Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,194
- 1,041
Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) imepanga kujenga matenki ya kuhifadhi mafuta (Farm Tanks) yenye uwezo wa kuhifadhi tani 360,000 kwa wakati mmoja ili kufanya Meli za mafuta zisikae bandarini muda mrefu hivyo kuongeza ufanisi na kupunguza gharama kwa wateja.
Hayo yamebainika Septemba 26, 2023 wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile katika bandari ya Dar-es-Salaam.
Mhe. Kihenzile ametembelea eneo yatakapojengwa matenki ya kuhifadhi mafuta, eneo la kuhifadhi mizigo inayoharibika (perishable goods), Gati la Mafuta (KOJ), Gati Na. 1-7, Gati la Magari na Gati la Meli za kwenda Zanzibar na Visiwa vya Comoro.
Mhe. Kihenzile ameipongeza Menejimenti ya TPA na kuitaka kusimamia miradi kikamilifu ili ikamilike kwa wakati, pamoja na kuhakikisha thamani ya uwekezaji (value for money) inapatikana.
Mhemishiwa Naibu Waziri alikuwa katika ziara yake ya kwanza TPA kufuatia uteuzi wake katika nafasi hiyo hivi karibuni.
Hayo yamebainika Septemba 26, 2023 wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Uchukuzi Mhe. David Kihenzile katika bandari ya Dar-es-Salaam.
Mhe. Kihenzile ametembelea eneo yatakapojengwa matenki ya kuhifadhi mafuta, eneo la kuhifadhi mizigo inayoharibika (perishable goods), Gati la Mafuta (KOJ), Gati Na. 1-7, Gati la Magari na Gati la Meli za kwenda Zanzibar na Visiwa vya Comoro.
Mhe. Kihenzile ameipongeza Menejimenti ya TPA na kuitaka kusimamia miradi kikamilifu ili ikamilike kwa wakati, pamoja na kuhakikisha thamani ya uwekezaji (value for money) inapatikana.
Mhemishiwa Naibu Waziri alikuwa katika ziara yake ya kwanza TPA kufuatia uteuzi wake katika nafasi hiyo hivi karibuni.