Najuta kuoa mwanamke mlokole

Najuta kuoa mwanamke mlokole

Too much of anything is harmful, hta dini. "Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa"
 
Makanisa haya ni shida na yanavunja ndoa sana. Mengine yanakataza wanawake kuchangia huduma za nyumbani hata kidogo kwa kisingizio eti mwanaume ndiye kichwa cha nyumba. Kumbe wanawabana na hela zote zinaishia kanisani. Halafu waumini wanakuwa kama vile mazezeta tu na kila wanachoambiwa wanafanya. Wachungaji hawa wanaishi maisha ya kitajiri sana kumbe ni kwa kuwapumbaza na kuwaibia waumini wao. Hizi kweli ni siku za mwisho na tulishaonywa. Kila mtu na ashike sana alichonacho.

Huyo mke watamshauri huko kanisani akuache kwani ni dhambi kwa mlokole kuolewa na mtu ambaye hajaokoka. Pole!

hivi ulitaka stress kama hii haimalizie wap kama si jf? Walokole malaya hadi wazazi washakuwa chizi itakuwaje mke atelekeze mtoto mdogo ivo kisa kanisani? Sote tunampenda mungu kama aliona mme wake sio hawataendana ilibidi aolewe na walokole wenzake.

Ebu amchalaze. Tena ulisahau kabla hajamchalaza ilibidi achepuke siku mbili alale ukoooo mke atikoka kanisani akute mme hayupo tuone. Loh shameless woman
 
Sijahalalisha, ila kinachotakiwa mume amshawishi mkewe kwa upendo. Mimi binafsi mke wangu alikuwa akisali kanisa fulani sitaki kulitaja, lilikuwa na ratiba kama ya mke wa mtoa uzi. Nilimwacha mke wangu akiendelea kusali kama kawaida huku nikimshawishi kujali familia yake kwa kutumia biblia ileile. Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa soma mwanzo. Mke anapaswa kumtii mumewe na mume anapaswa kumpenda mkewe kama mwili wake. Mtu amwenye upendo hawezi kuupiga mwili wake hadi kuutengua ubavu. Biblia inatuasa ' mke anayeishi na mume asiyeamini asimwache kwa maana mume aweza kuokoka kwa kuangalia matendo ya mkewe. Mke mwema ana wajibu wa kutunza familia yake kwa umahiri mkubwa.
Mwisho, kwa kuwa nilikuwa natumia pia mafundisho ya biblia, mke wangu akaona ni kweli. Dini inapswa iwe ile iletayo upendo katikati ya chuki, ilete faraja miungoni mwa wenye ndoa, ilete gundi ya kuwaunganisha badala ya kuwatenganisha, kwa maana imeandikwa 'alichokiunganisha Mungu mwanadamu asitenganishe. Biblia inasema tuonyane kwa upendo siyo kwa kutenguana mbavu. Shughuli nzima ya mapenzi ni ya kubembelezana, kama huwezi kubembeleza na kubembelezwa hakika huwezi mapenzi. Acha fanya kazi nyingine, lakini hakuna kazi nyingine mbala wa mapenzi

Huu ushauri ni mzuri saana..


We jamaa uuzingatie huu
 
Haya yote ni kwa sababu unamuwaza Rachel

Ndoa unajua maana yake wewe?
 
Huyo kashajifunza ilo si kosa hata ingawa alilifanya adi likaonekana ni kosa usimwache huyo ndo mkeo. na uko alipokua amegundua alpokua anakosea kwaiyo kama kaja muulize tu swali moja je ameona mapungufu? kama ameona mrudishe home make ni heri huyo ambae umemjua kuliko ambae utaanza kutaka kumjua.
 
Ukioa tena unafanya dhambi ya kuzini kwa mujibu wa bible,lakini pia usi "generalize"wapo wadada wengi walokole wanaojua wajibu wao na ambao wana hekima ya maisha tena mikono yao ni salama kuliko wale wa misri
 
Kwanza umenifurahisha ulipomjumlisha na shemeji kwenye kichapo.good huo ndio uanaume.

Harafu muache akaolewe na kanisa maana Hanna namna.
 
