Naishukuru serikali ya CCM imenipa ajira

Naishukuru serikali ya CCM imenipa ajira

"naishukuru serikali ya ccm na hasa mh rais katika hii miaka hamsini na ushehe ya uhuru,nimepata ajira.mimi ni dereva bodaboda"...nilimsikia kijana mwenzangu akiropoka,cjui alikuwa keshapewa buku 7 au ndo yuko brainwashed

hana sababu ya kushukuru,ajira ni haki yake ya KIMSINGI,labda hajui tu,na serikali yeyote dunian ni lazima ihakikishe watu wake wanakua na ajira,aidha kwa kuwaajiri,au kuwatengenezea mazingira ya wao kujiajiri
 
Ajira zingine zinakatisha wanaosoma tamaa degree holder kuwa mwendesha bodaboda securty gurd, customer care au bank taylor damn sh*t
 
hana sababu ya kushukuru,ajira ni haki yake ya KIMSINGI,labda hajui tu,na serikali yeyote dunian ni lazima ihakikishe watu wake wanakua na ajira,aidha kwa kuwaajiri,au kuwatengenezea mazingira ya wao kujiajiri

ameshatekwa akili,hajitambui.amekuwa msukule.akipewa tshirt na kofia kwishey
 
Mkuu,

Yaani nisome miaka;
7;primary
4;secondary
2;high school
5;university
Total;18

Halafu nije niendeshe BODABODA?

EXCUSE ME!!!!!!!!!!!!!!!!
Kama ndio hivyo mbona hao wanenu tuliosoma nao wanaajiriwa kwenye makampuni makubwa na kuendesha ma-range wakati walikuwa vilaza tu?

Mie niendeshe BODABODA na yule alomaliza la saba afenyaje sasa?Tunawafundisha nini wale wanafunzi wanaosoma sasa?Kuwa elimu ni ufunguo wa BODABODA!?

MSHINDWE!

mkuu umenena, ipo siku watu wa darasa la saba wataanza maandamano ya kupinga kuchukuliwa ajira zao na graduates, tujipange!!!
 
Ajira zinatangazwa kila kukicha bado mnalalamika hata hivyo serikali haiwezi kuajiri kila mwanafunzi anaemaliza chuo kikuu ndio maana tunasisitizWa kuangalia fursa nyingine katika sekta binafsi.
 
Ajira zinatangazwa kila kukicha bado mnalalamika hata hivyo serikali haiwezi kuajiri kila mwanafunzi anaemaliza chuo kikuu ndio maana tunasisitizWa kuangalia fursa nyingine katika sekta binafsi.

sawa mkuu but graduate ukafanye kibarua kiwandani kwa muhindi buku 5 kwa siku,inatosha?
 
Mimi haijalishi unasukuma mkokoteni, unaendesha bodaboda, unalima nyanya unafuga kuku, bata sungura n.k kama unaweza kuendesha maisha yako na kutatua matatizo ya hapa na pale, una afadhali sana kuliko msomi anaesubiri serikali impatie ajira.
 
mbona ndo inavyowafanyia hivyo wengine?kwanini sisi?

Umenena vema na ukishaelewa kwamba kuna "wengine" na "wewe" chukua hatua. Inamaana inawafanyia hivyo wengine ila wewe ukikaa bila kufanya chochote haitakufanyia hivyo mkuu. Na chunguza vizuri hao unaowaita wengine na madai ya kufanyiwa hivyo na elimu.
 
sawa mkuu but graduate ukafanye kibarua kiwandani kwa muhindi buku 5 kwa siku,inatosha?

kazi si lazima kufanya kwa muhindi tu vijana wasomi wanaweza kujiunga nchi hii ina rasilimali ardhi kubwa wakaitumia kupata mikopo kwenye mabenki. vijana ambao hawakwenda shule wamejikomboa sana wana bodaboda ,wamejiunga vikoba wanafanya biashara ndogondogo na maisha yanasonga mbele. tatizo vijana wasomi wanataka mafanikio ya haraka bila kuumiza kichwa mwisho wana baki kuichukia serikali na kuwa na imani upinzAni ukishika serikali ajirA Zitatolewa Kama njugu.
 
