Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,903
- 945
Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile amefanya ziara kutembelea reli ya kati kujionea hali ya uharibifu uliojitokea baada mvua kunyesha kuanzia January 25 mwaka huu.
Mhe. Naibu Waziri akiwa kwenye Kiberenge ameanzia ziara katika eneo la Lukobe Manispaa ya Morogoro, Munisagara na Mzangaza Wilaya ya Kilosa na Gulwe Wilaya Mpwawa mkoani Dodoma ambapo ameambata na Wataalamu kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC)
Mhe. Kihenzile amejionea hali ya uharibifu wa Reli ya kati maji kujaa kwenye Reli sehemu ya Mzangaza ikisombwa maji ambapo tayari mafundi wameanza kazi ya kurejesha miundombunu hiyo katika maeneo yote yaliyoathirika Ili usafiri kupitia treni hiyo uweze kurudi baada ya kusitishwa tangu mwishoni mwa mwezi January.
Mhe. Naibu Waziri akiwa kwenye Kiberenge ameanzia ziara katika eneo la Lukobe Manispaa ya Morogoro, Munisagara na Mzangaza Wilaya ya Kilosa na Gulwe Wilaya Mpwawa mkoani Dodoma ambapo ameambata na Wataalamu kutoka Shirika la Reli Tanzania (TRC)
Mhe. Kihenzile amejionea hali ya uharibifu wa Reli ya kati maji kujaa kwenye Reli sehemu ya Mzangaza ikisombwa maji ambapo tayari mafundi wameanza kazi ya kurejesha miundombunu hiyo katika maeneo yote yaliyoathirika Ili usafiri kupitia treni hiyo uweze kurudi baada ya kusitishwa tangu mwishoni mwa mwezi January.