Mkuu matatizo yako na wife ni makubwa lakini siwezi ungana na wewe mkono katika swala zima la kumpiga mwanamke, nashangaa watu hawaiongelei hili, Hivi we mtu mzima kweli unampiga mke wako hadi anazimia? Chunga sana utaletewa kesi ya mauaji siku moja, unamgusa kidogo tu mwanamke wa watu anakufa moja kwa moja.

Kwanza achana na kumpiga mke wako unaonekana mgomvi sana, mimi lawama zangu zinaenda kwako na si kwa mke wako, sababu umeshindwa kumcontrol, hakuna kitu rahisi kama kumcontrol mwanamke sijui watu hua mnashindwa vipi, jaribu kucheza na psychology yake tu, kupunguza frequency za kwenda kanisani its very possible na ni kitu rahisi sana, tatizo tabia yako inaonekana ya kigomvi sana, kumbadilisha akili mwanamke kama huyo itakutoa jasho
 
Sredi zingine unajikuta unacheka badala ya kusikitika.

Stoo......kutenguliwa mbavu... Oooh Rachel.

Lol
 
Maisha twenyewe tufupi utu; usikubali kabisa mtu akuties stress. Hatujaletwa duniani kupata tabu bana. Usimrudie, itakugharimu sana. Akirudi atapambana akubadilishe. Nawe unaonekana nunda, hautabadilika. Utampiga tena akufie bure; maskini hautaweza hata kupost hapa maana utakua unanyea debe segerea huko. Mwaambie aende tu...aongeze maombi atapata mwenzake anayependa hiyo ratiba na wakaishi kwa furaha milele yao yote.
 
ukweli lazima usemwe, kuna mmoja nilikutana naye tulipishana kama hatujuani, alivaa soksi imembana hatari wakati mwanzo alikuwa anazipiga vvita na kupondea, shame on them walokole!

Kuna mlokole nilisoma nae chuo tukiwa hostel tunatoka anavaa kimini na kanga,
Tukifika kwenye usafiri anaficha kanga,
Ila akiingia darasani ni mwendo wa charanga na Magauni..
Kiukweli nilikua namuambia tu aache unafiki maanake ulokole si kumridhisha binaadamu Bali Mungu pekee!
 
Vioja haviishi. Yaan kiukwel hapo huna mke. Anamwachisha mtoto na miez sita na wazazi wanamuunga mkono? Too bad! Hajitambui na hayuko tayari kibadilika kwasabababu kwanza anaburuzwa na ndg zake. Maandiko yanasema mke na mume wataambatana na kuwa kitu kimoja. Sasa huyo kakuachia housegerl akulelee mtoto maanake anataka huyohuyo housegerl akupe unyumba alafu mwisho wa siku atalalamika. Jaman wanaopata bahati za kuolewa wanazichezea.
 
makubwa madogo ya na nafuu kweli unampiga mtoto wa watu kisa nini jamani
si ungemwacha tu kwani yeye kaamua hivyo

si busara kuingilia uhuru wa mtu mwache afanye atakavyo yaani wewe unarushia ngumi utadhani
unapiga gunia kumbe mtu mwenye moyo na nyama kwanini wanaume mmekuwa mafisadiwa utu wa mtu?

wanawake katika kutetea upumbavu wao
 
Kweli mwanamke mpumbavu huvunja nyumba kwa mikono yake menyewe. Achn na huyo mama kwani hakufai na pia adabu hana, m'mke mwenye hekima, heshima na busara kwa mumewe anapoambiwa jambo fulan acha bas anapaswa kuacha hrka.. Na km hujaridhika na amri yake ukiwa faragha mueleweshe taratibu kwa upole kuwa unaomba jambo fulan uendelee kulifanya na km mpk hapo imeshindikana basi ni uliache kabsa.Ila kutaka kujifanya kweny nyumba eti vichwa vimelingana bas utaumia wew utamuacha yeye. Be obedient to your man
 
Miezi miwili iliyopita nilipelekwa polisi na wazazi wa mke wangu, kwa kosa la kumpiga binti yao karibu nimuue, ndugu walikuja kunitoa

Iko hivi;
Huyu binti nilimuoa miaka miwili iliyopita na tuna mtoto mmoja, yeye na wazazi wake wote wameokoka, Hivi sasa naweza kusema kwamba mke wangu ameolewa na kanisa na si mimi.

