Najuta Kusoma hadi chuo Kikuu

Najuta Kusoma hadi chuo Kikuu

Tatizo la ajira nchini ni kubwa ila mimi nitapingana na mawazo ya wadau kidogo,mimi nimebaahatika kuwafanyia usahili zaidi ya watanzania elfu mbili mpaka sasa na nimegundua kuwa kuna tatizo kubwa katika mifumo yetu ya elimu,unakuta mtu ana masters lakini ukimuuliza maswali rahisi tu yanayolenga kupima uwezo wake binafsi inasikitisha,wengine lugha ya kiingereza ambayo ni msingi kwa kampuni nyingi za binafsi ni matatizoMy take is ukikutana na mtu aliyeomba kazi sehemu zaidi ya tano bila kupata ana matatizo na wewe unaejuta unaweza kuwa mmoja wao.Mtu kubali kuanza chini ujenge uzoefu na utagrow in three years katika level unayotaka nina mifano hai kabisa,kama huna habari makampuni yanatumia mamilioni ya shilingi kwenda nchi za nje kutafuta watanzania wanaosoma huko kuja kufanya kazi tanzania na eanachukua fresh graduates tusilalamike bila sababu
Nakuunga mkono mdau, Nakumbuka siku moja tulikaa staff kadhaa na kuli discuss hili. Utakuta graduate anakuonesha vyeti vyake unashtuka. Ma GPA ya kufa mtu. Ma AA ya kumwaga. Haya mpe nafsi sasa uone madudu anayoyafanya. Mpaka muda mwingine unasema je ni kiwango cha elimu ndio kimeshuka ama?
 
Nimeishakutana na watu kama hawa kibao wana vyeti ila uwezi binafsi mdogo,mi nimeona madogo kibao tu hawana experience lakini mziki wao aibuuu
 
Jipe moyo mkuu mtumaini Mungu atakuwezesha yeye hutupitisha ktk magumu tusiyoyajua....
 
Baadhi ya sifa za mtu mwenye stress, ni kujuta, kuwa na mtazamo hasi, na kuangalia mambo ya nyuma. Aliyekuambia ukifika University utapata kazi baada ya wiki moja ni nani? Unapotafuta kazi ya kwanza omba kazi yoyote, hata kuwasaidia watu wanaoreseat masomo uliyosoma shule, ili upate nauli za kuzungukia unapoendelea kutafuta kazi. Ukishapata kazi ya kushikiza, kisha uendelee kutafuta kazi nyingine. Jifunze pia kuwa mvumilivu, kukata tamaa sio sifa za mtu mwenye nia ya kuendelea!

nimependa mistar yako ndugu, umendka point, bse mi pia nshawah kuwa na dalili hzo
 
Elimu yako imekufundisha nini kuhusu kubadilika kwa mujibu wa mazingira, kurekebisha makosa, kujiajiri na kujitegemea?

Umesomea nini?
Mimi huwa ninashangaa kidogo, hivi lengo halisi la kupata elimu(kusoma)huwa ni kuajiriwa?
Mtu anajuta kusoma hadi chuo kikuu kisa hajaajiriwa!!??

Eti mkuu, au mimi fikra zangu ndio zimepotoka, watu wa karibu yangu huwa wananishangaa sana nikisema kuwa nitasoma fani, sio kwa kuangalia kuwa fani husika ina soko, ila kwa sababu ninaipenda hiyo kitu, I want to be deep about it and I will do it regardless of payments.
 
Mimi huwa ninashangaa kidogo, hivi lengo halisi la kupata elimu(kusoma)huwa ni kuajiriwa?
Mtu anajuta kusoma hadi chuo kikuu kisa hajaajiriwa!!??

Eti mkuu, au mimi fikra zangu ndio zimepotoka, watu wa karibu yangu huwa wananishangaa sana nikisema kuwa nitasoma fani, sio kwa kuangalia kuwa fani husika ina soko, ila kwa sababu ninaipenda hiyo kitu, I want to be deep about it and I will do it regardless of payments.

Ni ugonjwa wetu ule ule wa kila siku wa kufanya mambo kwa mkumbo na utamaduni, bila kujiuliza.

Na kutumaini tu mambo yataenda sawa.

Dunia inabadilika, enzi za wazee wetu ukimaliza chuo cha East African Community una guarantee ya kupewa kazi nzuri na kufanya shirika hilo hilo kwa miaka 35 mpaka unastaafu zimepita na hazirudi.
 
tatizo lako ulisoma ili uje uajiriwe.
itakugharimu mpaka uzee wako.
stuka sasa.
 
Mimi huwa ninakatisha tamaa watu wanaosoma ili wapate hela(wawe matajiri).
Huwa ninawaambia tafuta mtaji tu anza biashara, matajiri wengi hawajasoma.

Personally, I always argue that the aim of education should be pursuit of wisdom, not wealthy.
Ni ugonjwa wetu ule ule wa kila siku wa kufanya mambo kwa mkumbo na utamaduni, bila kujiuliza.

Na kutumaini tu mambo yataenda sawa.

Dunia inabadilika, enzi za wazee wetu ukimaliza chuo cha East African Community una guarantee ya kupewa kazi nzuri na kufanya shirika hilo hilo kwa miaka 35 mpaka unastaafu zimepita na hazirudi.
 
Inawezekana hili jina unalotumia humu JF linasadifu tabia yako halisi...fanya kumwomba admin ubadili jina labda litakusaidia.Kwa sisi tuaminio maandiko tunaamini Sauli alipobadili jina na kuwa Paulo haiba yake ilibadilika pia
 
Ni Aibu mtu wa chuo kikuu kuajiriwa. Yeye ndiye alitakiwa kuvumbua vitu, kuanzisha taasisi na kuwaajiri ma Form Four
 
YEREMIA 32 ; 27
Ukiisoma inakufaa sana na mbele utaona tumaini la kuaminika.
 
Kukata tamaa ni vibaya sn mkuu,i understand ur situation..nilikuwa km ww nilipokaa kitaa miaka mitatu bila kazi,lkn sikukata tamaa,niliendelea kukomaa huku nikimuomba Mungu.
utakuja kupata kazi tu,mi nilipata kazi ambazo hata ndugu zangu wanashangaa nilipata vp.sikuwa na god faza wala nn ni msaada wa Mungu tu.mpk sasa nimefanya kazi km sehem tatu tofauti,mwanzo nilikuwa nataman kaz yoyote ile lkn sasa nacheck maslah.so nawe utapata tu mkuu,muamin Mungu,kama alikupa degree bas na kaz atakupa...
 
Elimu yako imekufundisha nini kuhusu kubadilika kwa mujibu wa mazingira, kurekebisha makosa, kujiajiri na kujitegemea?

Umesomea nini?
Siku hizi kuna kuchukua hakuna kusomea
 
Hapana!! Jitazame tena upya, msomi unaishia kulalama? Elimu inatakiwa ikupe changamoto ya wewe kupambana na kutatua changamoto kama hizo hapo sasa!! Unaposema unajutia elimu hiyo..nashindwa kukuelewa?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom