Nahitaji simu (Google pixel 9 a/pro)

Nahitaji simu (Google pixel 9 a/pro)

888I

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
461
Reaction score
575
Wanajamvi nahitaji simu aina hiyo sasa kila nikipita mitandaoni nakutana na matangazo Cha ajabu Bei ni Chee kweli kweli Hadi zinanitisha mara Tsh 400k mara 350k nikiwasiliana nao wananieleza lipia nusu ukipokea mzigo unakamilisha nimewachek watatu Hadi sasa na wote ujumbe ni huo. This deal is too good to be true

Nakuuliza ndiyo utapeli mpya ama ni halisi ?
 
Wanajamvi nahitaji simu aina hiyo sasa kila nikipita mitandaoni nakutana na matangazo Cha ajabu Bei ni Chee kweli kweli Hadi zinanitisha mara Tsh 400k mara 350k nikiwasiliana nao wananieleza lipia nusu ukipokea mzigo unakamilisha nimewachek watatu Hadi sasa na wote ujumbe ni huo ...this deal is too good to be true

Nakuuliza ndiyo utapeli mpya ama ni halisi ?
Wako chakechake Zanzibar?😄😄Andaa maumivu
 
Jichanganye uchanganywe kama zege
Atalia muda sio mrefu. Kuna shemeji yangu alitaka kukopa Kuna watu wanaitwa TALA! Wakamwambia atume deposit laki nne ili wamkopeshe milioni 4!

Alivyotuma tu hakuwaona tena. Na police hawana msaada TZ fraud nje nje, ukifika police na wao wanataka yaani ni kukamuliwa kama ngombe
 
Atalia muda sio mrefu. Kuna shemeji yangu alitaka kukopa Kuna watu wanaitwa TALA! Wakamwambia atume deposit laki nne ili wamkopeshe milioni 4!

Alivyotuma tu hakuwaona tena. Na police hawana msaada TZ fraud nje nje, ukifika police na wao wanataka yaani ni kukamuliwa kama ngombe
Sijui mtu unakua na ujinga wa kiasi gani utume 400k ili eti wao wakutumie 4m. Swali rahisi si wakutumie 3.6m?
 
Simu zimepigwa bandarini ni nzima na nzuri ila Kwa ushahuri waulize wapo wapi? Na kama unaweza nenda kakabidhiane mkono Kwa mkono itakuwa vyema

Nimesoma koment ya mmoja hapo anasema wapo chakechake, yeah wengi wenye biashara hiyo ni wa Zanzibar na ikitokea wamekuuzia simu na ikazingua wanakubadilishia yaani wanakupa na guarantee

Fika mahali husika ukabidhiane Mali Kwa Mali , usitume na ya kutolea
 
Nchi haiishi wajinga hii. Na moja ya wajinga hao ni wewe. Ngoja utapeliwe ndio akili ikukae sawa.
 
Ni wezi hao simu ya 2.3m wakuuzie laki nne aisee watu mnatafuta sehemu za kupoteza hela kirahisi ili mje kuanzisha nyuzi..
 
Simu zimepigwa bandarini ni nzima na nzuri ila Kwa ushahuri waulize wapo wapi? Na kama unaweza nenda kakabidhiane mkono Kwa mkono itakuwa vyema

Nimesoma koment ya mmoja hapo anasema wapo chakechake, yeah wengi wenye biashara hiyo ni wa Zanzibar na ikitokea wamekuuzia simu na ikazingua wanakubadilishia yaani wanakupa na guarantee

Fika mahali husika ukabidhiane Mali Kwa Mali , usitume na ya kutolea
Eti Google Pixel 9 imepigwa bandarini. Hayo yamekuwa marobota ya mitumba?

Simu ya less than 350g package nzima, ikiwa used haifiki robo kilo na bei yake ni zaidi ya milioni moja. Na iko delicate kupasuka kioo, ndio upakie kwenye kontena?
 
Nafikiri mnawasiliana, vipi ukipiga hatua hadi huko kwao uwape pesa wakupe simu urudi home kuliko kurisk kisichoeleweka ndugu. Coz kama sio matapeli watakwambia walipo uende huko lakini wakikwambia haina haja uende wao ni kutuma tu iyo hela tunza tu itakusaidia kwingne
 
Unahamasisha mtu aibiwe mazee inakuaje unaweza kutuma picha ya hiyo simu unayoitumia hapa ukiwa umefungua sehemu ya mafaili hapa sio ya kudownload..
Sasa mzee kama mtu ana akili zake timamu anashindwa kujua anakwenda kupigwa mm nifanyaje, Acha apigwe tuu hata hao matapeli wana familia.

Mtu anajua kabisa simu inauzwa sio chini ya 1m, amepata sehemu huko hiyo hiyo simu inauzwa 400k na anaambiwa atume pesa na yeye anaona fresh tuu sasa unataka kumshauri nn huyu?
 
Sasa mzee kama mtu ana akili zake timamu anashindwa kujua anakwenda kupigwa mm nifanyaje, Acha apigwe tuu hata hao matapeli wana familia.

Mtu anajua kabisa simu inauzwa sio chini ya 1m, amepata sehemu huko hiyo hiyo simu inauzwa 400k na anaambiwa atume pesa na yeye anaona fresh tuu sasa unataka kumshauri nn huyu?
Haujaandika kitu cha maana kabisa mazee nimeomba picha ya simu unayotumia maana umesema upo nayo goggle pixel 256 Gb kwa laki kadhaa kwa msisitizo umesema umetuma hela mara mbili ili kuipata baadae unakuja na maelezo ya uongo...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom