Naibu Waziri Kihenzile: Miradi itekelezwe kwa kuzingatia Muda na Thamani ya Fedha

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,908
945

NAIBU WAZIRI KIHENZILE: MIRADI ITEKELEZWE KWA KUZINGATIA MUDA NA THAMANI YA FEDHA

F8Flm9QXgAAgSs4.jpg

"Nawapongeza Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kwa kuweka taa katika uwanja wa ndege wa Dodoma, uwanja huu kwa ripoti kutoka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) inaonesha unashika nafasi ya 4 kwa kuhudumia abiria wengi, nina imani maboresho yakifanyika utapanda zaidi kutoka nafasi hiyo na sababu kubwa ni kwamba Dodoma kuna idadi kubwa ya watu hivi sasa" - Mhe. David Kihenzile, Naibu Waziri wa Uchukuzi.

F8FlnckW4AEaGB0.jpg

"Miradi yote inayotekelezwa katika Wizara ya Uchukuzi sharti mojawapo ni kwamba ni lazima izingatie muda. Kama mradi unapaswa kukamilika ndani ya miezi 6 hakikisheni unakamilika ndani ya miezi 6. Serikali haiko tayari kuvumilia uzembe, sababu wala visingizio lakini pia miradi hiyo izingatie thamani ya fedha" - Mhe. David Kihenzile, Naibu Waziri wa Uchukuzi.

F8FlmwCXgAA4p6m.jpg
F8Flm9QXgAAgSs4.jpg
F8FlnckW4AEaGB0.jpg
F8Fln-yWcAAC-6M.jpg
 
Back
Top Bottom