Naitwa Ashery Jamal Masoud, natafuta ndugu zangu. Marehemu mama yangu aliitwa Sara Mponela

ASHJAM

New Member
Mar 3, 2023
2
11
Habari zenu? Natumaini wote wa forum hii hamjambo.

Kwa jina naitwa Ashery Jamal Masoud, nina miaka 57. Nilizaliwa hapa Dar es Salaam, na nimeishi hapa miaka yote kasoro kwa kipindi fulani nilipopata kazi Dodoma.

Hapo nimeamua kujieleza kwa sababu nawatafuta ndugu zangu na natumaini mtu mmoja anaweza kujitokeza kunisaidia.

Mama yangu Sara Mponela aliolewa na Mturuki baharia ambaye alinilea mpaka nilipokuwa na miaka 14 alafu akarudi kwao.

Mama mwenyewe aliwahi kutoroka nyumbani (Kisarawe?)kuja hapa mjini alipokuwa bado msichana, hii kwa sababu hakutaka kuolewa na Mzee kwa ndoa ya kupangiwa.

Hapa Dar es Salaam akakutana na Baba yangu na mwaka 1965 alipata mimba. Kwa hiyo alijaribu kurudi kwa ndugu zake lakini alikuta wengine walishahamia mjini, wengine walimchukia kwa mimba huo.

Na ndo maana hajataka mimi niwafahamu ndugu zangu, alisema walikuwa hawampendi na mimi pia hawatanipenda.

Mama yangu kwa bahati mbaya alifariki kwenye ajali ya meli Bukoba huko Mwanza mwaka 1996, na maiti haikupatikana.Angekuwepo, mwaka huu angekuwa na miaka 75 maana alizaliwa mwaka 1948.

Na mimi nimebaki peke yangu mpaka sasa hivi naangahika na kazi zangu za fundi umeme mitaani.Maisha yameenda si vibaya na nina kazi yangu najitegemea, na hela inanitosha kwa kuishi vizuri.

Mwaka jana nilipata ajali ya bodaboda na nikaumia mguu: nilipata operesheni lakini mguu haujakaa sawa. Kwa bahati nzuri nilikutana na mtu mkubwa ambaye nilifanyakazi kwake na alinionea huruma akaniahidi kwamba nikipata paspoti atanilipia matibabu nje ambayo yatanirudisha kwenye hali ya kawaida na uwezo wangu wa kutembea bila fimbo ambaye mpaka sasa naitumia.

Hapo nilipo naishi na akiba yangu na kazi ndogo ndogo na maisha yanaenda siyo vibaya lakini nawatafuta ndugu zangu.

Hawa ndugu tulipoteana nao si kwa ajili ya ugomvi bali kwa ajili ya matakwa ya Mama yangu marehemu.

Nikimpata ndugu yangu hata mmoja ntafurahi sana alafu itanisaidia kumtambulisha Mama yangu kwenye ofisi ya kuomba paspoti maana pale wameniambia kwamba wanahitaji mtu ambaye ni ndugu ya Mama yangu kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Mama anaweza kutambulika.

Hapo nitaweza kupata paspoti, kwenda kutibiwa nje na kurudi mzima hapa nchini ili niweze kuendelea na maisha ya kawaida.

Naomba sana kama kuna mtu aliweza kumjua Mama yangu Sara Mponela na ni ndugu yake, ajitokeze basi:nitafurahi kumjua ndugu yangu mmoja na kujua kwamba sipo peke yangu dunia hii.

Samahani kama nimeeleza mengi lakini naamini kwamba kwa kutumia grupu hii yenye watu wengi nitaweza kubahatika kumpata ndugu yangu yeyote ambaye anaweza kukumbuka mambo niliyoadithia hapo.

Natanguliza shukrani kwa wote na Mungu awabariki katika maisha yenu.

Namba yangu ya simu ni: 0655-404494

Asante,

Ashery Jamal Masoud
 
Pole sana ndugu yangu, weka picha ya mama na huyo baba kama ipo hii itakuwa rahisi kuwatambua,maana sehemu zingine watu hutambulika kwa majina mengine au ya utani.
 
Pole sana ndugu yangu, weka picha ya mama na huyo baba kama ipo hii itakuwa rahisi kuwatambua..
Ahsante Kwa ushauri wako. kwa bahati mbaya mpaka mwaka ule Mama yangu alipofariki, Kwa Sisi watu wa chini ilikuwa si kawaida kupiga picha maana hapa namwongelea mtu aliozaliwa mwaka 1948.

Naomba uiposti hivyo hivyo Bila kitu linguine maana naamini kwamba ndug kami wapo watakumbuka stori hii.

Halafu Mkuu Jana nimepokea msg kutoka Kwa mtu kama ifuatavyo.

Habari vp ndugu yng, shkamoo, nimepata namba yako jamii forum. Samahani naomba msaada ndugu yangu mimi naitwa mashaka ni kijana wa miaka28 na baba wa watoto wawili, ni mwalimu kitaaluma nina miez4 sina kaz nafanya vibarua, nipo kahama, sijala na familia yangu tangia jana asubuhi, naomba msaada hata wa kilo1 ya unga wa ugali,
Nimeshangaa Kwa sababu kama posti bado haijawekwa kwenye forum maana yake ni kwamba kuna mtapeli kwenye staff yenu?

Ukihitaji nitakutumia namba
 
Ahsante Kwa ushauri wako. kwa bahati mbaya mpaka mwaka ule Mama yangu alipofariki, Kwa Sisi watu wa chini ilikuwa si kawaida kupiga picha maana hapa namwongelea mtu aliozaliwa mwaka 1948.

