Kaka Kapo
JF-Expert Member
- Nov 23, 2012
- 535
- 329
- Thread starter
- #21
Kwanza nikupe hongera kijana kwa kufanya maamuzi,kama umempata right person utajuta kwa nini hukuoa miaka kumi iliyopita!Bei za pete inategemea bajeti yako,kuanzia laki na nusu hivi mpaka mamilioni ya shilingi kutegemea unataka ya uzito gani na aina gani(silver,gold,tanzanite,e.t.c),lakini medium laki 3 na nusu hivi nne(kwa gold) zinatosha kwa watu wa kawaida.
Ni vizuri uende na huyo mchumba wako ili achague pete anayoipenda,unajua hiyo ni ya kuvaa kila siku maisha yake yote,so ukimletea kitu hapendi atateseka kuivaa isitoshe pia ni lazima afanye fitting kuona kama inamtosha!Unaweza mnunulia pete hata ya milioni 2 lakini hasiipende yeye akata pete ya laki 3!Pia bajeti yako kama inatosha mnaweza nunua pete zote hadi za ndoa kwa wakati mmoja,hii itakusaidia kupunguziwa bei lakini pia kukuweka huru ,kipindi cha maandalizi ya harusi si mchezo!Best wishes,utulie sasa karibu unakuwa baba
Ahsante sana kaka Sungura! Ntafanya hivyo mkuu!