Najikuta nina stress kupindukia

Najikuta nina stress kupindukia

Siku za hivi karibuni najiona ovyo, sina amani ndani ya moyo, muda mwingine najiuliza kwanini nilizaliwa hapa duniani.

Kuna muda machozi yananitoka ndo najihisi angalau mtu.

Nimekuwa mnyonge, hata kazini huwa akili yangu haipo serious, muda mwingine najihisi kuondoa uhai wangu.

Nimekuwa na hasira, muda mwingine huwa natumia lugha mbaya kwa wanaume wanao ni-aproach.

Naombeni ushauri tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app

TAFADHALI cutelove SOMA HAPA
Sonona (Depression): Jinsi ya kupambana nayo na kumsaidia mwathirika


Kama una stress pitia hapa, usiache kutupia na wewe maneno yako
Mtafute yule jamaa wa 7800 anaweza kukusaidia
 
Jaribu kupunguza mawazo, fanya unayoyapenda zaidi eg: movie, game, sports, sex, reading, etc.
Kuwa karibu na marafiki sahihi wenye mitazamo chanya, epuka kukaa peke yako.
 
Haya maisha yana changamoto nyng sana,jitahd kuyakabili kadri uwezavyo na kuwa makini na maamuzi utayoyachukua pengine yanaweza kukuza matatizo zaid...muombe Mungu akutangulie uweze kukabiliana nayo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana mkuu, haya mambo ya kawaida lazima yatutokee wanadamu, kama n mpenz wa kusoma soma usikae mbali na Jamii Forum mm ilinisaidia sana nikikutana na vistory vya ajabu na comment unarefresh kwa kucheka ukiwa peke yako.
Pia mtafute mtu ambae utakua unawasaliana nae mara kwa mara ambae ulishawah kukutana nae akawa faraja kwako hata kama n ex wako. Hali ya kuwasiliana na mtu ambae unampenda mara kwa mara inasaidia sana kuondoa stress.
 
Doh, ina maana unskosa amani pasi na kuwepo na chanzo chochote cha moja kwa moja?

Hapo ni shida sasa.

Ila unaposhikwa na hisia za kuchoka maisha ni lazima kuna kitu kibaya au cha kuumiza unachodhani utakiepuka wewe ukiondoka, ni kipi hicho? Kuanzia hapo watu wanaweza kupata pa kuanzia.
Kasema wanaume wakim approach anasikia hasira..
Hujajua tatizo?
 
Uta kuwa una madeni ya vikobo na hali ome colapt


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Pamoja na ushauri wa wadau utakuwa una mambo mawili matatu yanakusibu na hupati/huoni njia ya kujinasua.
1.mahusiano
2.madeni/marejesho
3.umri
4.majukumu
5.n.k
Yoye hayo yakijichanganya lazima kichwa kipate moto.
Suluhu....(nitaendelea)
 
Utakuwa labda una plans kubwa kubwaa kimaisha ila huna hata mkakati mmoja serious wa kufikia malengo yako zaidi ya kuota au kuwaza tu hayo mafanikio unayotaka kwa muda mrefu huku umri unakwenda kasi, hivyo ikiwa mafanikio yako unayowazia ni kuwa na biashara kubwa, au kujenga nyumba kubwa na nzuri au kuolewa na mwanaume wa ndoto yako etc. na time inaenda huoni chochote sbb huna any strategic approach kufanikiwa ndio akili yako inaanza hayo makirikiri na moyo unapokea na kuanza kukata tamaa.. Hiyo ndio dalili mbaya maishani, kukata tamaa. Sbb kuu sijui yako ni ipi, ila hizo ndio dalili za kuona huna mwelekeo, yaani umeanza kukata tamaa kabisa. Think first wapi umekwama, kuna kitu, sisi wote hatukijui, ni ww tu unakijua
 
Ukiwa mtu wa kutokujali hutoweza kaa na kusononeka, au kukosa raha hata siku moja
 
Wale jamaa waliosema tumo kwenye nchi zenye watu wasio na furaha hawakukosea..ni mengi yanatuvuruga..lakini hasa mahusiano na kipato kisichokidhi mahitaji.. mwisho anazaliwa bwana HOFU.

Hauko peke yako hali hii inawakumba wengi kila mmoja na namna yake ya kukabiliana nayo..lakini kimsingi epuka kukaa mwenyewe,fanya vile vitu unavyopenda..Haya maisha hatuishi milele usichukulie vitu serious sana.
 
cutelove ukifikishwa kileleni tatizo lako litakuwa solved !naweza kujitolea kwa hiari yangu mwenyewe kukufikisha kileleni


Sent using IPhone X
 
Siku za hivi karibuni najiona ovyo, sina amani ndani ya moyo, muda mwingine najiuliza kwanini nilizaliwa hapa duniani.

Kuna muda machozi yananitoka ndo najihisi angalau mtu.

Nimekuwa mnyonge, hata kazini huwa akili yangu haipo serious, muda mwingine najihisi kuondoa uhai wangu.

Nimekuwa na hasira, muda mwingine huwa natumia lugha mbaya kwa wanaume wanao ni-aproach.

Naombeni ushauri tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app

TAFADHALI cutelove SOMA HAPA
Sonona (Depression): Jinsi ya kupambana nayo na kumsaidia mwathirika


Kama una stress pitia hapa, usiache kutupia na wewe maneno yako
Pole,
Kama hutajali tuongee tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom