Saguda47
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 10,766
- 18,620
Ndugu zanguni Assalam!
Natumai mu-wazima wapendwa wengi wetu mkisherehekea pasaka.
Iko hivi, imetokea tatizo kati yangu na mke wangu. Kiukweli nikiri kuwa mimi ndio chanzo cha tatizo. Jana tulipishana kidogo kauli nikatoa matamshi yasiyofaa dhidi yake!! Kiukweli nilipomwambia hizo kauli alianza kulia na kulalamika kuwa simpendi japo alinivumilia sana hasa kipindi nikiwa na hali mbovu kimaisha. Nilipoyasikia hayo nikaingiwa na huzuni na huruma kubwa, nilimbembeleza jana nikadhani yameisha!
Asubuhi tena kaanza kulia, yaani nimebembeleza sana!! Ndio saivi naona katulia na kunielewa. Ukweli niseme huyu mwanamke nampenda sana na najivunia yeye kwa mchango mkubwa maishani mwangu. Toka tuoane naye sijaona tatizo la kunikwaza kihivyo. Ananipenda na ananishauri mazuri na ninafanikiwa.
Najuta sana jamani, tuwapende wake zetu. Muda mwingine sisi ndio wasababishi wa migogoro kwenye ndoa zetu. Aisee nimejifunza nitampenda zaidi na zaidi mke wangu huyu.
Pasaka njema!!
Natumai mu-wazima wapendwa wengi wetu mkisherehekea pasaka.
Iko hivi, imetokea tatizo kati yangu na mke wangu. Kiukweli nikiri kuwa mimi ndio chanzo cha tatizo. Jana tulipishana kidogo kauli nikatoa matamshi yasiyofaa dhidi yake!! Kiukweli nilipomwambia hizo kauli alianza kulia na kulalamika kuwa simpendi japo alinivumilia sana hasa kipindi nikiwa na hali mbovu kimaisha. Nilipoyasikia hayo nikaingiwa na huzuni na huruma kubwa, nilimbembeleza jana nikadhani yameisha!
Asubuhi tena kaanza kulia, yaani nimebembeleza sana!! Ndio saivi naona katulia na kunielewa. Ukweli niseme huyu mwanamke nampenda sana na najivunia yeye kwa mchango mkubwa maishani mwangu. Toka tuoane naye sijaona tatizo la kunikwaza kihivyo. Ananipenda na ananishauri mazuri na ninafanikiwa.
Najuta sana jamani, tuwapende wake zetu. Muda mwingine sisi ndio wasababishi wa migogoro kwenye ndoa zetu. Aisee nimejifunza nitampenda zaidi na zaidi mke wangu huyu.
Pasaka njema!!