mtakavyote
Senior Member
- May 21, 2015
- 143
- 71
Too much of anything is harmful, hta dini. "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa"
Makanisa haya ni shida na yanavunja ndoa sana. Mengine yanakataza wanawake kuchangia huduma za nyumbani hata kidogo kwa kisingizio eti mwanaume ndiye kichwa cha nyumba. Kumbe wanawabana na hela zote zinaishia kanisani. Halafu waumini wanakuwa kama vile mazezeta tu na kila wanachoambiwa wanafanya. Wachungaji hawa wanaishi maisha ya kitajiri sana kumbe ni kwa kuwapumbaza na kuwaibia waumini wao. Hizi kweli ni siku za mwisho na tulishaonywa. Kila mtu na ashike sana alichonacho.
Huyo mke watamshauri huko kanisani akuache kwani ni dhambi kwa mlokole kuolewa na mtu ambaye hajaokoka. Pole!
Sijahalalisha, ila kinachotakiwa mume amshawishi mkewe kwa upendo. Mimi binafsi mke wangu alikuwa akisali kanisa fulani sitaki kulitaja, lilikuwa na ratiba kama ya mke wa mtoa uzi. Nilimwacha mke wangu akiendelea kusali kama kawaida huku nikimshawishi kujali familia yake kwa kutumia biblia ileile. Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa soma mwanzo. Mke anapaswa kumtii mumewe na mume anapaswa kumpenda mkewe kama mwili wake. Mtu amwenye upendo hawezi kuupiga mwili wake hadi kuutengua ubavu. Biblia inatuasa ' mke anayeishi na mume asiyeamini asimwache kwa maana mume aweza kuokoka kwa kuangalia matendo ya mkewe. Mke mwema ana wajibu wa kutunza familia yake kwa umahiri mkubwa.
Mwisho, kwa kuwa nilikuwa natumia pia mafundisho ya biblia, mke wangu akaona ni kweli. Dini inapswa iwe ile iletayo upendo katikati ya chuki, ilete faraja miungoni mwa wenye ndoa, ilete gundi ya kuwaunganisha badala ya kuwatenganisha, kwa maana imeandikwa 'alichokiunganisha Mungu mwanadamu asitenganishe. Biblia inasema tuonyane kwa upendo siyo kwa kutenguana mbavu. Shughuli nzima ya mapenzi ni ya kubembelezana, kama huwezi kubembeleza na kubembelezwa hakika huwezi mapenzi. Acha fanya kazi nyingine, lakini hakuna kazi nyingine mbala wa mapenzi
ukweli lazima usemwe, kuna mmoja nilikutana naye tulipishana kama hatujuani, alivaa soksi imembana hatari wakati mwanzo alikuwa anazipiga vvita na kupondea, shame on them walokole!
makubwa madogo ya na nafuu kweli unampiga mtoto wa watu kisa nini jamani
si ungemwacha tu kwani yeye kaamua hivyo
si busara kuingilia uhuru wa mtu mwache afanye atakavyo yaani wewe unarushia ngumi utadhani
unapiga gunia kumbe mtu mwenye moyo na nyama kwanini wanaume mmekuwa mafisadiwa utu wa mtu?
Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa
Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.
Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.
Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi
Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.
Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu
Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana
Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.
Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao
Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa
Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena
Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.
Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?
Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?
Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense
Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.
Mkuu matatizo yako na wife ni makubwa lakini siwezi ungana na wewe mkono katika swala zima la kumpiga mwanamke, nashangaa watu hawaiongelei hili, Hivi we mtu mzima kweli unampiga mke wako hadi anazimia? Chunga sana utaletewa kesi ya mauaji siku moja, unamgusa kidogo tu mwanamke wa watu anakufa moja kwa moja.
Kwanza achana na kumpiga mke wako unaonekana mgomvi sana, mimi lawama zangu zinaenda kwako na si kwa mke wako, sababu umeshindwa kumcontrol, hakuna kitu rahisi kama kumcontrol mwanamke sijui watu hua mnashindwa vipi, jaribu kucheza na psychology yake tu, kupunguza frequency za kwenda kanisani its very possible na ni kitu rahisi sana, tatizo tabia yako inaonekana ya kigomvi sana, kumbadilisha akili mwanamke kama huyo itakutoa jasho