Kalamu Nzito
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 318
- 662
Leo nipo safarini kuelekea Dar es salaam kupitia route ya Msata-Bagamoyo. Nimepita hotel ya kitalii ya KIROMO VIEW RESORT ambayo ilizinduliwa na Kikwete mwaka 2009.
Hivi sasa yamebaki maghofu chakavu tu. Sifahamu ni sababu zipi zilimfanya muwekezaji ashindwe kuendeleza uwekezaji ule, ila naamini kabisa sera za uwekezaji ni changamoto Tanzania.
Uwekezaji Tanzania unategemea ni nani yupo madarakani. Hatuongozwi na sera wala sheria bali mihemko ya atakaeingia madarakani.
NB: KIROMO inawakilisha biashara nyingi zilizokufa kutokana na kukosekana kwa sera thabiti za uwekezaji.
Mungu iponye Tanzania.