Akitoka kazini saa kumi na moja jioni anakwenda kwenye maombi kanisani hadi saa tatu , na hii ratiba ni kila siku Monday to Friday, Jumamosi pia wanakwenda Jumapili ni kutwa nzima, wakati mwingine kuna mkesha katikati ya wiki, hali hii, imefanya ashindwe hata kupataa muda wa kumlea mtoto wetu wa mwaka alielazimika kumwachisha ziwa akiwa na miezi mitatu kutokana kubanwa na mambo ya kanisa.

Mtoto huyu ni kama amebadilishiwa mama, maana sasa analelewa na house girl wetu kwa hali na Mali
Ilifika pahala nikashindwa kuvumilia hali hii na nikamuita na kumueleza hali halisi na kumtaka abadilishe ratiba zake, akadai kwamba hana jinsi kwa kua ratiba ya kanisa kwake haina substitute , nikamwambia ni amri sio ombi

Akaendelea hivyo hivyo, kwa Mara ya kwanza nilimpa kipigo kwa kukaidi amri yangu, niliendelea kumpiga mara kwa Mara sababu ikiwa ni kanisa, kila tunapoitwa kusuluhishwa wazazi wake humtetea na kudai walikosea kunipa mm binti yao, ikawa tunagombana na wazazi wake vikaoni hadi nikaamua kuachana na vikao.

Mwanzoni mwa mwezi wa sita alidai kuna mkesha wa maombi siku hiyo na hivyo atalala huko, nikamwambia ukitoka huko utafute nyumba nyingine, baadae mama yake akanipigia kwamba kuna mkesha hivyo wote watalala church kwenye mkesha, nikamjibu haiwezekani wamruhusu wife arudi kwa kuwa ana mtoto mdogo, akakata simu

Kweli, wife hakurudi, ila kila saa alikua akinipigia simu karibu usiku kucha nami sikua napokea naiangalia tu hadi inakatika hadi saa kumi alfajiri, alikuja amesindikizwa na dada yake maana walijua nimekasirika sana

Walipofika tu niliwakamata wote wawili na kuwapa kipigo kizito sana hadi wife kuzirai, dada mtu aliniponyoka na kukimbilia main road huku nikiwa nimemtengua mbavu akapanda boda boda, saa moja wazazi wa wife wakaja nilikua nimemfungia stoo wakamchukua wakaenda nae.

Baadae wakanifuata kazini na polisi wakaniweka ndani kwa shambulio la kudhuru mwili, nilitoka kesho yake , kesi ikahamia Ustawi wa Jamii tuliitwa pale, mbele ya wazee wa pande zote, ikaamriwa kwamba binti arudi kwa wazazi wake hadi hapo baadae hali ikiwa nzuri, ila wazazi wake wakasema wanamchukua kimoja hawanihitaji tena, kwamba nisubiri taratibu za talaka, nikasema haina shida nipo tayari, tukaja nyumbani wakamchukua mtoto na hg na nguo zake wakarudi kwao

Nimeyasahau hayo naishi kwa auheni kiasi kwa sasa Ingawa bado nina msongo, surprisingly Friday wife akanifuata kazini hatukua tumeonana for two months, roho yangu iliingia kitu flani hata mtoto wangu sikutaka hata kuwa naenda kumuona ingawa pale ustawi wa jamii niliruhusiwa

Wife akaniomba tuongee, akasema anahitaji turudiane, akadai anaomba arudi home kwangu hata kesho yake ikiwezekana, kwamba ananipenda, kwamba tutarekebisha tu, nikamwambia haiwezekani simtaki tena

Wadau wana Jf, nimemwambia atafute Mme mwingine kanisani kwao ndo watawezana na sio Mimi, mke wa hivi hanifai, hata mshahara wote anapeleka huko, hilo kanisa Jumapili moja tu kuna sadaka kama 12 hivi tangu asubuhi hadi jioni, unaweza kwenda na laki mbili usirudi hata na shilingi jioni, bado katikati ya wiki, halafu wachungaji wanaishi kifajari.

Huyo mchungaji wa hilo kanisa ameshawateka akili, mimi binafsi nilikua huko nikahama kutokana na hiyo biashara ya kutakiwa kushinda huko 24/7 na pia kutumia sehemu kubwa ya mapato yangu kanisani badala ya kujenga familia, kanisa gani wanaomba hadi salary slip? Na usipowapa watakusema sana kwamba umepotea njia na kadhalika
Kanisa gani halijali ndoa za watu?

