Tumbiliwaulaya
JF-Expert Member
- Nov 22, 2020
- 280
- 435
Kwa muda mrefu nimekuwa nikifuatilia harakati mbalimbali za wanasiasa hapa nchini, zikiwamo oparesheni mbalimbali za vyama vya kisiasa na nyingi zikiisha kwa mafanikio makubwa, kwa faida ya vyama husika. Kati ya chache ninazo zikumbuka ni operation ya kufufua uhai wa chama cha mapinduzi, iliyoongozwa na katibu mkuu wa CCM wakati ule Abdulhaman Kinana, na katibu mwenezi wake Nape Nnauye mwaka 2015,Nyingine ni ile ya kuhamasisha mabadiriko M4C iliyofanywa na CHADEMA, ambayo ilitikisa nchi hadi slogan hiyo kufikia kutumiwa na CCM katika uchaguzi wa 2015, ili kuzima cheche za matokeo chanya ya operation hiyo.
Lakini cha kushangaza ni kuwa panapofanyika operation hizi, hakuna kusudi la moja kwa moja la chama kutaka kukiuwa chama kingine hata kama huwa ni dhamiri zilizo ndani ya wanachama wa vyama hivi viwili.
CHA AJABU: kila aliye wahi kujigamba hadharani kuwa yeye ataifutilia mbali CHADEMA mwisho wake kisiasa huwa mbaya! labda mnisaidie wenzangu kunani CHADEMA?
Mtu mmoja wa hivi karibuni kabisa ni Yule iliyejisifu kuiua CHADEMA huko Hai Kilimanjaro sasa yu almahututi kisiasa shida ni nini?
Kwa hiyo kusema CHADEMA ni mpango wa Mungu ni kweli?