Kwa maelezo yako na uwelewa wangu nianze na jinsi ninavyo kuona:
Ulipaswa kabla ya kuoa, uchunguze kwanza: Unataka mke wa kushinda kwenye baa au saloon ama kitchen party, maana hawa nao wapo ni wewe tu na upendeleo wako. Si rahisi kumbadilisha mtu mlevi akawa mlokole na mlokole akawa mlevi hivyo ulipaswa upate ready made kuliko kutransform. Mkeo, licha ya mapenzi yako ya kizamani ya kupigana pigana, amekusamehe, anataka mrudiane wewe hutaki. Maana yake huna roho ya msamaha. Waswahili husema 'Asiye samehe haliwezi penzi.' Kumbe wewe huwezi penzi ingawa unaweza kupanda.
- Mosi, unaelekeakuwa una wivu wa kupindukia kiasi kuwa hupendi mkeo atoke nyumbani hata kwa kwenda kanisani.
- Pili una udikiteta fulani, ndani mwako ni amri tu hakuna mjadala (negotiation), Unalotaka ndilo linakuwa.
- Una mapenzi ya kizamani ya kikurya ambayo yanahusisha kupigana pigana.
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatoa uhuru wa kila mtu kuabudu imani aitakayo, lakini wewe unataka mkeo aabudu namna unavyotaka wewe, hivyo bila kujua, unataka kuwa juu ya Katiba ambayo ndiyo sheria mama ya sheria zote nchini. Masikini nduyu yangu hata hujui kuwa kuvunja Katiba ni kosa. Unaishi katika jamii ya watu wasiostarabika, wastaarabu huheshimu sheria zilizowekwa. Ni wanyama wa porini ndiyo wanaoishi kama unavyotaka wewe na mkeo muishi.
Sijazungumzia upande wa mkeo wala wazazi wake kwa sababu sijawasikia, lakini kubwa ni wewe uliyeomba ushauri na wao hawajaomba chochote. Ndoa ni taasisi inapaswa iheshimiwe na watu wote ukiwemo wewe mwenye ndoa. Mtu yeyote aliyemo kwenye ndoa hushawishiwa wakati wote na mtu mmoja mmoja vikundi vya watu marafiki mbalimbali wakike kwa wakiume, lakini wewe mwenye ndoa unapaswa kuwa na ushawishi mkubwa kushinda makundi yote. Tunapomshawishi mke hatumshawishi kwa mabavu, tunamshawishi kwa hoja huku ukinyunyiza juu yake UPENDO usiopatikana mahala pengine popote isipokuwa kwako tu
Sijahalalisha, ila kinachotakiwa mume amshawishi mkewe kwa upendo. Mimi binafsi mke wangu alikuwa akisali kanisa fulani sitaki kulitaja, lilikuwa na ratiba kama ya mke wa mtoa uzi. Nilimwacha mke wangu akiendelea kusali kama kawaida huku nikimshawishi kujali familia yake kwa kutumia biblia ileile. Mungu ndiye mwanzilishi wa ndoa soma mwanzo. Mke anapaswa kumtii mumewe na mume anapaswa kumpenda mkewe kama mwili wake. Mtu amwenye upendo hawezi kuupiga mwili wake hadi kuutengua ubavu. Biblia inatuasa ' mke anayeishi na mume asiyeamini asimwache kwa maana mume aweza kuokoka kwa kuangalia matendo ya mkewe. Mke mwema ana wajibu wa kutunza familia yake kwa umahiri mkubwa.
Mwisho, kwa kuwa nilikuwa natumia pia mafundisho ya biblia, mke wangu akaona ni kweli. Dini inapswa iwe ile iletayo upendo katikati ya chuki, ilete faraja miungoni mwa wenye ndoa, ilete gundi ya kuwaunganisha badala ya kuwatenganisha, kwa maana imeandikwa 'alichokiunganisha Mungu mwanadamu asitenganishe. Biblia inasema tuonyane kwa upendo siyo kwa kutenguana mbavu. Shughuli nzima ya mapenzi ni ya kubembelezana, kama huwezi kubembeleza na kubembelezwa hakika huwezi mapenzi. Acha fanya kazi nyingine, lakini hakuna kazi nyingine mbala wa mapenzi
mwanaume kamili hapigi mke wala kulalamika. kama mtu anazingua unachukua njia yako. sioni hata haja ya kuwasema mabinti wa kilokole kwa sababu hukulazimishwa kuwa naye. kama na ameona mchungaji wake ni wa maana kuliko wewe chukua maamuzi magumu au mlowase. pia kuna ulokole na ugonjwa. ulokole hausemi mtu aharibu ndoa yake. hizo ni Imani za watu wasiojua wanachofanya. pia kisheria ukimuachisha mtoto maziwa kabla ya miezi sita unaharibu ubongo na kinga yake.
pia ungeenda kuongea na mchungaji wake. sio ustaarabu kupiga mke ambaye hulingani naye nguvu. pia hata wewe unaoneka una wenge jingi maana umempiga mke wako na kuja kumangaza hapa jf wakati yeye hawezi kujitetea. unapomsema mtu hakikisha naye yupo na anaweza kujitetea kama wewe. pia kwangu sioni tija ya ulichofanya hapa. mahusiano sio jela. mtu akizingua unajiachia kivyakooo
Acha kumshauri vibaya mwenzako,
Kwanini amle housegirl? ?
tatizo sio Rachel,tatizo ni huyo mwanamke aliyemuoa hana akili, ni bora amuache kwani ipo siku atapata kesi ya kuua, sasa yote ya nn hayo ?The red highlight is too wrong! Lengo la kuadhibu ni kurekebisha tabia-wanawake ni watoto wakubwa tu, so sometimes wanapaswa kurejeshwa kwenye njia sahihi!(kinachopaswa kuzingatiwa ni kiwango/ukubwa wa adhabu/kichapo). Binadamu tukiishi kwa kukatana/kuachana utahacha wangapi, na tutatengeneza jamii za aina gani? Naamini unaacha pale ambapo mazungumzo na adhabu zimeshindwa kufanya kazi!
Anyway, the "Rachel Gal" naona analeta balaaaaaaa! Mchepuko siyo dili japo njia kuu kuna foleni!
Mleta huu uzi nina mashaka na wewe kwa sababu kama kweli umemuoa mke mlokole basi ni lazima na wewe uwe mlokole vinginevyo ni udanganyifu unaleta hapa Jf. Swali kwako je wewe ni wa imani gani hasa?
duuuuuh mikasa hiii dunian kuna mengi