Naomba uiposti hivyo hivyo Bila kitu linguine maana naamini kwamba ndug kami wapo watakumbuka stori hii.

Halafu Mkuu Jana nimepokea msg kutoka Kwa mtu kama ifuatavyo.

Habari vp ndugu yng, shkamoo, nimepata namba yako jamii forum. Samahani naomba msaada ndugu yangu mimi naitwa mashaka ni kijana wa miaka28 na baba wa watoto wawili, ni mwalimu kitaaluma nina miez4 sina kaz nafanya vibarua, nipo kahama, sijala na familia yangu tangia jana asubuhi, naomba msaada hata wa kilo1 ya unga wa ugali,
Nimeshangaa Kwa sababu kama posti bado haijawekwa kwenye forum maana yake ni kwamba kuna mtapeli kwenye staff yenu?

Ukihitaji nitakutumia namba
Matapeli wapo mkuu
 
Pole mno mkuu kwa yote yaliyokukuta, haya ndio matokeo ya kutawaliwa na watawala walio selfish, wakoloni walikuwa na utaratibu wa kutunza hizi kumbukumbu za uraia, walipoingia wakoloni weusi wakavuruga systems yote, lingekua jambo rahisi kwako kwenda home affairs na jina kamili la mama yako, officials wange run hili jina kwenye systems (finger prints ni sehemu yake)definitely ungepata pa kuanzia kwa sasa, jaribu kurudi tena kisarawe anzia kule ila unahitaji muda na fedha, good luck
 
Habari zenu? Natumaini wote wa forum hii hamjambo.

Kwa jina naitwa Ashery Jamal Masoud, nina miaka 57. Nilizaliwa hapa Dar es Salaam, na nimeishi hapa miaka yote kasoro kwa kipindi fulani nilipopata kazi Dodoma.

Hapo nimeamua kujieleza kwa sababu nawatafuta ndugu zangu na natumaini mtu mmoja anaweza kujitokeza kunisaidia.

Mama yangu Sara Mponela aliolewa na Mturuki baharia ambaye alinilea mpaka nilipokuwa na miaka 14 alafu akarudi kwao.

Mama mwenyewe aliwahi kutoroka nyumbani (Kisarawe?)kuja hapa mjini alipokuwa bado msichana, hii kwa sababu hakutaka kuolewa na Mzee kwa ndoa ya kupangiwa.

Hapa Dar es Salaam akakutana na Baba yangu na mwaka 1965 alipata mimba. Kwa hiyo alijaribu kurudi kwa ndugu zake lakini alikuta wengine walishahamia mjini, wengine walimchukia kwa mimba huo.

Na ndo maana hajataka mimi niwafahamu ndugu zangu, alisema walikuwa hawampendi na mimi pia hawatanipenda.

Mama yangu kwa bahati mbaya alifariki kwenye ajali ya meli Bukoba huko Mwanza mwaka 1996, na maiti haikupatikana.Angekuwepo, mwaka huu angekuwa na miaka 75 maana alizaliwa mwaka 1948.

Na mimi nimebaki peke yangu mpaka sasa hivi naangahika na kazi zangu za fundi umeme mitaani.Maisha yameenda si vibaya na nina kazi yangu najitegemea, na hela inanitosha kwa kuishi vizuri.

Mwaka jana nilipata ajali ya bodaboda na nikaumia mguu: nilipata operesheni lakini mguu haujakaa sawa. Kwa bahati nzuri nilikutana na mtu mkubwa ambaye nilifanyakazi kwake na alinionea huruma akaniahidi kwamba nikipata paspoti atanilipia matibabu nje ambayo yatanirudisha kwenye hali ya kawaida na uwezo wangu wa kutembea bila fimbo ambaye mpaka sasa naitumia.

Hapo nilipo naishi na akiba yangu na kazi ndogo ndogo na maisha yanaenda siyo vibaya lakini nawatafuta ndugu zangu.

Hawa ndugu tulipoteana nao si kwa ajili ya ugomvi bali kwa ajili ya matakwa ya Mama yangu marehemu.

Nikimpata ndugu yangu hata mmoja ntafurahi sana alafu itanisaidia kumtambulisha Mama yangu kwenye ofisi ya kuomba paspoti maana pale wameniambia kwamba wanahitaji mtu ambaye ni ndugu ya Mama yangu kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Mama anaweza kutambulika.

Hapo nitaweza kupata paspoti, kwenda kutibiwa nje na kurudi mzima hapa nchini ili niweze kuendelea na maisha ya kawaida.

Naomba sana kama kuna mtu aliweza kumjua Mama yangu Sara Mponela na ni ndugu yake, ajitokeze basi:nitafurahi kumjua ndugu yangu mmoja na kujua kwamba sipo peke yangu dunia hii.

Samahani kama nimeeleza mengi lakini naamini kwamba kwa kutumia grupu hii yenye watu wengi nitaweza kubahatika kumpata ndugu yangu yeyote ambaye anaweza kukumbuka mambo niliyoadithia hapo.

Natanguliza shukrani kwa wote na Mungu awabariki katika maisha yenu.

Namba yangu ya simu ni: 0655-404494

Asante,

Ashery Jamal Masoud

Mkuu samahani ,ikikupendeza uweke majina matatu ya mama .
 
Pole sana Mkuu

Shida inaweza kuwa hata nao wasikukubali km wewe jinsi ambavyo hukuwakubali kwa kukaa kimya muda woote ukimsingizia mama ila kwa kuwa yamekukuta na Una shida ndo unawatafuta

Ila mungu ni mwema unaweza kuwapata
 
Back
Top Bottom