mbona ndo inavyowafanyia hivyo wengine?kwanini sisi?

ulishawahi kujiuliza ni vijana wangapi wanahitimu kila mwaka kutoka vyuo vyote nchini? umeshawahi kujiuliza uwezo wa serikali na sekta binafsi ni vijana wangapi kwa mwaka?!! Enzi zile "wasomi" walikuwa wachache, watu walikuwa wakimaliza kidato cha nne na sita ajira zinawafuata waliko, sasa hivi "wasomi" ni wengi, ukingoja ajira utashangaa unazeeka na bahasha ya khaki mkononi!
 
kazi si lazima kufanya kwa muhindi tu vijana wasomi wanaweza kujiunga nchi hii ina rasilimali ardhi kubwa wakaitumia kupata mikopo kwenye mabenki. vijana ambao hawakwenda shule wamejikomboa sana wana bodaboda ,wamejiunga vikoba wanafanya biashara ndogondogo na maisha yanasonga mbele. tatizo vijana wasomi wanataka mafanikio ya haraka bila kuumiza kichwa mwisho wana baki kuichukia serikali na kuwa na imani upinzAni ukishika serikali ajirA Zitatolewa Kama njugu.

"wasomi" watakwambia kazi za wasioenda shule!
 
ulishawahi kujiuliza ni vijana wangapi wanahitimu kila mwaka kutoka vyuo vyote nchini? umeshawahi kujiuliza uwezo wa serikali na sekta binafsi ni vijana wangapi kwa mwaka?!! Enzi zile "wasomi" walikuwa wachache, watu walikuwa wakimaliza kidato cha nne na sita ajira zinawafuata waliko, sasa hivi "wasomi" ni wengi, ukingoja ajira utashangaa unazeeka na bahasha ya khaki mkononi!

Sijui kwa nini hatutaki kukubadiliana na mabadiliko ya mfumo wa maisha, enzi hizo kijijini baba yangu na baba mdogo ndio walikua wamemaliza darasa laba kijiji kizima na zikaja nafasi za ualimu baba akaenda kusoma na kuajiriwa ualimu ikafuatiwa na nafasi za mafunzo ya uaskari baba mdogo nae akaenda chuo cha polisi Moshi, wakiwa huko kwenye mafunzo vita ya Uganda ikaanza wakapelekwa huko na aliporudi nafikiri hapakua na haja ya kuendelea tena na mafunzo kwa sababu alikua amefuzu zaidi ya mafunzo aliyostahili kujifunza chuoni, akaenda moja kwa moja kwenye ajira.

mazingira yetu sasa hivi yako tofauti sana, hata pale unapotaka kusomea fani au ujuzi wa aina flani unajiuliza mara mbilimbili, nje ya ajira hichi nnachotaka kujifunza ntakitumiaje kunisaidia kuingiza kipato na kuendesha mambo yangu? zile enzi za kusoma kisha unakaa unatulia ukisubiri ajira zilikwisha kitambo! Thanks mkuu
 
ulishawahi kujiuliza ni vijana wangapi wanahitimu kila mwaka kutoka vyuo vyote nchini? Umeshawahi kujiuliza uwezo wa serikali na sekta binafsi ni vijana wangapi kwa mwaka?!! Enzi zile "wasomi" walikuwa wachache, watu walikuwa wakimaliza kidato cha nne na sita ajira zinawafuata waliko, sasa hivi "wasomi" ni wengi, ukingoja ajira utashangaa unazeeka na bahasha ya khaki mkononi!

umesema vema mkuu,but serikali ina wajibu wa kuandaa mazingira ya ajira.ni miaka sasa hatuna ajira mpya,yaani zilizopo ni zile zile,wakati nchi ina rasilimali za kutosha.kwanini zisitumike kupanua wigo wa ajira.tunajua kuwa serikali na secta binafsi haviwezi kuajiri kila mtu but kuna mazingira ambayo yanafanywa ili kutengeneza ajira.imagine,kuna bilions ngapi uswizi?zisingeweza kufufua viwanda hata vitatu?vingetoa ajira kiasi gani kwa vijana?kila kinacholipa kinabinafsishwa kiujanja ujanja
 
Back
Top Bottom