Sio kwamba sipendi mke wangu aende kanisani, aende kwa kiasi na ratiba akizingatia kuwa yeye ni mama wa familia, inapaswa kwenda kanisani unashiriki na wenzako mchana au jioni unarudi home, jumatano unakwenda kwa maombi masaa mawili, six jioni unarudi kwako, there will be nothing wrong, lakini huwezi kwenda kushinda huko 24/7. Seven days a week, inakuja kweli hiyo?

Hata dada wa mke wangu niliempiga, mumewe pia alikuja kwangu na malalamiko kama haya ya kwangu, nimeamua simtaki tena, kwanza akili yangu imeshachanganyikiwa,
Nonsense

Ni bora nirudi kwa Rachel, alinivumilia tangu chuo hadi mtaani nikamtendea vibaya nikaoa mlokole nisiemjua, kwa kweli najuta sikujua nachofanya.

Mkuu kwanza nakushukuru kwa kujitokeza na kuomba msaada wa mawazo. Inaonesha ni jinsi gani ulivyo muungwana.
Nakupa pole kwa yaliyotokea. Kwa kiasi kikubwa kuna makosa ya kimaarifa ambayo mkeo anaonekana kuyakosa. Kushinda kanisani sio kujua neno la Mungu. Sitaki kuwashutumu wala kuwatukana ila kuna tatizo la kimsingi la ukosefu wa maarifa ya neno la Mungu hususani kwa mkeo. Milipo highlight humo na kubold nataka ni kushauri umsamehe mkeo na kumkubalia arudi nyumbani isipokuwa kwa masharti ya msingi kabisa. Kwanza, we ni muungwana sana kwa jinsi unavyoonekana uko tayari walau kumpa fursa ya siku kadha wa kadha za kwenda kanisani. Kaa nae na umweleze kinagaubaga kuwa akitaka kurudi awe tayari kufuata ratiba mpya utakayompa. Pili awe tayari kuachana na ushauri wa wazazi wake linapokuja suala la ndoa yenu.
Biblia yenyewe iko makini inaposema mke na mume wataambatana na kuwa kitu kimoja. Wakwe zako wanafanya kosa kubwa sana kuingilia sheria za nyumba yako. Kingine cha msingi awe tayari kuwaambia wazazi wake kuwa hataki kuingiliwa kwenye ndoa yenu. Hebu tuanzie hapo kwanza halafu urudi unipe mlishonyuma kwa sababu nna mengi ya kunena nawe
 
Mkuu matatizo yako na wife ni makubwa lakini siwezi ungana na wewe mkono katika swala zima la kumpiga mwanamke, nashangaa watu hawaiongelei hili, Hivi we mtu mzima kweli unampiga mke wako hadi anazimia? Chunga sana utaletewa kesi ya mauaji siku moja, unamgusa kidogo tu mwanamke wa watu anakufa moja kwa moja.

Kwanza achana na kumpiga mke wako unaonekana mgomvi sana, mimi lawama zangu zinaenda kwako na si kwa mke wako, sababu umeshindwa kumcontrol, hakuna kitu rahisi kama kumcontrol mwanamke sijui watu hua mnashindwa vipi, jaribu kucheza na psychology yake tu, kupunguza frequency za kwenda kanisani its very possible na ni kitu rahisi sana, tatizo tabia yako inaonekana ya kigomvi sana, kumbadilisha akili mwanamke kama huyo itakutoa jasho

Yeye mleta mada hana akili angekuwa na akili wala asingetumia nguvu. Mwanamke ni kiumbe rahisi sana kukibadilisha nashangaa mleta mada anampiga zaidi ya nara moja na anaona habadiliki bado anampiga wala hajiulizi shida ni nini na kipigo habadiliki yaani hii dunia ni heri unyimwe mali lakini upewe akili.
 
Nakupongeza sana kwa maamuzi uliyochukua ya kuwachapa wote wawili. Haya mambo mengine ni kupeana stress tu. Aende kanisani kwa kiasi na isiwe too much. Hakuna mtu ambaye hapendi kuabudu
 
Back
Top Bottom