardless of payments.
 
Kukata tamaa ni vibaya sn mkuu,i understand ur situation..nilikuwa km ww nilipokaa kitaa miaka mitatu bila kazi,lkn sikukata tamaa,niliendelea kukomaa huku nikimuomba Mungu.
utakuja kupata kazi tu,mi nilipata kazi ambazo hata ndugu zangu wanashangaa nilipata vp.sikuwa na god faza wala nn ni msaada wa Mungu tu.mpk sasa nimefanya kazi km sehem tatu tofauti,mwanzo nilikuwa nataman kaz yoyote ile lkn sasa nacheck maslah.so nawe utapata tu mkuu,muamin Mungu,kama alikupa degree bas na kaz atakupa...
Usijali kuwa mpole na mwamini Mungu nae atakuthibitisha kwa kazi itakayokushangaza itakayokufanya usahau machungu na kukata tamaa kwingi ulikopitia. Mungu na akufungulie mlango wake mr
 
Inakuwaje Mbishi 4 real halafu unakata tamaa katika mihangaiko ya dunia hii,Jina ulilotumia ni kinyume kabisa na tabia uliyo nayo.Muombe Mungu usikate tamaa na ukishapata hiyo kazi endelea kumtumikia Mungu siyo kuchota mihela hata ya watoto yatima kwa kuhongea mabinti,sawa!!! :hat:
 
Last edited by a moderator:
Tatizo mnasoma kozi kwa kufuata mkumbo bila kuangalia soko la ajira.Mara BBA,HR,Socilogy n.k.Ungesoma education ungejikuta sasa hivi unapiga mluzi tu.Somo zuri sana wengine wajifunze

Kitu BAED
 
Wewe umepita tu shule ila hujaelimika! Akili yako haina tofauti na Gari ya kwanza iliyotengenezwa na Henry Ford ambayo haikuwa na gear ya rivasi (reverse)!

Eeeeeeh😱😕😕😕😕😕😕😱😱😱
 
Mimi huwa ninashangaa kidogo, hivi lengo halisi la kupata elimu(kusoma)huwa ni kuajiriwa?
Mtu anajuta kusoma hadi chuo kikuu kisa hajaajiriwa!!??

Eti mkuu, au mimi fikra zangu ndio zimepotoka, watu wa karibu yangu huwa wananishangaa sana nikisema kuwa nitasoma fani, sio kwa kuangalia kuwa fani husika ina soko, ila kwa sababu ninaipenda hiyo kitu, I want to be deep about it and I will do it regardless of payments.

wewe umenena, eti mtu anapost humu kuuliza "nisomee kozi gani kwa matokeo haya?' yani yeye hana ambition yoyote anataka watu wa jf ndo wamchagulie, mi mwanangu wa miaka nane tayari anaijua ndoto yake, he wants to become a president... lol.
 
Hili suala la mtu kusomea kitu kwa sababu tu amesikia inalipa sana au ina soko ndio sababu mojawapo ya kuzalisha mbumbumbu, Anakuwa hayuko interested na kitu hicho ila anafuata tu mshahara, matokeo yake anakuwa anasomea cheti, yaani lengo lake ni kupata cheti tu, hajali yuko "deep"kiasi gani kwenye hiyo fani!!!

Nachukia sana watu wanaosomea vyeti.
Umenikumbusha wakati nataka kwenda chuo, niligombana sana na mzee wangu, alitaka nisome electrical engineering sababu inalipa, nikasema sisomi kitu ambacho sikipendi ng'o. Nikaenda kuibuka na kozi hata hawakuwa wanaelewa nitaajiriwa wapi, lakini ndio kitu nilikuwa napenda, sijawahi regret aisee.

Hakuna kitu kizuri kama kusoma kitu unachopenda, hata darasani huhangaiki sana na mambo yakiwa magumu hulaumu mtu, kiroho safi.
 
Usikate tamaa wewe mbishi dhihirisha ubishi wako lol...
 
wewe umenena, eti mtu anapost humu kuuliza "nisomee kozi gani kwa matokeo haya?' yani yeye hana ambition yoyote anataka watu wa jf ndo wamchagulie, mi mwanangu wa miaka nane tayari anaijua ndoto yake, he wants to become a president... lol.
Teh teh teh!!!
He wants to become a president!!!, huyo mtoto wako yuko bright, hata kama haijawa clear kwake kwamba atasomasomaje, lakini he can see a "a big person"in him. He sees that he has a destiny, very good.
 
Kijana pole sana nafsi yako imekata tamaa ukisoma Zabur42:5 inaeleza suala lako hapo nafsi imeinama Mtumaini Mungu utatoka .Mimi ni mfano tosha kwako katika familia yangu ndo wa Kwanza kuingia hicho chuo kikuu kwanza nlimshukuru Mungu kunipa hiyo nafasi mana kaka zang na dada hawakufika hyo level. Baada ya kupata elimu mtihani wa kutafuta kazi ulikuja nikiangalia huko ofisini sina hata wa kunipigia debe . Nashukuru nlianza maombi nikiwa mwaka wa tatu 2012 semister ya mwisho nkatoa na fungu la Kumi katika boom langu nkamwambia Mungu unitetee mana sina uzoefu wala ndugu mambo nliyofanya ni Maombi changaya na sadaka na kufunga mbona kazi nlipata Tangu mwaka jana yani nlikuwa nalala bt saa 9ucku lazima niamke kufanya maombi ndug yangu Mungu anasikia maombi ya mwenye haki mind you ukiamua kutumia mbinu hii uache dhambi mana maombi ya mwenye dhambi ni kelele kwa Mungu chunga sana hapa. My miracle come this way niko home nimekaaa akanipigia simu mtu ambaye ni graduate kama akiniambia kuna ofisi inatak mtu wa kuvolunteer nkamwambia niko tayari hapo ndo kazi ilianzia hapo mpaka leo .Soma mifano hii katika Luka 11 na 18. unakomaa mpaka Mungu anacheka .MUNGU AKUBARIKI
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom