Nahitaji Ushauri hii kwa wanaume wenzangu tu

Nahitaji Ushauri hii kwa wanaume wenzangu tu

jamaa hakuwa vizuri kifedha kama mimi, yaaani mimi naingia kwake mara 10
Wewe unaingia kwake mara 10? yani wewe x10 ndie yeye..

Ndio maana umefeli kwa uyo mtoto japo unaumri mkubwa..

Demu akichakuweka kwenye friend zone uchomoki..

Nadhani umetuuzi wengi tu kitendo cha wewe ku-spy ma-boyfriends wake, always be yourself..
 
Kila mtu ana shida a kimapenzi, leo nimeona nielezee za kwangu
Nina rafiki yangu wa kike, rafiki wa mda mrefu nahisi miaka mitano. Tumekuwa marafiki sana ila nimetokea kumpenda bila ye kujua. Nimekuwa rafiki yake muda mrefu na nachopendea toka kwake, hana tamaa (kwao wapo vizuri sana baba ana kampuni ya kilimo kubwa tu tanzania na vyeo kede kede) ni mcha Mungu kanisani hakosi na ana akili balaa yani yupo smart sana kichwani sio kama wanawake wengine, mnaweza mkakaa msichana akakuchambulia uchumi wa urusi mpaka marekani china yaani humdanganyi, pia ni mtafutaji balaa. Huyu dada kawa rafiki yangu miaka takribani 5, hajawahi kuniomba hela hata siku moja na nikimnunulia wine kesho ananinulia bia kwa kweli me nimemwona wife material yuko very caring pia mkienda sehemu akinunua kitu lazima na wewe akununulie. Ila shida moja tu, huyu msichana ana penda watu wasiompenda , alikuwa na uhusiano na jamaa flani rubani mlalahoi kwa kumwona tu jamaa mtandaoni nikajua huyu jamaa ni wa kupita tu. kujisikia sana maisha ya kificho ficho mno na alikuwa hajiamini kwa huyo mwanamke ka jinsi rafiki yangu alivyokuwa ananisimulia. Alimfanyia vituko vingi sana huyu binti na iliniuma maana nilikuwa najua huyo ndo bwana wake wa pili tu tangu aanze kujihusisha na mahusiano yani alikuwa fresh kabisa kwa mchezo wa mapenzi jamaa wake wa awali alikuwa mlevi na alikuwa akilewa anampiga waliachana baada miezi 6 tu, na binti ni mdogo bado, mwaka huu ana 23 kama sio 24 nimemjua toka anamaliza chuo akiwa na miaka 19, basi wakaachana na huyo jamaa rubani mlalahoi nikajua yes nimepata sasa wakati wangu wa kumuinga mara bin vuuup jamaa wakarudiana. nikaamuuliza vipi tena? akasema amemsamehe kwa yote na amebadilika. Basi mi nikafanya uchunguzi mdogo tu nikagundua jamaa ana mwanamke mwingine ana mimba yake na kamuahidi ndoa (nilimuona facebook nikamdadisi huyu mwanamke wa rubani mlalahoi mpaka instagram) nikamwonesha huyu binti ila cha kushangaza akaacha kuongea namimi akaweka vipicha vya jamaa wake instagram ikaniuma sana ila sikufanya lolote, nikaendelea kumdadisi huyo mischana wa jamaa mpaka akaniblock (nadhani niliblow my cover au demu alimwambia jamaa). Basi hatukuongea tena. Baadae nikaja kusikia wameachana na jamaa kaoa tayari mwanamke mwingine ( in a span of 3 months baada ya kuachana jamaa kaoa). Maskini huyu binti hakuwa vizuri aliachana kabisa na mapenzi hata nikimtamfuta anasema hayupo tayari kwa mapenzi kwani haamini tena wanaume. Cha kunishangaza yani ni mzuri mno sura shepu figa mzuri wa roho na ni mcheshi haswa huwezi boreka hata chembe ukikaa nae, kwanini kuwakibmbilia wasiompenda? Nimpataje huyu bidada maana nimeoza kwake na ye ndo hataki kabisa mapenzi, kahama kabisa na mkoa anafanya biashara maeneo tofauti, ana mashamba mafinga, ana nyumba za kupanga dodoma, ana biashara nyingine mbeya yani ni mtafutaji ila nashindwa kabisa jinsi ya kumuingia.

update
nimejaribu mbinu nyingi, nimeshawahi mkatia ticket twende serengeti huko tukashangae nikijua binti atakubali ila waaaapi. Kila nachofanya anadecline, wenzangu nipeni mawazo
[emoji121]
IKISHAANDIKWA VEMA KWA KUZINGATIA AYA
NA KAIDA ZA UANDISHI
NITAKUJA KUTOA USHAURI WA KIMATAIFA!
 
Umesema alikua ba rubani mlala hoi...Ru serious...watu wanasema marubani ndo wanapesa vipi anakua mlalahoi.ufafanuzi plz
Mkuu marubani hawana pesa kama unavofikiri. huwezi walingnisha na sisi wafanyabiashara, kipato chao kwa mwezi ni kam kipato cha wiki ha mfanyabiashara. usitishike
 
Mkuu marubani hawana pesa kama unavofikiri. huwezi walingnisha na sisi wafanyabiashara, kipato chao kwa mwezi ni kam kipato cha wiki ha mfanyabiashara. usitishike
Nmekupata mkuu
 
Shyeeeh...!!! Umefanya uzembe, 5 years ungekuwa ushai-graduetisha dudu kwa kuivalisha ndox.

Ona sasa umeishia kuwa mpenzi mtazamaji.
 
Wewe mwenyewe inaonekana muoga...kwa miaka mitano uliomfahamu umeshindwa kumtangazia hisia zako?? Pole sana.. Keep trying May be someday the sun will shine on you..
 
Kama hiyo dada ulimjua akiwa amesha maliza chuo akiwa na umri wa miaka 19..[emoji15] [emoji15]
Hebu ngoja tuanze hesabu kwanza kabla sija kushauri.

19 toa miaka 4 ya chuo = 16
16 toa miaka 2 ya A- level = 14
14 toa miaka 4 ya O-level = 10
10 toa miaka 7 ya primary= 3

Kwahivyo, huyo Rafiki yako alianza shule akiwa na umri wa miaka miaka 3..[emoji23] [emoji23]
Minawaza kwa sauti tu
[emoji125] [emoji125] [emoji125]
 
Kama hiyo dada ulimjua akiwa amesha maliza chuo akiwa na umri wa miaka 19..[emoji15] [emoji15]
Hebu ngoja tuanze hesabu kwanza kabla sija kushauri.

19 toa miaka 4 ya chuo = 16
16 toa miaka 2 ya A- level = 14
14 toa miaka 4 ya O-level = 10
10 toa miaka 7 ya primary= 3

Kwahivyo, huyo Rafiki yako alianza shule akiwa na umri wa miaka miaka 3..[emoji23] [emoji23]
Minawaza kwa sauti tu
[emoji125] [emoji125] [emoji125]
Alianza shule akiwa na miaka nne international school na hakuenda darasa la saba wala form 5 na six. Pia kasoma nje. Ni kitu cha kawaida sana ukiangalia sasa ivi watoto miaka 2 wanaanza daycare wana miaka 2
 
ebhanae safar hio uliianzia mguu wa kushoto , ulishakosea sana kumfanya shosti yako, daima mwanamke akishakufanya rafiki yake hautaona ndani , hii kitu ya kuitwa friendzone isikie tu isikukute
 
Tatizo
19 years kamaliza chuo?????
Watanzania wengi tunachelewa kuanza shule. Binti alianza shule miaka 4. Tena hio miaka 19 alivyomaliza alianza kufanya biashara zake kabisa
 
ebhanae safar hio uliianzia mguu wa kushoto , ulishakosea sana kumfanya shosti yako, daima mwanamke akishakufanya rafiki yake hautaona ndani , hii kitu ya kuitwa friendzone isikie tu isikukute
Daah mkuu kati ya wote wewe ndo umesikia maumivu yangu
 
Mkuu marubani hawana pesa kama unavofikiri. huwezi walingnisha na sisi wafanyabiashara, kipato chao kwa mwezi ni kam kipato cha wiki ha mfanyabiashara. usitishike
Mkuu lazima utakuwa ni mfanyabiashara mkubwa sana, nna mshkaji wangu ni rubani hapahapa tz na bado hana flying hours za kutosha sana lakini analipwa zaidi ya US$ 6000 kwa mwezi nimeshangaa kidogo unapowaita marubani walalahoi
 
Daah mkuu kati ya wote wewe ndo umesikia maumivu yangu
hio hali ishawah kunikuta mkuu ,, nilifurukuta nnavoweza lakini sikuona ndani , mwishoe hata urafiki nikapiga chini nikaona bora nikose vyote,, maana ukikaa nae karbu utazid kujitesa na kuna raia zitakuwa zinamuumiza kaz yako itakuwa kubembeleza tu bob
 
Mkuu kampuni gani. Maaana kama mlipaji mkubwa kwa aviation tz ni fj na analipa 4500 ..huyo anafanya wapi
Mkuu lazima utakuwa ni mfanyabiashara mkubwa sana, nna mshkaji wangu ni rubani hapahapa tz na bado hana flying hours za kutosha sana lakini analipwa zaidi ya US$ 6000 kwa mwezi nimeshangaa kidogo unapowaita marubani walalahoi
 
Mkuu kampuni gani. Maaana kama mlipaji mkubwa kwa aviation tz ni fj na analipa 4500 ..huyo anafanya wapi
KLM mkuu, hiyo unayosema mbona ni ya line maintenance engineers na hapo bado inategemeana na leseni alizonazo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom